Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kitabu cha Methali

Sura

Muhtasari wa Yaliyomo

  • 1

    • Kusudi la methali (1-7)

    • Hatari za marafiki wabaya (8-19)

    • Hekima ya kweli hupaza sauti hadharani (20-33)

  • 2

    • Thamani ya hekima (1-22)

      • Tafuta hekima kama hazina zilizofichika (4)

      • Uwezo wa kufikiri ni ulinzi (11)

      • Uasherati huleta msiba (16-19)

  • 3

    • Uwe na hekima na umtumaini Yehova (1-12)

      • Mheshimu Yehova kwa vitu vyenye thamani (9)

    • Hekima huleta furaha (13-18)

    • Hekima huleta usalama (19-26)

    • Mambo mema ya kuwatendea wengine (27-35)

      • Watendee wengine mema inapowezekana (27)

  • 4

    • Mafundisho ya baba yenye hekima (1-27)

      • Zaidi ya yote, pata hekima (7)

      • Epuka vijia vya uovu (14, 15)

      • Kijia cha waadilifu huzidi kung’aa (18)

      • “Ulinde moyo wako” (23)

  • 5

    • Onyo dhidi ya wanawake waasherati (1-14)

    • Shangilia pamoja na mke wako (15-23)

  • 6

    • Jihadhari kuhusiana na kutoa dhamana ya mkopo (1-5)

    • “Mwendee chungu, ewe mvivu” (6-11)

    • Mtu mwovu asiyefaa kitu (12-15)

    • Vitu saba ambavyo Yehova anachukia (16-19)

    • Jilinde dhidi ya mwanamke mwovu (20-35)

  • 7

    • Zishike amri za Mungu uishi (1-5)

    • Kijana mjinga atongozwa (6-27)

      • “Kama ng’ombe dume anayeenda machinjioni” (22)

  • 8

    • Hekima yaongea kama mtu (1-36)

      • ‘Mimi ni mwanzo kabisa wa kazi za Mungu’ (22)

      • ‘Nilikuwa kando ya Mungu nikiwa mfanyakazi stadi’ (30)

      • “Niliwapenda sana wanadamu” (31)

  • 9

    • Hekima ya kweli inatoa mwaliko (1-12)

      • “Nitafanya siku zako ziwe nyingi” (11)

    • Mwanamke mpumbavu awaalika watu (13-18)

      • “Maji yaliyoibwa ni matamu” (17)

  • METHALI ZA SULEMANI (10:1–24:34)

    • 10

      • Mwana mwenye hekima humfanya baba yake ashangilie (1)

      • Mikono yenye bidii huleta utajiri (4)

      • Kusema maneno mengi husababisha makosa (19)

      • Baraka ya Yehova hutajirisha (22)

      • Kumwogopa Yehova hurefusha maisha (27)

    • 11

      • Wenye kiasi wana hekima (2)

      • Mwasi imani huwaangamiza wengine (9)

      • “Washauri wengi huleta mafanikio” (14)

      • Mtu mkarimu atapata ufanisi (25)

      • Anayeutumaini utajiri wake ataanguka (28)

    • 12

      • Anayechukia karipio hana akili (1)

      • “Maneno yanayosemwa bila kufikiri huchoma kama upanga” (18)

      • Kusitawisha amani huleta shangwe (20)

      • Midomo inayosema uwongo humchukiza Yehova (22)

      • Mahangaiko huulemea moyo (25)

    • 13

      • Wanaotafuta ushauri wana hekima (10)

      • Tumaini likikawia huufanya moyo uwe mgonjwa (12)

      • Mjumbe mwaminifu huleta maponyo (17)

      • Kutembea na wenye hekima humfanya mtu awe na hekima (20)

      • Nidhamu huonyesha upendo (24)

    • 14

      • Moyo hujua uchungu wake wenyewe (10)

      • Njia inayoonekana kuwa sawa inaweza kusababisha kifo (12)

      • Mjinga huamini kila neno (15)

      • Tajiri ana marafiki wengi (20)

      • Moyo mtulivu huupa mwili uzima (30)

    • 15

      • Jibu la upole hutuliza hasira (1)

      • Macho ya Yehova yako kila mahali (3)

      • Sala ya mtu mnyoofu humfurahisha Mungu (8)

      • Mipango huvunjika watu wasiposhauriana (22)

      • Tafakari kabla ya kujibu (28)

    • 16

      • Yehova huchunguza nia (2)

      • Mkabidhi Yehova kazi zako (3)

      • Mizani ya unyoofu hutoka kwa Yehova (11)

      • Kiburi hutangulia kuanguka kwa kishindo (18)

      • Mvi ni taji la umaridadi (31)

    • 17

      • Usilipe uovu kwa wema (13)

      • Ondoka kabla ugomvi haujaanza (14)

