Nitaenda kwa Nani?
Pakua:
1. Nimemtii Yesu
Kwenye hali ngumu.
Ni mwanga wangu
Namsikiliza.
Mchungaji mwema,
Ananifundisha.
Huniongoza,
Kwenye njia bora.
(KIBWAGIZO)
Kwa nini nisikie
Sauti za wapinzani,
Wenye nia mbaya
Wanitoe njia hi’?
(KORASI)
Nitaenda kwa nani?
Nikabilipo matatizo?
Nitaenda kwa nani?
Kuna hatari
Kufuata mgeni.
Namsikiliza Yesu tu.
2. Nahisi kuridhika
Naye hunitunza,
Tuna upendo
Miongoni mwetu.
Ninatazamia
Baraka za Mungu.
Katuma Mwanaye
Awe Mwokozi.
(KIBWAGIZO)
Sitasikiliza
Sauti za wapinzani.
Kwa nini nitoke
Niache njia hii?
(KORASI)
Nitaenda kwa nani?
Nikabilipo matatizo?
Nitaenda kwa nani?
Kuna hatari
Kufuata mgeni.
Namsikiliza Yesu tu.
(KORASI)
Nitaenda kwa nani?
Nikabilipo matatizo?
Nitaenda kwa nani?
Kuna hatari
Kufuata mgeni.
Namsikiliza Yesu tu.
Nitaenda kwa nani?
Kamwe, kamwe sitapotoshwa.