Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kitabu cha Zaburi

Sura

Muhtasari wa Yaliyomo

  • 1

    • Njia mbili zatofautishwa

      • Kusoma sheria ya Mungu huleta furaha (2)

      • Waadilifu ni kama mti unaozaa matunda kwa wingi (3)

      • Waovu ni kama makapi yanayopeperushwa mbali (4)

  • 2

    • Yehova na mtiwa-mafuta wake

      • Yehova anayacheka mataifa (4)

      • Yehova amweka mfalme wake (6)

      • Mheshimuni mwana (12)

  • 3

    • Kumtumaini Mungu licha ya hatari

      • ‘Kwa nini maadui wamekuwa wengi sana?’ (1)

      • “Wokovu ni wa Yehova” (8)

  • 4

    • Sala ya kumtumaini Mungu

      • “Kasirika, lakini usitende dhambi” (4)

      • ‘Nitalala usingizi kwa amani’ (8)

  • 5

    • Yehova ni kimbilio la mwadilifu

      • Mungu anachukia uovu (4, 5)

      • ‘Niongoze katika uadilifu wako’ (8)

  • 6

    • Ombi la kupata kibali

      • Waliokufa hawamsifu Mungu (5)

      • Mungu husikia sala za kuomba kibali (9)

  • 7

    • Yehova ni Mwamuzi mwadilifu

      • “Nihukumu, Ee Yehova” (8)

  • 8

    • Utukufu wa Mungu na heshima ya mwanadamu

      • “Jinsi jina lako lilivyo kuu!” (1, 9)

      • ‘Mwanadamu anayeweza kufa ana faida gani?’ (4)

      • Mwanadamu avikwa taji la fahari (5)

  • 9

    • Kutangaza kazi za Mungu zinazostaajabisha

      • Yehova ni kimbilio salama (9)

      • Kulijua jina la Mungu humaanisha kumtumaini yeye (10)

  • 10

    • Yehova ni msaidizi wa wasio na uwezo

      • Mwovu hujigamba: “Hakuna Mungu” (4)

      • Wasio na uwezo humgeukia Yehova (14)

      • “Yehova ni Mfalme milele” (16)

  • 11

    • Kumkimbilia Yehova

      • “Yehova yumo katika hekalu lake takatifu” (4)

      • Mungu humchukia yeyote anayependa ukatili (5)

  • 12

    • Yehova ainuka ili kutenda

      • Maneno ya Mungu ni safi (6)

  • 13

    • Kutamani wokovu wa Yehova

      • ‘Mpaka lini, Ee Yehova?’ (1, 2)

      • Yehova huthawabisha kwelikweli (6)

  • 14

    • Ufafanuzi kumhusu mpumbavu

      • “Hakuna Yehova” (1)

      • “Hakuna yeyote anayetenda mema” (3)

  • 15

    • Ni nani anayeweza kuwa mgeni katika hema la Yehova?

      • Husema ukweli moyoni mwake (2)

      • Hachongei (3)

      • Hutimiza ahadi hata inapomletea madhara (4)

  • 16

    • Yehova ni Chanzo cha wema

      • “Yehova ni fungu langu” (5)

      • ‘Mawazo yangu hunirekebisha usiku’ (7)

      • ‘Yehova yuko mkono wangu wa kulia’ (8)

      • “Hutaniacha Kaburini” (10)

  • 17

    • Sala ya kuomba ulinzi

      • “Umeuchunguza moyo wangu” (3)

      • “Katika kivuli cha mabawa yako” (8)

  • 18

    • Kumsifu Mungu kwa sababu ya wokovu

      • “Yehova ni jabali langu” (2)

      • Yehova ni mshikamanifu kwa walio washikamanifu (25)

      • Njia ya Mungu ni kamilifu (30)

      • “Unyenyekevu wako hunifanya niwe mkuu” (35)

  • 19

    • Uumbaji wa Mungu na sheria yake hutoa ushahidi

      • ‘Mbingu hutangaza utukufu wa Mungu’ (1)

      • Sheria kamilifu ya Mungu hurudisha nguvu (7)

      • “Dhambi nisizojua” (12)

  • 20

    • Wokovu kwa ajili ya mfalme mtiwa-mafuta wa Mungu

      • Wengine hutegemea magari ya vita na farasi, “lakini sisi tunaliitia jina la Yehova” (7)

  • 21

    • Baraka kwa mfalme anayemtumaini Yehova

      • Mfalme apewa maisha marefu (4)

