Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Juu ya Nini Ni Muzuri Kuwa na Tumaini

Juu ya Nini Ni Muzuri Kuwa na Tumaini

Juu ya Nini Ni Muzuri Kuwa na Tumaini

MAMBO ingekuwa namna gani kama Daniel, ule kijana mwenye alikuwa na kansere mwenye tulizungumuzia ku mwanzo ya habari yenye ilitangulia, angeendelea kuwa na tumaini yenye nguvu? Angepona? Angekuwa muzima leo? Inawezekana hata watu wenye wanaamini kabisa kama tumaini inaweza kusaidia hawawezi kusema vile. Na ile inaonyesha hii jambo ya maana yenye tunapaswa kukumbuka: Hatupaswe kuwaza kama tumaini ni dawa ya kila kitu.

Wakati munganga Nathan Cherney alikuwa anaulizwa maulizo na watangazaji wa habari wa CBS, alionyesha kama ni mubaya kuambia watu wenye wanagonjwa sana kama watasikia muzuri ikiwa wako na tumaini. Alisema hivi: “Tumejionea bwana wenye wanalaumu bibi zao kwa kuwaambia kama hawako najikaza kuamini kama watapona na kutumaini kama mambo itakuwa muzuri.” Munganga Cherney aliongeza hivi: “Ile namna ya kufikiri imefanya watu wakuwe na mawazo yenye haiko ya kweli. Wanawaza kama kuwa na tumaini kunaweza kusaidia kansere isiendelee. Na kama inaendelea, ni kusema mutu hakujikaza kuwa na tumaini. Lakini, ile haiko kweli.”

Kusema kweli, mambo haikuwake mwepesi kwa wale wenye wako na ugonjwa wenye unakaribia kuwaua. Watu wa familia yao na marafiki wao hawawezi kupenda hata kidogo kuwaongezea magumu kwa kufanya wawaze kama ikiwa hawapone ni juu hawako najikaza kuwa na tumaini. Ni kusema hakuna faida ya kuwa na tumaini?

Haiko vile, kuko faida. Kwa mufano, kuliko kutunza ugonjwa ao kujaribu kurefusha maisha ya wagonjwa, uleule munganga anasaidiaka watu wenye wako na magonjwa yenye haiwezi kupona juu waishi siku za mwisho-mwisho za maisha yao bila maumivu kadiri inawezekana. Wanganga wenye wanatunzaka watu vile wanaamini kama kusaidia mutu atazamie kama mambo itakuwa muzuri kuko na faida sana hata kwa watu wenye wanagonjwa sana. Kuko ushuhuda wenye kuonyesha kama kuwa na tumaini kunaweza kusaidia sana wagonjwa.

Faida ya Kuwa na Tumaini

Munganga Gifford-Jones anasema hivi: “Tumaini ni dawa ya nguvu sana.” Alijifunza uchunguzi mbalimbali wenye watu walifanya kuhusu faida ya kutia moyo wagonjwa wenye wanakaribia kufa. Watu wengi wanawaza kama kufanya vile kunasaidia wagonjwa wakuwe na tumaini zaidi na watazamie kama mambo itakuwa muzuri. Uchunguzi fulani wenye ulifanywa mu 1989 ulionyesha kama watu wenye walikuwa wanatiwa moyo waliishi wakati murefu zaidi. Lakini uchunguzi mbalimbali wenye ulifanywa kisha pale haukuonyesha vile. Hata vile, uchunguzi mbalimbali umeonyesha kama wagonjwa wenye wanatiwa moyo hawakuwake na huzuni ya kupita kiasi na hawasikiake maumivu sana sawa wagonjwa wenye hawatiwe moyo.

Fikiria uchunguzi mwingine wenye ulifanywa juu ya kutafuta kujua ikiwa kuwa na tumaini ao kukosa tumaini kunaweza kufanya mutu apate ugonjwa wa mishipa ya moyo ao hapana. Wanaume 1 300 walichunguzwa kwa uangalifu juu ya kuona ikiwa walikuwa na tumaini ao hapana. Kisha miaka 10, wanaume 160 kati ya wale wanaume walikuwa wamepata aina fulani ya ugonjwa wa mishipa ya moyo. Wengi kati ya wale wanaume 160 walikuwa wale wenye hawakukuwa na tumaini. Laura Kubzansky, mwenye anafundishaka ku masomo fulani ya kinganga, anasema hivi kuhusu ule uchunguzi: “Mupaka sasa hakukuwa ushuhuda wenye kuonyesha wazi kabisa kama kuwa na tumaini kunaweza kusaidia afya. Huu ni ushuhuda wa kwanza wa kinganga wenye unaonyesha kama kuwa na tumaini kunaweza kusaidia moyo.”

Uchunguzi fulani umeonyesha kama wale wenye wanaonaka kama afya yao haiko muzuri, hawaponake mbio kisha kufanyiwa upasuaji (opération) kwa kulinganisha na wale wenye wanaonaka kama wako na afya ya muzuri. Hata ushuhuda umeonyesha kama wale wenye wako na tumaini wanakuwaka wanaishi siku mingi. Watu fulani wenye kufanya uchunguzi walitafuta kujua kama mambo inakuwaka namna gani wakati muzee iko na mawazo ya muzuri ao ya mubaya juu ya uzee. Wakati wazee walionyeshwa habari zenye zilisema kama watu wenye kuzeeka wako na hekima na uzoefu, wale wazee walitembea na nguvu zaidi. Faida yenye walipata ilikuwa sawa vile faida yenye wangepata kisha kufanya mazoezi mu majuma 12!

