Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kuwasaidia Vijana Wanaotaabika (Aprili 8, 2005) Mfululizo huu wa makala ulikuwa wenye kuarifu sana. Nyakati nyingine utineja una magumu, lakini kuwa na makala zenye kutia moyo kama hizi hupunguza mkazo. Hii ndiyo habari tunayohitaji hasa ili kutuchochea katika ‘nyakati hizi za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo.’ (2 Timotheo 3:1) Vikumbusho katika makala hizi vitatusaidia tusianguke katika “hila za Ibilisi.” (Waefeso 6:11) Asanteni kwa kuandaa chakula cha kiroho kwa wakati unaofaa.

K. S., Marekani

Nyumba Safi—Kila Mtu Ana Sehemu Yake (Juni 8, 2005) Nilipokuwa nikikua, wazazi wangu walikuwa wakifanya kazi nasi watoto watatu tulikuwa tukicheza ndani ya nyumba. Tuliboronga mambo kwelikweli. Mimi huchukia kusafisha nyumba hadi leo hii. Lakini niliposoma makala hiyo nilihisi kana kwamba mama yangu ananifunza kwa fadhili jinsi ya kusafisha. Sasa nina watoto wakubwa, na hawapendi kufanya usafi. Ninahitaji kuwafunza mambo mengi. Nilitiwa moyo na makala hiyo.

Y. E., Japani

Mambo ya Kurudia na Familia (Mei 8, 2005) Nililia nilipoona makala hii. Nilimwonyesha binti yangu. Kisha akaniambia kwamba tayari alikuwa amesoma makala kuhusu shomoro aliyejeruhiwa na kujibu maswali yote mawili kwenye makala “Mambo ya Kurudia na Familia.”

L. S., Marekani

Maktaba—Funguo za Kupata Ujuzi (Mei 22, 2005) Ningependa kutaja kwamba picha iliyo kwenye ukurasa wa 18 si ya Mfalme Ashurbanipali wa Ashuru. Kwa kweli, picha hiyo ni ya Mfalme Esar-hadoni wa Ashuru.

A. W., Ujerumani

“Amkeni!” lajibu: Asante kwa kututajia jambo hilo. Kama inavyotajwa katika kitabu cha marejeo cha Biblia “Insight on the Scriptures,” Buku la 1, ukurasa wa 757, Esar-hadoni alikuwa mwana mchanga na mrithi wa Mfalme Senakeribu wa Ashuru. *

Kalenda Yenye Kustaajabisha ya Wamaya (Aprili 8, 2005) Makala hii ilinichochea kufanya utafiti kwenye Intaneti. Niligundua kwamba kuna uhusiano wa karibu sana kati ya kalenda ya Wamaya na unajimu. Ninahisi kwamba kuchapisha makala kama hizi kunaweza kuwachochea wasomaji waanze kupendezwa na unajimu na ufundi wa uchawi.

J. K., Poland

“Amkeni!” lajibu: Kama inavyotajwa katika ukurasa wa 4 wa “Amkeni!,” gazeti hili “huripoti habari, husimulia juu ya watu katika nchi nyingi, huchunguza dini na sayansi.” Bila shaka, hilo halimaanishi kwamba tunaunga mkono kila jambo linalotukia katika nyanja hizo. Katika makala fupi uliyotaja, tuliandika kuhusu Wamaya wa zamani, ambao walipiga hesabu kwa ustadi ambayo iliwasaidia kutokeza kalenda sahihi kwa njia yenye kustaajabisha. Kwa kuwa kalenda hiyo ilitumiwa kwa ajili ya uaguzi—jambo ambalo limetajwa katika makala hiyo—wasomaji wetu hawapaswi kuchochewa kwa njia yoyote ile kutaka kujifunza kuhusu unajimu.

Pindi kwa pindi, sisi hupokea maswali kama hayo kuhusu picha za vichapo vyetu. Picha za sanamu, ishara za kidini, au vitu vya kishirikina havipaswi kumchochea mtu atake kujua mengi zaidi bali kuondoa hali ya kutatanisha kuvihusu na kutahadharisha wasomaji wajiepushe navyo kabisa. Maelezo mengi ambayo tumepokea yanaonyesha kwamba watu wengi wamenufaishwa sana na makala na picha zetu.

[Maelezo ya Chini]

^ fu. 10 Kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.