      • Maadui wa Mungu watashindwa (8-12)

  • 22

    • Baada ya kukata tamaa, amsifu Mungu

      • “Mungu wangu, kwa nini umeniacha?” (1)

      • “Wanalipigia kura vazi langu” (18)

      • Kumsifu Mungu kutanikoni (22, 25)

      • Dunia yote itamwabudu Mungu (27)

  • 23

    • “Yehova ni Mchungaji wangu”

      • “Sitakosa chochote” (1)

      • “Huniburudisha” (3)

      • “Kikombe changu kimejazwa vizuri” (5)

  • 24

    • Mfalme mtukufu aingia malangoni

      • ‘Dunia ni ya Yehova’ (1)

  • 25

    • Sala ya kuomba mwongozo na msamaha

      • “Nifundishe vijia vyako” (4)

      • “Urafiki wa karibu pamoja na Yehova” (14)

      • “Unisamehe dhambi zangu zote” (18)

  • 26

    • Kutembea katika utimilifu

      • “Nichunguze, Ee Yehova” (2)

      • Kuepuka marafiki wabaya (4, 5)

      • ‘Nitapiga mwendo kuzunguka madhabahu ya Mungu’ (6)

  • 27

    • Yehova ni ngome ya uhai wangu

      • Kulithamini hekalu la Mungu (4)

      • Yehova anajali hata ikiwa wazazi hawajali (10)

      • “Mtumaini Yehova” (14)

  • 28

    • Sala ya mtunga zaburi yasikiwa

      • ‘Yehova ni nguvu zangu na ngao yangu’ (7)

  • 29

    • Sauti ya Yehova yenye nguvu

      • Abuduni katika mapambo matakatifu (2)

      • “Mungu mtukufu hunguruma” (3)

      • Yehova huwapa nguvu watu wake (11)

  • 30

    • Maombolezo yabadilishwa kuwa shangwe

      • Kibali cha Mungu hudumu maisha yote (5)

  • 31

    • Kumkimbilia Yehova

      • “Naiweka roho yangu mkononi mwako” (5)

      • “Yehova, Mungu wa ukweli” (5)

      • Wema mwingi wa Mungu (19)

  • 32

    • Wenye furaha ni wale waliosamehewa

      • “Nikaungama dhambi yangu kwako” (5)

      • Mungu hukupa ufahamu (8)

  • 33

    • Sifa kwa Muumba

      • “Mwimbieni wimbo mpya” (3)

      • Yehova aumba kupitia neno lake na roho yake (6)

      • Taifa la Yehova lina furaha (12)

      • Jicho la Yehova hulinda (18)

  • 34

    • Yehova huwaokoa watumishi wake

      • “Na tulikweze jina lake pamoja” (3)

      • Malaika wa Yehova hulinda (7)

      • “Onjeni mwone kwamba Yehova ni mwema” (8)

      • ‘Hakuna hata mfupa wake mmoja uliovunjwa’ (20)

  • 35

    • Sala ya kuomba ukombozi kutoka kwa maadui

      • Maadui watafukuzwa (5)

      • Kumsifu Mungu katikati ya umati wa watu (18)

      • Achukiwa bila sababu (19)

  • 36

    • Upendo mshikamanifu wa Mungu wenye thamani

      • Mwovu hamwogopi Mungu (1)

      • Mungu ni chanzo cha uhai (9)

      • “Kwa nuru yako tunaweza kuona nuru” (9)

  • 37

    • Wanaomtumaini Yehova watafanikiwa

      • Usikasirishwe na waovu (1)

      • “Pata furaha tele katika Yehova” (4)

      • “Mkabidhi Yehova njia yako” (5)

      • “Wapole wataimiliki dunia” (11)

      • Waadilifu hawatakosa chakula (25)

      • Waadilifu wataishi milele duniani (29)

  • 38

    • Sala ya mtu aliyetubu anayeteseka

      • “Nimesononeka na kushuka moyo kupita kiasi” (6)

      • Yehova huwasikia wale wanaomngojea (15)

      • “Nilihangaishwa na dhambi yangu” (18)

  • 39

    • Ufupi wa maisha

      • Mwanadamu ni pumzi tu (5, 11)

      • “Usipuuze machozi yangu” (12)

  • 40

    • Kumshukuru Mungu asiyeweza kulinganishwa na yeyote

      • Kazi za Mungu ni nyingi sana zisiweze kusimuliwa (5)