      • Rafiki wa kweli hupenda nyakati zote (17)

      • “Moyo wenye shangwe ni dawa nzuri” (22)

      • Mtu mwenye utambuzi huyazuia maneno yake (27)

    • 18

      • Kujitenga na wengine ni jambo la kichoyo lisilo la hekima (1)

      • Jina la Yehova ni mnara wenye nguvu (10)

      • Mali ni ulinzi wa kuwaziwa tu (11)

      • Hekima ya kusikiliza pande zote mbili (17)

      • Rafiki hushikamana na mtu kwa ukaribu kuliko ndugu (24)

    • 19

      • Ufahamu hutuliza hasira (11)

      • Mke mgomvi ni kama paa linalovuja (13)

      • Mke mwenye busara hutoka kwa Yehova (14)

      • Mtie mtoto nidhamu wakati bado kuna tumaini (18)

      • Hekima ya kusikiliza mashauri (20)

    • 20

      • Divai ni mdhihaki (1)

      • Mvivu halimi katika majira ya baridi kali (4)

      • Mawazo ya mtu ni kama maji yenye kina (5)

      • Onyo dhidi ya kuapa haraka-haraka (25)

      • Utukufu wa vijana ni nguvu zao (29)

    • 21

      • Yehova huuelekeza moyo wa mfalme (1)

      • Haki ni bora kuliko dhabihu (3)

      • Bidii huleta mafanikio (5)

      • Asiyemsikiliza mtu wa hali ya chini hatasikilizwa (13)

      • Hakuna hekima katika kumpinga Yehova (30)

    • 22

      • Jina jema ni bora kuliko mali nyingi (1)

      • Mazoezi ya mapema ya mtoto yatadumu maisha yake yote (6)

      • Mvivu huogopa kwamba simba yuko nje (13)

      • Nidhamu huondoa ujinga (15)

      • Mfanyakazi stadi huwatumikia wafalme (29)

    • 23

      • Uwe na busara unapokubali mwaliko (2)

      • Usifuatie utajiri (4)

      • Utajiri unaweza kuruka mbali nawe (5)

      • Usiwe miongoni mwa walevi (20)

      • Kileo huuma kama nyoka (32)

    • 24

      • Usiwaonee wivu waovu (1)

      • Nyumba hujengwa kwa hekima (3)

      • Mwadilifu anaweza kuanguka lakini atainuka (16)

      • Usilipize kisasi (29)

      • Kusinzia huleta umaskini (33, 34)

  • METHALI ZA SULEMANI ZILIZONAKILIWA NA WATU WA MFALME HEZEKIA (25:1–29:27)

    • 25

      • Kutunza siri (9)

      • Maneno yaliyochaguliwa vizuri (11)

      • Kuheshimu faragha ya wengine (17)

      • Kukusanya makaa ya mawe juu ya kichwa cha adui (21, 22)

      • Habari njema ni kama maji baridi (25)

    • 26

      • Ufafanuzi kuwahusu watu wavivu (13-16)

      • Epuka ugomvi usiokuhusu (17)

      • Epuka mizaha inayodhuru (18, 19)

      • Pasipo na kuni, moto huzimika (20, 21)

      • Maneno ya mchongezi ni kama matonge matamu (22)

    • 27

      • Karipio kutoka kwa rafiki hunufaisha (5, 6)

      • Mwanangu, ufanye moyo wangu ushangilie (11)

      • Chuma hunoa chuma (17)

      • Lijue kundi lako (23)

      • Mali haidumu milele (24)

    • 28

      • Sala ya mtu asiyesikiliza inachukiza (9)

      • Anayeungama huonyeshwa rehema (13)

      • Anayeharakisha kupata utajiri hatakosa hatia (20)

      • Karipio ni bora kuliko kusifusifu (23)

      • Mtu mkarimu hakosi chochote (27)

    • 29

      • Mtoto aliyeachiliwa huleta aibu (15)

      • Bila maono, watu hutenda wapendavyo (18)

      • Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi (22)

      • Mtu mnyenyekevu hupata utukufu (23)

      • Kuwaogopa wanadamu ni mtego (25)

  • 30

    • MANENO YA AGURI (1-33)

      • Usinipe umaskini wala utajiri (8)

      • Vitu visivyotosheka kamwe (15, 16)

      • Vitu visivyoacha alama (18, 19)

      • Mwanamke mzinzi (20)

      • Wanyama wenye hekima ya kisilika (24)

  • 31

    • MANENO YA MFALME LEMUELI (1-31)

      • Ni nani anayeweza kumpata mke mwema? (10)

      • Hufanya kazi kwa bidii na jitihada (17)

      • Fadhili ziko kwenye ulimi wake (26)

      • Watoto wake na mume wake humsifu (28)

      • Sura nzuri na urembo hutoweka upesi (30)