Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Unaweza Kuachana na Mawazo ya Kukosa Tumaini

Unaweza Kuachana na Mawazo ya Kukosa Tumaini

Unaweza Kuachana na Mawazo ya Kukosa Tumaini

UNAFANYAKA nini wakati unapata magumu? Watu wengi wenye elimu wanaamini kama namna unatendaka wakati unapata magumu njo inaonyesha kama uko na tumaini ao hapana. Siye wote tunapataka magumu mu maisha, wamoja wanapataka magumu mingi kuliko wengine. Sasa, juu ya nini watu fulani wenye wanapata magumu ya kidogo wanavunjikaka moyo na kuacha kujikaza, lakini wengine wanapataka tena nguvu na kujikaza kuendelea na maisha hata kama walipata magumu ya nguvu sana?

Kwa mufano, tuseme uko unatafuta kazi. Unaenda kuzungumuza na mukubwa wa kazi lakini hakupatie kazi. Kisha pale, utajisikia namna gani? Unaweza kuwaza kama ni kosa yako, na kama hakuna mutu mwenye atakupatiaka kazi. Ao, jambo ya mubaya zaidi, unaweza kuwaza kama, vile tu haukupata ile kazi, maana yake hauko mutu wa maana na hakuna mutu mwenye anaweza kuwa na lazima yako. Kuwaza vile ni alama ya kukosa tumaini.

Namna ya Kuachana na Mawazo ya Kukosa Tumaini

Unaweza kufanya nini juu upiganishe mawazo ya kukosa tumaini? Kwanza, ni muzuri ujikaze kutambua mawazo ya kukosa tumaini yenye uko nayo. Kisha uipiganishe. Ujikaze kuelewa ni juu ya nini haukupata kazi. Kwa mufano, ni kweli kama haukupata kazi juu hakuna mutu mwenye anakufurahia? Ao ni juu tu mukubwa wa kazi alikuwa anatafuta mutu mwenye iko na uwezo tofauti na wako?

Kama unachunguza mambo muzuri, utaona kama mawazo ya kukosa tumaini yenye uko nayo, haina musingi. Juu jambo moja tu inashindikana, ni kusema hauwezi kuweza kitu? Hakuna mambo ingine yenye iko inaendeka muzuri kwa kadiri fulani mu maisha yako, sawa vile urafiki wako na Mungu, hali ya familia yako, na urafiki wako na watu wengine? Ujikaze juu usikuwe unawaza kama kila kitu yenye unafanya itashindikana. Tuseme tu kweli, unaweza kabisa kujua kama hautapataka kazi? Kuko mambo ingine yenye unaweza kufanya juu upiganishe mawazo ya kukosa tumaini.

Uamini Kama Unaweza Kutimiza Mipango Yako

Mu miaka yenye imepita, watu wenye kufanya uchunguzi wamefasiria muzuri maana ya kuwa na tumaini. Lakini, ile mafasirio haineze kabisa maana yote ya kuwa na tumaini. Wanasema kama kuwa na tumaini ni kuamini kama utaweza kutimiza mipango yako. Kama vile tutaona mu habari yenye kufuata, maana ya kuwa na tumaini haiishie pale. Lakini, ile mafasirio inaweza kusaidia mu njia mingi. Inaweza kutusaidia tuamini kama tunaweza kutimiza mipango yetu.

Kusudi tuamini kama tunaweza kutimiza mipango yetu, ni muzuri tuanze na mipango ya kidogo-kidogo. Wakati tunaitimiza, tutaamini kabisa kama tunaweza kutimiza mipango ingine ya mukubwa. Kama unaona kuwa hauyatimiza mupango hata moja, pengine ni muzuri ufikirie mipango yenye unajiwekea. Uko kwanza na mipango? Juu tuko na mambo mingi ya kufanya, ni mwepesi kusahau kupanga mambo yenye tunapenda kabisa kufanya mu maisha. Kuhusu kupanga mambo, Biblia inatushauria hivi: “Muhakikishe mambo ya maana zaidi.”​—Wafilipi 1:10.