      • Dhabihu si jambo kuu kwa Mungu (6)

      • “Ninafurahia kufanya mapenzi yako” (8)

  • 41

    • Sala katika kitanda cha ugonjwa

      • Mungu huwategemeza wagonjwa (3)

      • Asalitiwa na rafiki wa karibu (9)

  • 42

    • Kumsifu Mungu akiwa Mwokozi Mtukufu

      • Kuwa na kiu kwa ajili ya Mungu kama paa aliye na kiu ya maji (1, 2)

      • “Kwa nini nimesononeka?” (5, 11)

      • “Mngojee Mungu” (5, 11)

  • 43

    • Mungu ambaye ni Mwamuzi huokoa

      • “Itume nuru yako na kweli yako” (3)

      • “Kwa nini nimesononeka?” (5)

      • “Mngojee Mungu” (5)

  • 44

    • Sala ya kuomba msaada

      • “Ni wewe uliyetuokoa” (7)

      • Kama “kondoo wa kuchinjwa” (22)

      • “Amka utusaidie!” (26)

  • 45

    • Ndoa ya mfalme mtiwa-mafuta

      • Maneno yenye fadhili (2)

      • “Mungu ni kiti chako cha ufalme milele” (6)

      • Mfalme anautamani urembo wa bibi harusi (11)

      • Wana watakuwa wakuu katika dunia yote (16)

  • 46

    • “Mungu ni kimbilio letu”

      • Kazi za Mungu zinazostaajabisha (8)

      • Mungu akomesha vita katika dunia yote (9)

  • 47

    • Mungu ni Mfalme wa dunia yote

      • ‘Yehova ni mwenye kuogopesha’ (2)

      • Mwimbieni Mungu sifa (6, 7)

  • 48

    • Sayuni, jiji la Mfalme Mtukufu

      • Shangwe ya dunia yote (2)

      • Likagueni jiji na minara yake (11-13)

  • 49

    • Upumbavu wa kuutumaini utajiri

      • Hakuna mwanadamu anayeweza kumkomboa mwingine (7, 8)

      • Mungu hukomboa kutoka Kaburini (15)

      • Utajiri hauwezi kuokoa kutoka katika kifo (16, 17)

  • 50

    • Mungu huhukumu kati ya mtu mshikamanifu na mwovu

      • Wanaofanya agano pamoja na Mungu kwa dhabihu (5)

      • “Mungu mwenyewe ni Mwamuzi” (6)

      • Wanyama wote ni wa Mungu (10, 11)

      • Mungu awafichua waovu (16-21)

  • 51

    • Sala ya mtu aliyetubu

      • Mwenye dhambi tangu alipochukuliwa mimba (5)

      • “Nisafishe kutoka katika dhambi yangu” (7)

      • “Umba moyo safi ndani yangu” (10)

      • Moyo uliopondeka humpendeza Mungu (17)

  • 52

    • Kuutumaini upendo mshikamanifu wa Mungu

      • Wanaojigamba kwa sababu ya uovu waonywa (1-5)

      • Wasiomwogopa Mungu wanautumaini utajiri (7)

  • 53

    • Ufafanuzi kumhusu mpumbavu

      • “Hakuna Yehova” (1)

      • “Hakuna yeyote anayetenda mema” (3)

  • 54

    • Sala ya kuomba msaada unapokuwa kati ya maadui

      • “Mungu ni msaidizi wangu” (4)

  • 55

    • Sala ya mtu aliyesalitiwa na rafiki

      • Adhihakiwa na rafiki wa karibu (12-14)

      • “Mtupie Yehova mzigo wako” (22)

  • 56

    • Sala ya mtu anayeteswa

      • “Katika Mungu ninaweka tumaini langu” (4)

      • “Machozi yangu katika kiriba chako cha ngozi” (8)

      • “Mwanadamu ambaye ni duni tu atanifanya nini?” (4, 11)

  • 57

    • Sala ya kuomba kibali

      • Kimbilio chini ya mabawa ya Mungu (1)

      • Maadui waanguka katika mtego wao wenyewe (6)

  • 58

    • Kuna Mungu anayeihukumu dunia

      • Sala ya kuomba waovu waadhibiwe (6-8)

  • 59

    • Mungu ni ngao na kimbilio

      • “Usiwaonyeshe rehema wasaliti” (5)

      • “Nitaimba kuhusu nguvu zako” (16)

