Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SWALI LA 6

Biblia Ilitabiri Nini Kumhusu Masihi?

UNABII

“Wewe, Ee Bethlehemu Efratha, . . . kutoka kwako atatoka kwa ajili yangu yule atakayekuwa mtawala katika Israeli.”

Mika 5:2

UTIMIZO

“Baada ya Yesu kuzaliwa huko Bethlehemu ya Yudea katika siku za Mfalme Herode, tazama! wanajimu kutoka Mashariki walikuja Yerusalemu.”

Mathayo 2:1

UNABII

“Wanagawana mavazi yangu, nao wanalipigia kura vazi langu.”

Zaburi 22:⁠18

UTIMIZO

“Baada ya wanajeshi kumtundika Yesu kwenye mti, wakachukua mavazi yake ya nje na kuyagawanya vipande vinne . . . Lakini vazi la ndani halikuwa na mshono, lilikuwa limefumwa kutoka juu mpaka chini. Basi wakaambiana: ‘Tusilirarue, badala yake tupige kura ili tuamue litakuwa la nani.’”

Yohana 19:​23, 24

UNABII

“Anailinda mifupa yake yote; Haujavunjwa hata mmoja.”

Zaburi 34:⁠20

UTIMIZO

“Walipomfikia Yesu, waliona kwamba tayari amekufa, kwa hiyo hawakuivunja miguu yake.”

Yohana 19:⁠33

UNABII

“Alichomwa kwa sababu ya makosa yetu.”

Isaya 53:5

UTIMIZO

“Mwanajeshi mmoja akauchoma ubavu wa Yesu kwa mkuki, na mara moja damu na maji vikatoka.”

Yohana 19:⁠34

UNABII

“Wakanilipa mshahara wangu, vipande 30 vya fedha.”

Zekaria 11:​12, 13

UTIMIZO

“Ndipo mmoja wa wale 12, aliyeitwa Yuda Iskariote, akaenda kwa wakuu wa makuhani na kuwauliza: “Mtanipa nini ili nimsaliti kwenu?” Wakakubaliana naye vipande 30 vya fedha.”

Mathayo 26:​14, 15; 27:​5