Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Wanusurika Kifo

Wanusurika Kifo

Wanusurika Kifo

“Nyakati nyingine mimi huwaza kwamba nina miguu miwili tena. . . . Miaka mingi iliyopita, nilipokuwa mtoto, nilienda kucheza na rafiki zangu karibu na nyumba yetu. Ghafula, nilisikia ‘BUUM’ . . . Mguu wangu wa kulia ulilipuliwa wote.”—Song Kosal, mwenye umri wa miaka 12, Kambodia.

Kila siku, watu 70 kwa wastani hulemazwa au kuuawa na mabomu ya ardhini. Wahasiriwa wengi si wanajeshi. Badala yake, ni raia—wanaume wanaochunga ng’ombe, wanawake wanaoteka maji, na watoto wanaocheza. Kwa mfano, Rukia mwenye umri wa miaka minane tuliyemwonyesha kwenye jalada la gazeti hili, alikatwa kiungo cha mwili na bomu la ardhini lililoua nduguze watatu na shangaziye.

Bomu la ardhini laweza kubaki likiwa hatari kwa zaidi ya miaka 50 tangu linapotegwa. Hivyo, “ hiyo ndiyo silaha pekee inayoua watu wengi zaidi baada ya kukoma kwa vita kuliko wakati wa vita,” lasema gazeti la The Defense Monitor. Hakuna mtu ajuaye ni mabomu mangapi ya ardhini yametegwa ulimwenguni pote. Ni kawaida kusikia idadi ikikadiriwa kuwa angalau mabomu milioni 60. Ni kweli kwamba mabomu mengi ya ardhini yanaondolewa. Hata hivyo, hivi majuzi katika mwaka wa 1997, shirika la Umoja wa Mataifa liliripoti kwamba “bomu moja linapoondolewa, mabomu mengine 20 hutegwa ardhini. Mnamo mwaka wa 1994, mabomu yapatayo 100,000 yaliondolewa, na mabomu mengine milioni 2 yakategwa.”

Kwa nini mababe wengi wa vita leo wanapendelea mabomu ya ardhini? Yanaathirije uchumi na jamii? Manusura huathiriwaje? Je, sayari yetu itawahi kuwa bila mabomu ya ardhini?

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 3]

© ICRC/David Higgs

Copyright Nic Dunlop/Panos Pictures