  • 60

    • Mungu huwatiisha maadui

      • Wokovu kutoka kwa wanadamu hauna faida yoyote (11)

      • “Kwa msaada wa Mungu tutapata nguvu” (12)

  • 61

    • Mungu ni mnara wenye nguvu dhidi ya maadui

      • “Nitakuwa mgeni katika hema lako” (4)

  • 62

    • Wokovu wa kweli hutoka kwa Mungu

      • “Ninamngojea Mungu kimyakimya” (1, 5)

      • ‘Mwageni mioyo yenu mbele za Mungu’ (8)

      • Wanadamu ni pumzi tu (9)

      • Usitumaini mali (10)

  • 63

    • Kumtamani Mungu

      • “Upendo wako mshikamanifu ni bora kuliko uhai” (3)

      • “Nimeridhika na fungu bora” (5)

      • Kutafakari kumhusu Mungu wakati wa usiku (6)

      • ‘Ninashikamana na Mungu’ (8)

  • 64

    • Ulinzi dhidi ya mashambulizi yaliyofichika

      • “Mungu atawapiga mishale” (7)

  • 65

    • Mungu anaitunza dunia

      • “Msikiaji wa sala” (2)

      • “Mwenye furaha ni yule unayemchagua” (4)

      • Wema mwingi wa Mungu (11)

  • 66

    • Kazi za Mungu zinazostaajabisha

      • “Njooni mwone kazi za Mungu” (5)

      • “Nitatimiza nadhiri zangu kwako” (13)

      • Mungu husikia sala (18-20)

  • 67

    • Miisho ya dunia itamwogopa Mungu

      • Njia ya Mungu itajulikana (2)

      • ‘Mataifa yote na yamsifu Mungu’ (3, 5)

      • “Mungu atatubariki” (6, 7)

  • 68

    • ‘Maadui wa Mungu na watawanyike’

      • “Baba wa mayatima” (5)

      • Mungu huwapa makao walio wapweke (6)

      • Wanawake wanatangaza habari njema (11)

      • Wanaume kuwa zawadi (18)

      • ‘Yehova hutubebea mzigo wetu kila siku’ (19)

  • 69

    • Sala ya kuokolewa

      • “Bidii kwa ajili ya nyumba yako imenila” (9)

      • “Nijibu haraka” (17)

      • ‘Walinipa siki ninywe’ (21)

  • 70

    • Aomba asaidiwe haraka

      • “Tenda haraka kwa niaba yangu” (5)

  • 71

    • Tegemeo la waliozeeka

      • Kumtumaini Mungu tangu wakati wa ujana (5)

      • “Ninapoishiwa na nguvu” (9)

      • ‘Mungu amenifundisha tangu nilipokuwa kijana’ (17)

  • 72

    • Utawala wa amani wa mfalme aliyewekwa na Mungu

      • “Mwadilifu atasitawi” (7)

      • Raia kutoka bahari mpaka bahari (8)

      • Kuokolewa kutoka katika ukatili (14)

      • Nafaka itakuwa nyingi duniani (16)

      • Jina la Mungu lasifiwa milele (19)

  • 73

    • Mtu aliyemwogopa Mungu arudiwa na ufahamu wa kiroho

      • “Hatua zangu zilikuwa karibu kuteleza” (2)

      • “Nilitaabika mchana kutwa” (14)

      • “Mpaka nilipoingia mahali patakatifu pa Mungu” (17)

      • Waovu wako kwenye ardhi yenye utelezi (18)

      • Kumkaribia Mungu ni jambo jema (28)

  • 74

    • Asali Mungu awakumbuke watu wake

      • Matendo ya Mungu ya wokovu yakumbukwa (12-17)

      • “Kumbuka dhihaka za adui” (18)

  • 75

    • Mungu ahukumu kwa haki

      • Waovu watakunywa kikombe cha Yehova (8)

  • 76

    • Mungu atawashinda maadui wa Sayuni

      • Mungu awaokoa wapole (9)

      • Maadui wenye kiburi watanyenyekezwa (12)

  • 77

    • Sala ya wakati wa taabu

      • Kutafakari kazi za Mungu (11, 12)

      • ‘Ee Mungu, ni nani aliye mkuu kama wewe?’ (13)

  • 78

    • Utunzaji wa Mungu na ukosefu wa imani wa Waisraeli

      • Kisimulie kizazi kijacho (2-8)

      • “Hawakudhihirisha imani katika Mungu” (22)

      • “Nafaka ya mbinguni” (24)

