Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kitabu cha Ayubu

Sura

Muhtasari wa Yaliyomo

  • 1

    • Utimilifu wa Ayubu na mali zake (1-5)

    • Shetani atilia shaka nia ya Ayubu (6-12)

    • Ayubu apoteza mali na watoto wake (13-19)

    • Ayubu hamlaumu Mungu (20-22)

  • 2

    • Shetani atilia shaka tena nia ya Ayubu (1-5)

    • Shetani aruhusiwa kugusa mwili wa Ayubu (6-8)

    • Mke wa Ayubu: “Mtukane Mungu, ufe!” (9, 10)

    • Ayubu atembelewa na marafiki watatu (11-13)

  • 3

    • Ayubu ajuta kuzaliwa (1-26)

      • Auliza kwa nini anateseka (20, 21)

  • 4

    • Elifazi azungumza kwa mara ya kwanza (1-21)

      • Adhihaki utimilifu wa Ayubu (7, 8)

      • Asimulia ujumbe kutoka kwa kiumbe wa roho (12-17)

      • ‘Mungu hana imani na watumishi wake’ (18)

  • 5

    • Elifazi aendelea kuzungumza (1-27)

      • ‘Mungu huwanasa wenye hekima katika ujanja wao’ (13)

      • ‘Ayubu hapaswi kukataa nidhamu ya Mungu’ (17)

  • 6

    • Jibu la Ayubu (1-30)

      • Adai kwamba ana sababu ya kulia (2-6)

      • Wafariji wake ni wenye hila (15-18)

      • “Maneno ya unyoofu hayaumizi!” (25)

  • 7

    • Ayubu aendelea kujibu (1-21)

      • Maisha ni kama kazi ya kulazimishwa (1, 2)

      • “Kwa nini umenifanya niwe shabaha yako?” (20)

  • 8

    • Bildadi azungumza kwa mara ya kwanza (1-22)

      • Adai kwamba watoto wa Ayubu wametenda dhambi (4)

      • ‘Ikiwa ungekuwa safi, Mungu angekulinda’ (6)

      • Adai kwamba Ayubu amemkataa Mungu (13)

  • 9

    • Jibu la Ayubu (1-35)

      • Mwanadamu anayeweza kufa hawezi kushindana na Mungu (2-4)

      • ‘Mungu hufanya mambo yasiyochunguzika’ (10)

      • Mtu hawezi kubishana na Mungu (32)

  • 10

    • Ayubu aendelea kujibu (1-22)

      • ‘Kwa nini Mungu anapambana nami?’ (2)

      • Mungu si kama Ayubu anayeweza kufa (4-12)

      • ‘Naomba nipate kitulizo kidogo’ (20)

  • 11

    • Sofari azungumza kwa mara ya kwanza (1-20)

      • Amshutumu Ayubu kwa sababu ya maneno yake yasiyo na maana (2, 3)

      • Amwambia Ayubu aache uovu (14)

  • 12

    • Jibu la Ayubu (1-25)

      • “Mimi si duni kwenu” (3)

      • “Nimekuwa kichekesho” (4)

      • ‘Mungu ana hekima’ (13)

      • Mungu ni mkuu kuliko waamuzi na wafalme (17, 18)

  • 13

    • Ayubu aendelea kujibu (1-28)

      • ‘Ni afadhali nizungumze na Mungu’ (3)

      • ‘Ninyi ni matabibu wasiofaa kitu’ (4)

      • “Najua sina kosa” (18)

      • Auliza kwa nini Mungu anamwona kuwa adui (24)

  • 14

    • Ayubu aendelea kujibu (1-22)

      • Maisha ya mwanadamu ni mafupi na yamejaa taabu (1)

      • “Hata mti una tumaini” (7)

      • “Laiti ungenificha Kaburini!” (13)

      • “Mtu akifa, je, anaweza kuishi tena?” (14)

      • Mungu ataitamani sana kazi ya mikono yake (15)

  • 15

    • Elifazi azungumza kwa mara ya pili (1-35)

