Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Tunaweza Kupata Wapi Tumaini ya Kweli

Tunaweza Kupata Wapi Tumaini ya Kweli

Tunaweza Kupata Wapi Tumaini ya Kweli

Saa yako imesimama na inaonekana imeharibika. Unapenda fundi airekebishe lakini haujue, ni fundi gani njo atairekebisha. Watu wengi wanasema kama wanaweza kurekebisha saa lakini mawazo yao inapingana. Kisha unavumbula kama jirani yako njo alitengenezaka ile saa na anakuambia kama atakusaidia kuirekebisha bila kukuomba feza. Ni wazi kama yeye njo utachagua.

Sasa linganisha ile saa na uwezo wako wa kuwa na tumaini. Kama unatambua kama unaanza kupoteza tumaini, sawa watu wengi leo mu hii wakati wa magumu, wapi njo utatafutia musaada? Watu wengi wanasema kama wanaweza kukusaidia lakini mawazo yao inavuruga akili na inapingana. Hauone kama ni muzuri utafute ule mwenye alipatiaka wanadamu uwezo wa kuwa na tumaini? Biblia inasema kama Mungu “haiko mbali sana na kila mumoja wetu” na iko tayari kutusaidia.​—Matendo 17:27; 1 Petro 5:7.

Kuwa na Tumaini Kunamaanisha Nini Kabisa?

Biblia inafasiria muzuri zaidi maana ya kuwa na tumaini kuliko vile wanganga, watu wenye kujifunza sayansi, na watu wenye kujifunza saikolojia wanaifasiria. Mu Biblia, maneno ya luga ya kwanza-kwanza yenye inatafsiriwa “tumaini” iko na maana ya kungoya kwa hamu na kutazamia mambo ya muzuri. Ni kusema tumaini inafanyizwa na mambo mbili. Kwanza, ni kutamani mambo ya muzuri ifanyike. Na pili, ni kuwa na sababu ya kuamini kama ile mambo itafanyika. Tumaini yenye Biblia inatupatia, haiko ndoto. Inategemea mambo yenye iko hakika.

Kwa hiyo, tumaini iko sawa vile imani, juu imani nayo inategemea mambo yenye iko hakika, hapana mambo ya kuwazia-wazia tu. (Waebrania 11:1) Hata vile, Biblia inaonyesha kama kuko fofauti fulani kati ya imani na tumaini.​—1 Wakorinto 13:13.

Juu uelewe, fikiria hii mufano: Wakati unaomba rafiki yako akufanyie jambo fulani unaweza kutumainia kama atakusaidia. Uko na sababu ya kumutumainia juu unamuaminia. Na kama unamuaminia, ni juu unamujua muzuri na alishakakusaidia zamani. Kuko upatano kati ya imani na tumaini, na zile sifa zinaendaka pamoja hata kama ziko tofauti. Inawezekana umutumainie Mungu naye vile?

Sababu za Kuwa na Tumaini

Mungu njo anapatiaka watu tumaini ya kweli. Zamani, Biblia ilimuita Yehova kuwa “tumaini la Israeli.” (Yeremia 14:8) Tumaini yoyote ya kweli yenye watu wake walikuwa nayo ilitoka kwake, ni mu ile maana njo alikuwa tumaini la Israeli. Ile tumaini haikukuwa ndoto tu. Mungu aliwapatia sababu za kuwa na tumaini. Kwa miaka mingi, alikuwa anawaahidi mambo mbalimbali na alikuwa anaitimiza. Yoshua, kiongozi wao, aliwaambia hivi: “Munajua muzuri . . . kwamba hakuna hata neno moja lenye halikutimia kati ya ahadi zote za muzuri zenye Yehova Mungu wenu aliwaahidi.”​—Yoshua 23:14.

Hata leo, Yehova angali anatimiza ahadi zake. Biblia iko na ahadi za muzuri zenye Mungu alitoaka na inaonyesha waziwazi namna zilitimiaka. Ahadi za Mungu ni za kweli kabisa kiasi ya kwamba, wakati fulani, wenye waliziandika walitumia maneno yenye ilifanya zionekane kama zilishatimia.

Njo maana, tunaweza kusema kama Biblia ni kitabu yenye inatoa tumaini. Wakati utaendelea kujifunza namna Mungu alikuwa anatendea watu, utapata sababu za mingi za kumutumainia. Mutume Paulo aliandika hivi: “Mambo yote yenye yaliandikwa zamani yaliandikwa ili kutufundisha sisi, ili kupitia uvumilivu wetu na kupitia faraja kutoka katika Maandiko tukuwe na tumaini.”​—Waroma 15:4.

Mungu Anatupatia Tumaini Gani?