      • “Wakamhuzunisha Mtakatifu wa Israeli” (41)

      • Kutoka Misri mpaka Nchi ya Ahadi (43-55)

      • “Waliendelea kumjaribu Mungu” (56)

  • 79

    • Sala iliyotolewa mataifa yalipowavamia watu wa Mungu

      • ‘Sisi ni kitu cha kushutumiwa’ (4)

      • ‘Tusaidie kwa ajili ya jina lako’ (9)

      • “Walipize jirani zetu mara saba” (12)

  • 80

    • Mchungaji wa Israeli atafutwa ili awarudishe

      • “Ee Mungu, turudishe” (3)

      • Israeli, mzabibu wa Mungu (8-15)

  • 81

    • Wahimizwa watii

      • Msiabudu miungu ya kigeni (9)

      • ‘Laiti mngesikiliza’ (13)

  • 82

    • Mwito wa kutekeleza hukumu ya haki

      • Mungu anahukumu miongoni mwa “miungu” (1)

      • “Mteteeni mtu wa hali ya chini” (3)

      • “Ninyi ni miungu” (6)

  • 83

    • Sala ya mtu anayekabili maadui

      • “Ee Mungu, usinyamaze” (1)

      • Maadui ni kama mwiba unaopeperushwa (13)

      • Jina la Mungu ni Yehova (18)

  • 84

    • Kutamani sana hema tukufu la Mungu la ibada

      • Mlawi atamani kuwa kama ndege (3)

      • “Siku moja katika nyua zako” (10)

      • “Mungu ni jua na ngao” (11)

  • 85

    • Sala ya kuomba warudishwe

      • Mungu atawaambia washikamanifu wake kuhusu amani (8)

      • Upendo mshikamanifu utakutana na uaminifu (10)

  • 86

    • Hakuna mungu aliye kama Yehova

      • Yehova yuko tayari kusamehe (5)

      • Mataifa yote yatamwabudu Yehova (9)

      • ‘Nifundishe kuhusu njia yako’ (11)

      • “Unganisha moyo wangu” (11)

  • 87

    • Sayuni, jiji la Mungu wa kweli

      • Waliozaliwa Sayuni (4-6)

  • 88

    • Sala ya kuomba ulinzi dhidi ya kifo

      • “Uhai wangu uko kwenye kingo za Kaburi” (3)

      • ‘Kila asubuhi ninasali kwako’ (13)

  • 89

    • Kuimba kuhusu upendo mshikamanifu wa Yehova

      • Agano pamoja na Daudi (3)

      • Uzao wa Daudi utadumu milele (4)

      • Mtiwa-mafuta wa Mungu amwita Yeye “Baba” (26)

      • Agano la Daudi ni hakika (34-37)

      • Mwanadamu hawezi kuponyoka Kaburi (48)

  • 90

    • Mungu wa milele na mwanadamu anayeishi kwa muda mfupi

      • Miaka elfu moja ni kama jana (4)

      • Mwanadamu anaishi miaka 70-80 (10)

      • “Tufundishe jinsi ya kuhesabu siku zetu” (12)

  • 91

    • Ulinzi mahali pa siri pa Mungu

      • Kuokolewa kutoka kwa mwindaji wa ndege (3)

      • Kukimbilia chini ya mabawa ya Mungu (4)

      • Usalama hata elfu moja wakianguka (7)

      • Malaika waagizwa kutoa ulinzi (11)

  • 92

    • Yehova akwezwa milele

      • Kazi zake kuu na mawazo yake yenye kina (5)

      • ‘Waadilifu watasitawi kama mti’ (12)

      • Waliozeeka wataendelea kunawiri (14)

  • 93

    • Utawala wa Yehova wenye utukufu

      • “Yehova amekuwa Mfalme!” (1)

      • “Vikumbusho vyako vinategemeka” (5)

  • 94

    • Sala ya kuomba Mungu alipize kisasi

      • “Waovu wataendelea mpaka lini?” (3)

      • Kurekebishwa na Yah huleta furaha (12)

      • Mungu hatawaacha watu wake (14)

      • ‘Kutunga matatizo kwa kutumia sheria’ (20)

  • 95

    • Ibada ya kweli pamoja na utii

      • “Leo ikiwa mtaisikiliza sauti yake” (7)

      • “Msiufanye moyo wenu kuwa mgumu” (8)

      • “Hawataingia katika pumziko langu” (11)