      • Adai kwamba Ayubu hamwogopi Mungu (4)

      • Asema Ayubu ana kimbelembele (7-9)

      • ‘Mungu hana imani na watakatifu wake’ (15)

      • ‘Anayeteseka ni mwovu’ (20-24)

  • 16

    • Jibu la Ayubu (1-22)

      • ‘Ninyi ni wafariji wasumbufu!’ (2)

      • Adai kwamba Mungu anamfanya kuwa shabaha yake (12)

  • 17

    • Ayubu aendelea kujibu (1-16)

      • “Wadhihaki wananizunguka” (2)

      • “Amenifanya niwe kitu cha kudharauliwa” (6)

      • “Kaburi litakuwa makao yangu” (13)

  • 18

    • Bildadi azungumza kwa mara ya pili (1-21)

      • Aeleza yatakayowapata waovu (5-20)

      • Adai Ayubu hamjui Mungu (21)

  • 19

    • Jibu la Ayubu (1-29)

      • Akataa kukemewa na “rafiki” zake (1-6)

      • Asema kwamba ameachwa (13-19)

      • “Mkombozi wangu yuko hai” (25)

  • 20

    • Sofari azungumza kwa mara ya pili (1-29)

      • Adai kwamba Ayubu amemtukana (2, 3)

      • Adai kwamba Ayubu ni mwovu (5)

      • Adai kwamba Ayubu anafurahia dhambi (12, 13)

  • 21

    • Ayubu ajibu (1-34)

      • ‘Kwa nini waovu wanafanikiwa?’ (7-13)

      • Afichua hila za “wafariji” wake (27-34)

  • 22

    • Elifazi azungumza kwa mara ya tatu (1-30)

      • ‘Mwanadamu ana faida gani kwa Mungu?’ (2, 3)

      • Adai kwamba Ayubu ni mwenye pupa na hatendi haki (9)

      • ‘Mrudie Mungu, utarudishiwa hali njema’ (23)

  • 23

    • Ayubu ajibu (1-17)

      • Ataka kupeleka kesi yake mbele za Mungu (1-7)

      • Asema kwamba hampati Mungu (8, 9)

      • “Nimefuata njia yake bila kukengeuka” (11)

  • 24

    • Ayubu aendelea kujibu (1-25)

      • ‘Kwa nini Mungu haweki wakati wa hukumu?’ (1)

      • Asema kwamba Mungu ameruhusu uovu (12)

      • Watenda dhambi wanapenda giza (13-17)

  • 25

    • Bildadi azungumza kwa mara ya tatu (1-6)

      • ‘Mwanadamu anawezaje kuwa bila hatia mbele za Mungu?’ (4)

      • Adai kwamba utimilifu wa mwanadamu ni wa bure (5, 6)

  • 26

    • Ayubu ajibu (1-14)

      • “Jinsi mlivyomsaidia mtu asiye na uwezo!” (1-4)

      • ‘Mungu anaining’iniza dunia mahali pasipo na kitu’ (7)

      • ‘Ni kingo tu za njia za Mungu’ (14)

  • 27

    • Ayubu aazimia kuendelea kuwa mtimilifu (1-23)

      • “Sitaukana utimilifu wangu” (5)

      • Anayemkataa Mungu hana tumaini (8)

      • “Kwa nini mazungumzo yenu hayana maana yoyote?” (12)

      • Mtu mwovu habaki na chochote (13-23)

  • 28

    • Ayubu aonyesha tofauti iliyopo kati ya hazina za dunia na hekima (1-28)

      • Jitihada za wanadamu za kuchimba madini (1-11)

      • Hekima ina thamani kuliko lulu (18)

      • Kumwogopa Yehova ndiyo hekima ya kweli (28)

  • 29

    • Ayubu akumbuka maisha mazuri aliyokuwa nayo kabla ya mateso (1-25)

      • Aliheshimiwa kwenye lango la jiji (7-10)

      • Jinsi alivyokuwa akitenda haki awali (11-17)