Ni wakati gani njo tunakuwaka na lazima kabisa ya tumaini? Zaidi sana wakati mutu mwenye tunapenda anakufa. Lakini, ni ile wakati tena njo watu wengi wanapotezaka tumaini. Kusema kweli, kifo inafanyaka mutu aishiwe kabisa. Kifo inaweza kutufikia saa ni saa. Hakuna mutu mwenye anaweza kuepuka kifo, na hatuwezi kurudishia uzima mupendwa wetu. Njo maana, Biblia iko na sababu kabisa ya kuita kifo “adui wa mwisho.”​—1 Wakorinto 15:26.

Sasa, kuko tumaini kwa ajili ya wale wenye wamekufa? Ile andiko ya Biblia yenye inaita kifo kuwa adui, inasema tena kama ule adui “ataharibiwa.” Yehova Mungu iko na nguvu kuliko kifo. Na ameonyesha vile mara mingi. Namna gani? Kwa kufufua wafu. Biblia inazungumuzia watu kenda wenye Mungu alifufua kwa kutumia nguvu yake.

Kwa mufano, Yehova alipatia Yesu, Mwana wake, nguvu ya kufufua rafiki yake mupendwa, Lazaro, mwenye alikuwa alishafanya siku ine mu kaburi. Yesu hakufanya vile kwa uficho, lakini mbele ya watu wengi.​—Yohana 11:38-48, 53; 12:9, 10.

Unaweza kujiuliza, ‘Juu ya nini sasa Mungu alifufuaka wale watu? Si walizeekaka tena na wakakufa!’ Ni kweli walizeekaka tena na wakakufa. Lakini, zile habari za ufufuo zinatufanya tutamani kuona tena wapendwa wetu na zinatupatia sababu ya kuamini kama kuko siku wataishi tena. Ni kusema, tuko na tumaini ya kweli kabisa.

Yesu alisema hivi: “Mimi ndiye ufufuo na uzima.” (Yohana 11:25) Yeye njo Yehova atapatia nguvu ya kufufua watu mu dunia yote. Yesu alisema tena hivi: “Saa inakuja yenye wale wote wenye kuwa katika makaburi ya ukumbusho watasikia sauti [ya Kristo] na watatoka.” (Yohana 5:28, 29) Kwa kweli, wale wote wenye kuwa mu kaburi wako na tumaini ya kufufuliwa na kuishi mu dunia paradiso.

Nabii Isaya alizungumuzia ufufuo kwa kutumia hii maneno yenye kufurahisha: “Wafu wako wataishi. Maiti wangu wataamuka. Muamuke na mupige vigelegele vya shangwe, ninyi wenye kukaa katika mavumbi! Kwa maana umande wako ni kama umande wa asubui, na dunia itaacha wale wenye hawana uwezo katika kifo ili waishi tena.”​—Isaya 26:19.

Ile maneno inatia moyo kabisa. Wafu wako mu hali yenye kuwa salama kabisa, sawa vile mutoto anakuwaka salama mu tumbo ya mama yake. Tunasema vile juu Yehova anakumbuka muzuri watu wote wenye wamekufa. (Luka 20:37, 38) Na hivi karibuni watafufuliwa na kukaribishwa kwa furaha mu dunia, sawa vile familia yenye upendo inakaribishaka mutoto mwenye anazaliwa! Kwa hiyo, kuko tumaini hata kwa ajili ya wapendwa wetu wenye wamekufa.

Utapata Faida Gani Kama Unakuwa na Tumaini?

Paulo anatufundisha mambo mingi juu ya faida ya kuwa na tumaini. Alisema kama tumaini ni sehemu ya maana ya silaha za kiroho, aliifananisha na kofia ya chuma. (1 Watesalonike 5:8) Juu ya nini? Zamani, wakati askari alikuwa anaenda ku vita, alikuwa anavala kofia ya chuma juu ya kofia ingine ya nguo ao ya ngozi. Ile kofia ilikuwa inalinda kichwa yake ili asiumie ao hata kufikia kufa ikiwa wanamutupia kitu fulani ku kichwa. Paulo alipenda kusema nini wakati alizungumuzia kofia ya chuma? Sawa vile tu kofia ya chuma inalinda kichwa, vilevile tumaini inalinda akili, ni kusema uwezo wetu wa kufikiri. Kama unatumainia kabisa ahadi za Mungu, utakuwa na amani ya akili ao utatulia hata wakati wa magumu. Nani njo atasema kama hana lazima ya ile kofia ya chuma?