  • 96

    • “Mwimbieni Yehova wimbo mpya”

      • Yehova anastahili kusifiwa kuliko wote (4)

      • Miungu ya mataifa ni ubatili (5)

      • Abuduni katika mapambo matakatifu (9)

  • 97

    • Yehova amekwezwa juu ya miungu mingine

      • “Yehova amekuwa Mfalme!” (1)

      • Mpendeni Yehova, chukieni maovu (10)

      • Nuru kwa ajili ya mwadilifu (11)

  • 98

    • Yehova ni Mwokozi na Mwamuzi mwadilifu

      • Wokovu wa Yehova watangazwa (2, 3)

  • 99

    • Yehova ni Mfalme mtakatifu

      • Ameketi kwenye kiti cha ufalme juu ya makerubi (1)

      • Mungu anayesamehe na kuadhibu (8)

  • 100

    • Kumshukuru Muumba

      • “Mtumikieni Yehova kwa kushangilia” (2)

      • ‘Ni Mungu aliyetuumba’ (3)

  • 101

    • Mtawala anayetenda kwa utimilifu

      • ‘Sitavumilia kiburi’ (5)

      • “Nitawatazama waaminifu” (6)

  • 102

    • Sala ya mtu aliyekandamizwa, anapokuwa amekata tamaa

      • “Mimi ni kama ndege aliye peke yake” (7)

      • ‘Siku zangu ni kivuli kinachofifia’ (11)

      • “Yehova atalijenga upya Sayuni” (16)

      • Yehova hudumu milele (26, 27)

  • 103

    • “Nafsi yangu na imsifu Yehova”

      • Mungu huweka dhambi zetu mbali sana (12)

      • Mungu huonyesha rehema kama baba (13)

      • Mungu hukumbuka kwamba sisi ni mavumbi (14)

      • Kiti cha ufalme cha Yehova na ufalme wake (19)

      • Malaika hutekeleza neno la Mungu (20)

  • 104

    • Kumsifu Mungu kwa sababu ya maajabu ya uumbaji

      • Dunia itadumu milele (5)

      • Divai na mkate kwa ajili ya mwanadamu anayeweza kufa (15)

      • “Jinsi kazi zako zilivyo nyingi sana!” (24)

      • ‘Roho inapoondolewa, wanakufa’ (29)

  • 105

    • Matendo ya uaminifu ya Yehova kuelekea watu wake

      • Mungu anakumbuka agano lake (8-10)

      • “Msiwaguse watiwa-mafuta wangu” (15)

      • Yosefu aliye utumwani atumiwa na Mungu (17-22)

      • Miujiza ya Mungu nchini Misri (23-36)

      • Waisraeli watoka Misri (37-39)

      • Mungu akumbuka agano alilofanya pamoja na Abrahamu (42)

  • 106

    • Waisraeli wakosa kuthamini

      • Walisahau haraka matendo ya Mungu (13)

      • Walibadili utukufu wa Mungu kwa mfano wa ng’ombe dume (19, 20)

      • Hawakuwa na imani katika ahadi ya Mungu (24)

      • Walijiunga na ibada ya Baali (28)

      • Watoto watolewa dhabihu kwa roho waovu (37)

  • 107

    • Mshukuruni Mungu kwa sababu ya kazi zake zinazostaajabisha

      • Aliwaongoza katika njia inayofaa (7)

      • Aliwatosheleza wenye kiu na wenye njaa (9)

      • Aliwatoa gizani (14)

      • Alituma neno lake kuwaponya (20)

      • Huwalinda maskini ili wasikandamizwe (41)

  • 108

    • Sala ya ushindi dhidi ya maadui

      • Wokovu kutoka kwa wanadamu hauna faida yoyote (12)

      • “Kwa msaada wa Mungu tutapata nguvu” (13)

  • 109

    • Sala ya mtu anayeteseka

      • “Mtu mwingine na achukue cheo chake” (8)

      • Mungu husimama mkono wa kulia wa maskini (31)

  • 110

    • Mfalme na kuhani kama Melkizedeki

      • ‘Tawala kati ya maadui wako’ (2)

      • Vijana wanaojitoa kwa hiari ni kama matone ya umande (3)

  • 111

    • Msifuni Yehova kwa sababu ya kazi zake kuu

      • Jina la Mungu ni takatifu na linaogopesha (9)

      • Kumwogopa Yehova ni hekima (10)

  • 112

    • Mwadilifu humwogopa Yehova

      • Mtu anayekopesha kwa ukarimu atafanikiwa (5)