Juu ya nini inaonekana kama kuwa na tumaini na kutazamia kama mambo itakuwa muzuri kunaweza kusaidia afya? Inaonekana kama watu wenye kujifunza sayansi na wanganga hawawezi kujibia muzuri ile ulizo juu hawayaelewa muzuri kabisa namna akili na mwili wa mwanadamu vinafanya kazi. Lakini, wale wenye kujifunza ile mambo wanaweza kutoa mawazo fulani. Kwa mufano, mutu mumoja mwenye kujifunza ubongo anasema hivi: “Mutu anajisikiaka muzuri kama iko na furaha na tumaini. Wakati mutu iko na furaha, hakuwake na mahangaiko mingi, na ile inamusaidia akuwe na afya ya muzuri. Ile ni kati ya mambo yenye watu wanaweza kujitafutia juu waendelee kuwa na afya ya muzuri.”

Wanganga, watu wenye kujifunza saikolojia, na watu wenye kujifunza sayansi wanaweza kuona kama ile ni mawazo ya mupya. Lakini, haiko ya mupya kwa watu wenye kujifunza Biblia. Miaka 3 000 yenye imepita, roho ya Mungu iliongoza Mufalme Sulemani aandike hivi: “Moyo wenye furaha ni dawa ya muzuri, lakini roho yenye kupondwa inamaliza mutu nguvu.” (Mezali 17:22) Maneno ya ile andiko iko na usawaziko. Haiseme kama moyo wenye furaha unaponyeshaka magonjwa yote, lakini inasema tu kama moyo wenye furaha “ni dawa ya muzuri.”

Na kusema kweli, kama tumaini ingekuwa dawa ya magonjwa yote, wanganga wote wangeiandikia wagonjwa wao. Kuwa na tumaini hakusaidiake tu afya, lakini kuko na faida zingine za mingi.

Kuwa na Tumani na Kukosa Tumaini Kunaweza Kuwa na Matokeo Gani Juu ya Maisha Yako?

Watu wenye kufanya uchunguzi wametambua kama watu wenye kuwa na tumaini wanapataka faida mingi. Wanawezaka ku masomo, wanatumikaka muzuri, na wanafanyaka muzuri mu mambo ya michezo. Kwa mufano, uchunguzi ulifanywa mu kikundi ya wanamuke wenye kufanya michezo ya kukimbia. Wenye kuwazoeza walichunguza kwa uangalifu mambo yenye kila mwanamuke iko na uwezo wa kufanya wakati wa mashindano. Wale wanamuke pia waliulizwa maulizo juu ya kuona ni kwa kadiri gani walikuwa na tumaini. Ku mwisho, ilionekana kama mambo yenye wale wanamuke walitumaini kama wanaweza kutimiza njo ilionyesha kabisa uwezo wenye walikuwa nao kuliko vile wale wenye kuwazoeza waliwaza. Juu ya nini tumaini iko na nguvu vile?

Watu wenye kujifunza mambo ya sayansi wamejifunza mambo ingine ya mingi kwa kuchunguza watu wenye kukosa tumaini. Zaidi ya miaka 50 yenye imepita, watu wenye kujifunza mambo ya sayansi walivumbula kama wanyama na hata wanadamu wanaweza kujifunza kuishi bila tumaini. Kwa mufano, walitia watu mu chumba yenye iko na fujo na kuwaambia kama wanaweza kunyamazisha ile fujo kwa kuponda boutons mbalimbali. Na waliweza kunyamazisha ile fujo.

Kisha waliambia kikundi ya pili wafanye pia vile, lakini fujo haikuisha kisha kuponda zile boutons. Vile unaweza kuwazia, wengi kati ya wale wa kikundi ya pili walipoteza tumaini. Wakati waliambiwa wafanye tena vile, hawakupenda kupima tena. Walikuwa wamejiambia kama hata wafanye nini mambo haitabadilika. Lakini, hata mu ile kikundi ya pili, wale wenye walitazamia kama mambo itakuwa muzuri, hawakupoteza tumaini.

Martin Seligman, mwalimu wa saikolojia, alisaidiaka kufanya uchunguzi fulani kati ya zile uchunguzi. Kwa hiyo aliamua kuendelea kujifunza juu ya matokeo ya kuwa na tumaini na kukosa tumaini. Alijifunza mawazo ya watu wenye wanazoeaka kujiona kuwa wa bure. Alivumbula kama ile mawazo inazuiaka watu kutimiza mambo mingi mu maisha, na hata inawafanya wasipime kutimiza jambo yoyote. Seligman alifasiriaka hivi matokeo ya kukosa tumaini: “Nimejifunza matokeo ya kukosa tumaini kwa miaka 25. Nimejifunza juu ya watu wenye hawana tumaini wenye wanaamini kuwa ni kosa yao kama mambo ya mubaya iko nawafikia, na kama ile mambo itaendelea kuwapata hata wafanye nini. Niko hakika kama juu wako na ile mawazo, mambo ya mingi ya mubaya itawapata kuliko wale wenye wako na tumaini.”

Kama vile tuliona, leo wengine wanaweza kuona ile mawazo kuwa ya mupya, lakini haiko ya mupya kwa wale wenye kujifunza Biblia. Mezali moja inasema hivi: “Kama unavunjika moyo siku ya taabu, nguvu zako zitakuwa kidogo.” (Mezali 24:10) Kwa kweli, Biblia inafasiria waziwazi kama kuvunjika moyo na kukosa tumaini kunaweza kufanya mutu akose nguvu ya kutenda. Sasa, unaweza kufanya nini juu usikuwe mutu wa kukosa tumaini lakini ukuwe mutu mwenye anatazamia kama mambo itakuwa muzuri na mwenye iko na tumaini mu maisha?

[Picha]

Kuwa na tumaini kunaweza kusaidia sana