Paulo alitumia mufano ingine juu ya kuonyesha faida ya kutumainia kabisa mapenzi ya Mungu. Aliandika hivi: “Tumaini hilo [liko] kama nanga ya nafsi, likiwa hakika na pia imara.” (Waebrania 6:19) Paulo alivunjikiwaka na mashua mara mingi, kwa hiyo, alijua faida ya kuwa na nanga mu mashua. Wakati mashua ilipigwa na upepo mukali, watu wenye kutumika mu mashua walikuwa wanashusha nanga. Nanga ilikuwa inasaidia mashua isitikisike-tikisike sana wakati wa upepo mukali na ilikuwa inaisaidia isiende kujigonga ku miamba.

Vilevile, kama tunaona ahadi za Mungu kuwa tumaini yenye kuwa “hakika na pia imara,” tutaweza kupiganisha magumu yenye inafanana na upepo mukali. Yehova anaahidi kama karibuni wanadamu hawatateseka tena kwa sababu ya vita, jeuri, huzuni, ao hata kifo. (Ona kisanduku “Sababu za Kuwa na Tumaini.”) Kama tunashikamana na ile tumaini, itatulinda, na itatusaidia tutii kanuni za Mungu mu maisha yetu na tutaepuka matendo ya mubaya yenye watu wengi wako nayo leo.

Tumaini yenye Yehova anatoa inaweza kukusaidia na weye. Anapenda ukuwe na maisha ya muzuri. Na anapenda “watu wa namna zote waokolewe.” Sasa, wanaweza kufanya nini juu waokolewe? Kwanza, kila mutu anapaswa ‘kupata ujuzi wenye hauna makosa wa ile kweli.’ (1 Timoteo 2:4) Wachapishaji wa hii gazeti wanakutia moyo upate ujuzi juu ya kweli ya Neno ya Mungu. Ni ule ujuzi njo utakusaidia upate uzima wa milele. Tumaini yenye Mungu atakupatia inapita kabisa tumaini yoyote yenye unaweza kupata mu hii dunia.

Kama uko na ile tumaini, hautavunjika moyo, juu Mungu anaweza kukupatia nguvu ya kutimiza mipango yoyote yenye uko nayo kama tu inapatana na mapenzi yake. (2 Wakorinto 4:7; Wafilipi 4:13) Siye wote tuko na lazima ya ile tumaini. Kwa hiyo, kama na weye uko na lazima ya ile tumaini, na kama uko unaitafuta, ujue kama unaweza kuipata!

[Kisanduku]

Sababu za Kuwa na Tumaini

Hii mawazo yenye iko mu Maandiko inaweza kukusaidia ukuwe na tumaini kabisa:

◼ Mungu anasema kama maisha itakuwa muzuri mu siku zenye ziko nakuya.

Biblia inasema kama dunia yote itakuwa paradiso na mutakuwa watu wenye furaha na umoja.​—Zaburi 37:11, 29; Isaya 25:8; Ufunuo 21:3, 4

Mungu hawezi kusema uongo.

Yehova anachukia kila namna ya uongo. Iko mutakatifu kabisa, ni kusema iko safi. Kwa hiyo, haiwezekane aseme uongo.​—Mezali 6:16-19; Isaya 6:2, 3; Tito 1:2; Waebrania 6:18.

Nguvu ya Mungu haina mipaka.

Yehova tu njo Mweza-Yote. Hakuna kitu mu ulimwengu yenye inaweza kumuzuia kutimiza mambo yenye amesema kama atafanya.​—Kutoka 15:11; Isaya 40:25, 26.

Mungu anapenda uishi milele.

​—Yohana 3:16; 1 Timoteo 2:3, 4.

Mungu anatutumainia.

Anaamua kukaza akili juu ya sifa zetu za muzuri na juu ya mambo yenye tuko najikaza kufanya, hapana juu ya makosa yetu na uzaifu wetu. (Zaburi 103:12-14; 130:3; Waebrania 6:10) Anatumainia kama tutafanya mambo ya muzuri na anafurahi wakati tunafanya vile.​—Mezali 27:11.

Mungu anatuambia kama atatusaidia tutimize mipango yetu kama inapatana na mapenzi yake.

Watumishi wake hawapaswe kuvunjika moyo. Iko tayari kuwapatia roho yake takatifu, ni kusema nguvu yake, juu ya kuwasaidia.​—Wafilipi 4:13.

Kumutumainia Mungu haiko kuchokea bure.

Unaweza kumutumainia kabisa, hawezi kukuvunja moyo.​—Zaburi 25:3.

[Picha]

Sawa vile kofia ya chuma inalinda kichwa, vilevile tumaini inalinda akili

[Picha]

Sawa vile nanga, tumaini yenye kuwa hakika inaweza kutusaidia tutulie

[Picha imetolewa na]

Courtesy René Seindal​/Su concessione del Museo Archeologico Regionale A. Salinas di Palermo