      • “Mwadilifu atakumbukwa milele” (6)

      • Mtu mkarimu huwapa maskini (9)

  • 113

    • Mungu aliye juu humwinua mtu wa hali ya chini

      • Jina la Yehova lasifiwa milele (2)

      • Mungu huinama chini (6)

  • 114

    • Waisraeli wakombolewa kutoka Misri

      • Bahari ilikimbia (5)

      • Milima ilirukaruka kama kondoo dume (6)

      • Mwamba mgumu wabadilishwa kuwa chemchemi za maji (8)

  • 115

    • Mungu peke yake ndiye anayepaswa kutukuzwa

      • Sanamu zisizo na uhai (4-8)

      • Wanadamu wamepewa dunia (16)

      • “Watu waliokufa hawamsifu Yah” (17)

  • 116

    • Wimbo wa shukrani

      • “Nitamlipa Yehova nini?” (12)

      • “Nitakiinua kikombe cha wokovu” (13)

      • “Nitamtimizia Yehova nadhiri zangu” (14, 18)

      • Kifo cha washikamanifu kina thamani (15)

  • 117

    • Mataifa yote yahimizwa yamsifu Yehova

      • Upendo mshikamanifu wa Mungu ni mkubwa (2)

  • 118

    • Kushukuru kwa sababu ya ushindi wa Yehova

      • ‘Nilimlilia Yah, naye akanijibu’ (5)

      • “Yehova yuko upande wangu” (6, 7)

      • Jiwe lililokataliwa litakuwa jiwe kuu la pembeni (22)

      • “Yule anayekuja katika jina la Yehova” (26)

  • 119

    • Kulithamini neno la Mungu lenye thamani

      • ‘Vijana wanaweza kuisafishaje njia yao?’ (9)

      • “Ninavipenda sana vikumbusho vyako” (24)

      • “Neno lako ni tumaini langu” (74, 81, 114)

      • “Jinsi ninavyoipenda sana sheria yako!” (97)

      • “Ufahamu mwingi kuliko walimu wangu wote” (99)

      • “Neno lako ni taa ya mguu wangu” (105)

      • ‘Kiini cha neno lako ni kweli’ (160)

      • Wanaoipenda sheria ya Mungu wana amani (165)

  • 120

    • Mgeni atamani amani

      • ‘Niokoe kutoka kwa ulimi mdanganyifu’ (2)

      • “Mimi ni mtu wa amani” (7)

  • 121

    • Yehova huwalinda watu wake

      • “Msaada wangu hutoka kwa Yehova” (2)

      • Yehova halali usingizi kamwe (3, 4)

  • 122

    • Sala ya kuomba jiji la Yerusalemu liwe na amani

      • Shangwe ya kwenda katika nyumba ya Yehova (1)

      • Jiji lililounganishwa pamoja kama kitu kimoja (3)

  • 123

    • Kumtazama Yehova ili kupata kibali

      • ‘Kama watumishi, tunamtazama Yehova’ (2)

      • “Tumedharauliwa vya kutosha” (3)

  • 124

    • “Kama Yehova hangekuwa pamoja nasi”

      • Ponyoka kutoka katika mtego uliovunjika (7)

      • ‘Jina la Yehova ni msaada wetu’ (8)

  • 125

    • Yehova huwalinda watu wake

      • “Kama milima inavyozunguka Yerusalemu” (2)

      • “Amani na iwe juu ya Israeli” (5)

  • 126

    • Sayuni litarudishwa kwa shangwe

      • ‘Yehova ametenda mambo makuu’ (3)

      • Baada ya kutokwa na machozi, kutakuwa na shangwe (5, 6)

  • 127

    • Bila Mungu, kila kitu ni bure

      • “Yehova asipoijenga nyumba” (1)

      • Watoto ni thawabu kutoka kwa Mungu (3)

  • 128

    • Furaha kwa sababu ya kumwogopa Yehova

      • Mke kama mzabibu unaozaa matunda mengi (3)

      • “Na uone Yerusalemu likipata ufanisi” (5)

  • 129

    • Ashambuliwa lakini hakushindwa

      • Wanaolichukia Sayuni waaibishwa (5)

  • 130

    • “Kutoka vilindini ninakulilia”

      • ‘Ikiwa ungekuwa unatazama makosa’ (3)

      • Msamaha wa kweli hutoka kwa Yehova (4)

