Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kuingia Katika Ulimwengu Usio na Huruma!

Kuingia Katika Ulimwengu Usio na Huruma!

Kuingia Katika Ulimwengu Usio na Huruma!

MTOTO huzaliwa katika ulimwengu wenye ukatili, usio na huruma, na uliojaa matatizo. Ingawa mtoto hawezi kueleza hisia zake, wanasayansi fulani wanaamini kwamba mtoto hujua kinachoendelea hata kabla hajazaliwa.

Kitabu The Secret Life of the Unborn Child kinasema: “Sasa tunajua kwamba mtoto aliye tumboni ni mwanadamu anayetambua mambo na anayetenda, ambaye huanza kuwa na hisia katika mwezi wake wa sita tumboni (na labda hata mapema zaidi).” Ingawa mtoto hawezi kukumbuka, wanasayansi fulani wanadhani kwamba maisha yake ya baadaye yanaweza kuathiriwa na hali ngumu zinazokuwepo wakati wa kujifungua.

Matatizo huendelea baada ya kuzaliwa. Anapotoka nje ya tumbo la mama yake, mtoto haendelei kupata chakula na oksijeni kupitia kiunga-mwana kilichounganishwa na kitovu chake. Anahitaji kuanza kupumua na kula ili aendelee kuishi. Anahitaji mtu wa kumlisha na kumwandalia mahitaji mengine.

Mtoto anahitaji pia kukua kiakili, kihisia, na kiroho. Kwa hiyo, mtu fulani anahitaji kumlea. Ni nani anayeweza kumtunza vizuri? Mtoto anahitaji nini kutoka kwa wazazi wake? Mahitaji hayo yanaweza kutoshelezwaje? Makala zinazofuata zitajibu maswali hayo.