Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Mnyanyaso Makala ya “Mnyanyaso wa Kidini Huko Georgia—Utaendelea Hadi Lini?” (Januari 22, 2002) ilinifahamisha jinsi ulimwengu huu unavyobadilika-badilika. Mimi hufikiria makala kama hizo, na kujiuliza, ‘Nilifanya nini hayo yalipokuwa yakiendelea? Uhusiano wangu na Yehova ulikuwa wenye nguvu kiasi gani wakati ndugu na dada zangu walipoteswa vibaya?’ Tafadhali wajulisheni ndugu na dada zetu kwamba twawapenda na kwamba sisi pia huathiriwa na mateso yao.

K. S., Marekani

Niliposoma kuhusu mnyanyaso ambao Mashahidi wa Yehova huko Georgia wanapata, sikuweza kujizuia nisilie. Ninasali kwa Yehova awaimarishe na awalinde na awaonyeshe upendo wake. Ningependa kuwajulisha ndugu na dada zangu huko Georgia kwamba ninasali kwa ajili yao. Hata ingawa niko sehemu tofauti, ninashukuru sana kwa pendeleo la ajabu la kufanya kazi nao kwa nia moja.

M. T., Japan

Nilisikia ndugu wakisali kwa ajili ya ndugu na dada zetu huko Georgia katika mikutano yetu kila juma, lakini sikujua mengi kuwahusu. Sikuweza kuwazia kwamba ukatili kama ule uliotajwa katika makala hii ulikuwa ukitendeka. Waambieni kwamba ndugu na dada ulimwenguni kote wanasali kwa ajili yao. Wao ni chanzo cha kitia-moyo kwetu tulio na matatizo madogo sana kuliko wao.

V. P., Marekani

Imani ya ndugu hao ilinigusa sana, na nililia nilipojua mateso wanayopata. Wana ujasiri mwingi, msimamo thabiti, na wanamtegemea Yehova kabisa. Ningefurahi wakijulishwa kwamba ninawahurumia, ninawapenda, na ninawakumbuka katika sala zangu.

F. F., Italia

Mizungu Asanteni sana kwa makala “Vijana Huuliza . . . Kuna Hatari Gani Kujihusisha Kidogo Tu na Mambo ya Mizungu?” (Januari 22, 2002) Makali hii ilinipatia ujasiri wa kutupilia mbali kabisa kifaa kimoja kinachotilika shaka. Nilitiwa moyo kusoma zaidi kuhusu mfano wa Waefeso waliochoma vitabu vyao vya mizungu, ingawa viligharimu vipande 50,000 vya fedha. (Matendo 19:19) Thamani ya karatasi nilizotupa kwenye pipa la takataka haiwezi kulinganishwa na thamani ya vitu ambavyo Yehova atanipatia. Asanteni kwa kuchapisha makala hizo kwa wakati ufaao.

A. N., Japan

Nilibatizwa mwezi mmoja uliopita. Kabla ya kujifunza Biblia, niliwasiliana na roho kwa kushawishiwa na mamangu, ambaye si mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Makala hiyo ilikuja kwa wakati uliofaa. Ninajua mambo ya kuepuka, na ninamtumaini Yehova kabisa. Baada ya kusoma makala hiyo na kuizungumzia mara nyingi na dada Mkristo, hofu yangu inapungua.

A. P., Ujerumani

Kutoka kwa Mwalimu Nikiwa mwalimu katika shule ya msingi, ningependa kuwashukuru wahariri wa Amkeni! Gazeti lenu linaelimisha na linawasaidia wanafunzi kupata elimu iliyosawazika. Mimi na walimu wenzangu hulitumia darasani kufundishia kuhusu masuala ya maadili na ya kijamii. Amkeni! huchangia kujenga utu wa wanafunzi na kuboresha maisha yao kwa kuwasaidia kufanya maamuzi yenye hekima.

F. C., Brazili