      • “Ninamngojea Yehova kwa hamu” (6)

  • 131

    • Kuridhika kama mtoto aliyeachishwa kunyonya

      • Kutotafuta mambo makubwa sana (1)

  • 132

    • Daudi achaguliwa na pia Sayuni

      • “Usimkatae mtiwa-mafuta wako” (10)

      • Makuhani wa Sayuni wavishwa wokovu (16)

  • 133

    • Kukaa pamoja kwa umoja

      • Kama mafuta kwenye kichwa cha Haruni (2)

      • Kama umande wa Hermoni (3)

  • 134

    • Kumsifu Mungu nyakati za usiku

      • “Inueni mikono yenu katika utakatifu” (2)

  • 135

    • Msifuni Yah kwa sababu ya ukuu wake

      • Ishara na miujiza dhidi ya Misri (8, 9)

      • “Jina lako linadumu milele” (13)

      • Sanamu zisizo na uhai (15-18)

  • 136

    • Upendo mshikamanifu wa Yehova hudumu milele

      • Mbingu na dunia ziliumbwa kwa ustadi (5, 6)

      • Farao alikufa katika Bahari Nyekundu (15)

      • Mungu huwakumbuka walioshuka moyo (23)

      • Huwapa chakula viumbe wote walio hai (25)

  • 137

    • Kando ya mito ya Babiloni

      • Nyimbo za Sayuni hazikuimbwa (3, 4)

      • Babiloni kuangamizwa (8)

  • 138

    • Mungu anajali, ingawa amekwezwa

      • ‘Ulijibu sala yangu’ (3)

      • ‘Hata katikati ya hatari, unaniokoa’ (7)

  • 139

    • Mungu anawajua vizuri watumishi wake

      • Huwezi kujificha mbali na roho ya Mungu (7)

      • ‘Nimeumbwa kwa njia inayostaajabisha’ (14)

      • ‘Uliniona nikiwa kiinitete’ (16)

      • “Uniongoze katika njia ya milele” (24)

  • 140

    • Yehova ni Mwokozi mwenye nguvu

      • Waovu ni kama nyoka (3)

      • Watu wakatili wataangamia (11)

  • 141

    • Sala ya kuomba ulinzi

      • ‘Sala yangu na iwe kama uvumba’ (2)

      • Karipio la mwadilifu ni kama mafuta (5)

      • Waovu wanaanguka ndani ya nyavu zao wenyewe (10)

  • 142

    • Sala ya kuomba aokolewe kutoka kwa watesaji

      • “Sina mahali popote pa kukimbilia” (4)

      • “Ni wewe tu niliye nawe” (5)

  • 143

    • Kiu kwa ajili ya Mungu kama nchi iliyokauka

      • ‘Ninatafakari kazi zako’ (5)

      • “Nifundishe kufanya mapenzi yako” (10)

      • ‘Roho yako nzuri na iniongoze’ (10)

  • 144

    • Sala ya kuomba ushindi

      • ‘Mwanadamu anayeweza kufa ni nini?’ (3)

      • ‘Maadui na watawanywe’ (6)

      • Watu wa Yehova ni wenye furaha (15)

  • 145

    • Kumsifu Mungu, Mfalme mkuu

      • ‘Nitatangaza ukuu wa Mungu’ (6)

      • “Yehova ni mwema kwa wote” (9)

      • “Washikamanifu wako watakusifu” (10)

      • Ufalme wa Mungu ni wa milele (13)

      • Mkono wa Mungu huwatosheleza wote (16)

  • 146

    • Mtumaini Mungu, si wanadamu

      • Mawazo ya mwanadamu hupotea anapokufa (4)

      • Mungu huwainua juu walioinama chini (8)

  • 147

    • Kuzisifu kazi za Mungu za upendo na zenye nguvu

      • Huwaponya waliovunjika moyo (3)

      • Huziita nyota zote kwa majina (4)

      • Hutoa theluji kama sufu (16)

  • 148

    • Uumbaji wote na umsifu Yehova

      • “Msifuni, enyi malaika wake wote” (2)

      • ‘Msifuni, jua, mwezi, na nyota’ (3)

      • Vijana kwa wazee na wamsifu Mungu (12, 13)

  • 149

    • Wimbo wa kuusifu ushindi wa Mungu

      • Mungu anawafurahia watu wake (4)

      • Heshima ni ya washikamanifu wa Mungu (9)

  • 150

    • Kila kitu kinachopumua na kimsifu Yah