Wakati tunajua mambo ya maana mu maisha yetu, inakuwa mwepesi kupanga mambo yenye tunapenda kufanya mu sehemu mbalimbali za maisha, sawa vile mu urafiki wetu pamoja na Mungu, mu familia yetu, na mu mambo ingine. Lakini, ni muzuri tusijipangie mambo mingi ya kufanya, na ni muzuri tujipangie mambo yenye haitakuwa nguvu kutimiza. Juu kama tunajipangia mambo yenye iko nguvu kutimiza, tunaweza kuvunjika moyo na kuacha kujikaza. Njo maana, kama kuko jambo fulani kubwa yenye tunapenda kutimiza, inakuwaka muzuri kuigawanya mu mambo ya kidogo-kidogo yenye tunaweza kutimiza mu wakati kidogo-kidogo.

Kama mutu anapenda kabisa kufanya jambo fulani, anaweza kuitimiza. Ni kusema, kama tulishapanga kufanya mambo fulani, tunapaswa kuwa na nia ya kujikaza kuitimiza. Juu tukuwe na nia kabisa ya kutimiza ile mambo ni muzuri tufikirie faida zenye tutapata kama tunaitimiza. Kusema kweli, kutakuwa matatizo fulani yenye itafanya ikuwe nguvu kutimiza mipango yetu, lakini tusiache ile matatizo ituvunje moyo na kufanya tuache kujikaza.

Zaidi ya ile, tunapaswa kufikiria mambo yenye tunapaswa kufanya juu tutimize mipango yetu. Rick Snyder, muandikaji mwenye amejifunza sana juu ya faida ya kuwa na tumaini, anasema kama ni muzuri kufikiria njia mbalimbali za kutimiza mupango fulani. Juu kama njia moja haiendeke muzuri, tunaweza kutumia njia ya pili, ya tatu, na kuendelea.

Snyder anasema pia kama wakati fulani inakuwaka muzuri kubadilisha mipango yetu. Kama tumeshindwa kutimiza mupango fulani, kuendelea kujihangaisha juu ya ule mupango kutatuvunja tu moyo. Lakini, kama tunaachana na ule mupango na tunajiwekea mupango mwingine wenye tunaweza kutimiza, tunaweza kuwa tena na tumaini.

Kuhusu kubadilisha mipango yetu, Biblia iko na mufano wenye unaweza kutusaidia. Mufalme Daudi alipanga kujenga hekalu kwa ajili ya Yehova, Mungu wake. Lakini, Mungu aliambia Daudi kama mwana wake Sulemani njo atafanya ile kazi. Kuliko kuvunjika moyo na kutafuta tu kuijenga, Daudi alibadilisha mipango yake. Alitumikisha nguvu yake juu ya kukusanya feza na vitu vyenye Sulemani angetumikisha mu ile kazi.​—1 Wafalme 8:17-19; 1 Mambo ya Nyakati 29:3-7.

Hata kama tulishajikaza kupiganisha mawazo ya kukosa tumaini na tumekuwa watu wenye kutazamia kama mambo itakuwa muzuri, wakati fulani tunaweza kukosa tumaini. Juu ya nini? Juu hatuna uwezo wa kumaliza mambo mingi yenye inafanyaka watu wakose tumaini mu hii dunia. Inawezekana kabisa kuwa na tumaini wakati tunafikiria mambo mingi yenye iko inatesa wanadamu leo, sawa vile umaskini, vita, ukosefu wa haki, magonjwa, na kifo?

[Picha]

Wakati hawakupatie kazi yenye ulikuwa unatafuta, unawaza mara moja kama hautapataka kazi?

[Picha

Mufalme Daudi alikuwa tayari kubadilisha mipango yake