      • Kila mtu alisikiliza ushauri wake (21-23)

  • 30

    • Ayubu aeleza jinsi maisha yake yalivyobadilika (1-31)

      • Adhihakiwa na watu wasiofaa kitu (1-15)

      • Hakusaidiwa na wengine (20, 21)

      • “Ngozi yangu imekuwa nyeusi” (30)

  • 31

    • Ayubu atetea utimilifu wake (1-40)

      • “Agano na macho yangu” (1)

      • Aomba Mungu ampime (6)

      • Hakuwa mzinzi (9-12)

      • Hakupenda pesa (24, 25)

      • Hakuabudu sanamu (26-28)

  • 32

    • Kijana Elihu ajiunga na mazungumzo (1-22)

      • Amkasirikia Ayubu na rafiki zake (2, 3)

      • Alisubiri kwa heshima kabla ya kuzungumza (6, 7)

      • Umri peke yake haumfanyi mtu awe na hekima (9)

      • Elihu atamani kuongea (18-20)

  • 33

    • Elihu amkaripia Ayubu kwa sababu ya kujiona kuwa mwadilifu (1-33)

      • Fidia yapatikana (24)

      • Kurudia nguvu za ujana (25)

  • 34

    • Elihu atetea haki ya Mungu na njia zake (1-37)

      • Ayubu asema kwamba Mungu alimnyima haki (5)

      • Mungu wa kweli hawezi kamwe kutenda uovu (10)

      • Ayubu hana ujuzi (35)

  • 35

    • Elihu ataja mawazo yasiyofaa ya Ayubu (1-16)

      • Ayubu asema yeye ni mwadilifu kuliko Mungu (2)

      • Mungu yuko juu sana, haathiriwi na dhambi (5, 6)

      • Ayubu anapaswa kumngojea Mungu (14)

  • 36

    • Elihu autukuza ukuu wa Mungu usiochunguzika (1-33)

      • Wanaotii wanafanikiwa; wanaomkataa Mungu wanakataliwa (11-13)

      • ‘Ni nani aliye mfundishaji kama Mungu?’ (22)

      • Ayubu anapaswa kumtukuza Mungu (24)

      • “Mungu ni mkuu kuliko tunavyoweza kujua” (26)

      • Mungu hudhibiti mvua na radi (27-33)

  • 37

    • Nguvu za asili zinafunua ukuu wa Mungu (1-24)

      • Mungu anaweza kusimamisha shughuli za wanadamu (7)

      • ‘Tafakari kazi za Mungu zinazostaajabisha’ (14)

      • Wanadamu hawawezi kumwelewa Mungu (23)

      • Hakuna mwanadamu anayepaswa kufikiri kwamba ana hekima (24)

  • 38

    • Yehova afundisha kuhusu udogo wa mwanadamu (1-41)

      • ‘Ulikuwa wapi nilipoiumba dunia?’ (4-6)

      • Wana wa Mungu walishangilia kwa sauti (7)

      • Maswali kuhusu matukio ya asili (8-32)

      • “Sheria zinazoongoza mbingu” (33)

  • 39

    • Uumbaji wa wanyama waonyesha ujinga wa mwanadamu (1-30)

      • Mbuzi wa milimani na paa (1-4)

      • Punda mwitu (5-8)

      • Fahali mwitu (9-12)

      • Mbuni (13-18)

      • Farasi (19-25)

      • Kipanga na tai (26-30)

  • 40

    • Yehova amuuliza maswali zaidi (1-24)

      • Ayubu akiri hana la kusema (3-5)

      • “Je, utatilia shaka haki yangu?” (8)

      • Mungu aeleza kuhusu nguvu za Behemothi (15-24)

  • 41

    • Mungu aeleza kuhusu Lewiathani anayestaajabisha (1-34)

  • 42

    • Ayubu amjibu Yehova (1-6)

    • Rafiki watatu wa Ayubu washutumiwa (7-9)

    • Yehova ambariki tena Ayubu (10-17)

      • Wana na mabinti wa Ayubu (13-15)