Ona video zinazopatikana

Wakati Tabia za Watu Ziliharibika Kabisa

Wakati Tabia za Watu Ziliharibika Kabisa

Wakati Tabia za Watu Ziliharibika Kabisa

UNAWAZA ni wakati gani tabia za watu zilianza kuharibika? Ulionaka namna tabia za watu zinaanza kuharibika ao kuko watu wa familia yako ao marafiki wako wenye wanakushinda miaka wenye walionaka? Watu fulani wanasema kama tabia za watu zilianza kuharibika mu mwaka wa 1914, wakati Vita ya Kwanza ya Ulimwengu ilitokea. Robert Wohl, profesere wa historia, aliandika hivi mu kitabu yake The Generation of 1914: “Watu wengi wenye waliishi wakati wa ile vita, waliamini kama ulimwengu moja iliisha na ingine ikaanza mu Mwezi wa 8, 1914.”

Mwanahistoria Norman Cantor anasema hivi: “Kila fasi, tabia za watu zenye tayari zilikuwa zimeharibika, ziliharibika tena zaidi. Watu wenye kufanya mambo ya politike na viongozi wa jeshi walitendea watu sawa wanyama wenye wanaenda kuchinjwa. Njo maana watu waliacha kuhangaikiana na walianza kutendeana bila huruma sawa wanyama. . . . Mauaji yenye ilifanyika wakati wa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu [1914-18] ilifanya ionekane sawa uzima wa mwanadamu hauna maana.”

Mu kitabu yake The Outline of History, H. G. Wells, mwanahistoria Mwingereza, alionyesha kama tabia za watu zilianza “kuharibika sana” wakati walianza kuamini fundisho ya mageuzi. Juu ya nini? Juu watu fulani waliona kama mwanadamu naye ni munyama tu lakini mwenye iko na akili kupita wanyama wengine. Wells, mwenye alikuwa naamini mageuzi, aliandika hivi mu mwaka wa 1920: “Watu walisema kama mutu ni munyama mwenye anapendaka kuishi karibu na wengine sawa vile imbwa wa pori wa india . . . , njo maana waliona kama haiko mubaya kama mwanadamu mwenye kuwa na nguvu anaonea mwanadamu mwingine mwenye kuwa zaifu.”

Kwa kweli, kama vile Cantor alionyesha, Vita ya Kwanza ya Ulimwengu ilifanya watu washindwe kutofautisha mema na mabaya. Alisema hivi: “Watu hawakuhangaikia tena mawazo ya watu wenye kukomaa kuhusu mambo ya politike, namna ya kuvala, na ngono.” Ilikuwa pia vile juu makanisa ilikubali fundisho ya mageuzi, na ilitia watu moyo waende ku vita. Jenerale Frank Crozier aliandika hivi: “Makanisa yenye kujiita kuwa ya Kikristo ilitetea vita na kutia watu moyo waende ku vita, na siye maaskari tulifurahi kuona vile walitutegemeza.”

Watu Hawakuheshimia Tena Kanuni za Mwenendo

Mu miaka ya kisha Vita ya Kwanza ya Ulimwengu, watu walifuatia sana raha, walizarau kanuni za mwenendo, na kila mutu alifanya mambo yenye anataka. Mwanahistoria Frederick Lewis Allen anasema hivi: “Miaka kumi ya kisha Vita ya Kwanza ya Ulimwengu inaweza kuitwa miaka kumi ya tabia mubaya. . . . Watu wengi walikatala kanuni za zamani kuhusu mema na mabaya. Na ile ilifanya ikuwe nguvu kujua kanuni zenye kufaa, zenye mutu anapaswa kufuata.”

Mu miaka ya 1930, kulitokea matatizo makubwa sana ya kupata makuta. Na ile ilifanya watu wengi wakuwe maskini sana. Kufikia mwaka wa 1939, mu dunia mulitokea vita ingine ya mubaya sana yenye kuitwa Vita ya Pili ya Ulimwengu. Inchi mbalimbali zilianza kutengeneza silaha za nguvu sana. Na hata kama ile ilisaidia kupunguza umaskini, ilifanya watu wengi wateseke sana. Ku mwisho wa ile vita, miji mingi ilikuwa imebakia mabomoko. Kwa mufano, mabombe ya nguvu sana iliharibisha sana miji mbili ya Japani! Mamilioni ya watu walikufa mu kambi za mateso kwa sababu walitendewa bila huruma. Karibu watu milioni 50 walikufa mu ile vita; kati yao kulikuwa wanaume, wanamuke na watoto.

Wakati wa Vita ya Pili ya Ulimwengu, kuliko kufuata kanuni za mwenendo za tangu zamani, watu walijiendesha vile wanapenda. Kitabu Love, Sex and War​—Changing Values, 1939-​45 inasema hivi: “Ile wakati, watu hawakuruhusu jambo yoteyote iwazuie kufanya ngono. Juu watu walikuwa huru kufanya mambo yote yenye wanapenda wakati walikuwa ku vita, walileta ileile tabia mu nyumba zao na mu familia zao. . . . Watu waliogopa kama wanaweza kuuawa saa ni saa. Njo maana walitamani kuwa na mutu wa kuwaonyesha upendo hata kama ni kwa wakati kidogo tu.”

Juu ya kutetea ile tabia ya kukosa kujizuia mu mambo ya ngono, mwanamuke fulani Mwingereza alisema hivi: “Haiko kusema tulikuwa waasherati, ni juu kulikuwa vita.” Askari fulani wa Amerika alisema hivi: “Watu wengi wanaweza kuona kama tulikuwa na mwenendo mubaya, lakini tulikuwa vijana na tulikuwa najua kama tunaweza kufa saa ni saa.”

Watu wengi wenye walipona ile vita waliendelea kusumbuliwa na mambo yenye kuogopesha yenye walijionea. Watu wengi, hata wenye walikuwa wangali watoto wakati wa ile vita, wangali wanajisikia mubaya sana wakati wanakumbuka mambo yenye ilitokeaka. Watu wengi waliacha kumuamini Mungu na hawakujua tena kutofautisha mema na mabaya. Walianza kuona kama mema na mabaya inategemea tu hali yenye mutu iko ndani.

Kanuni Mupya za Mwenendo

Kisha Vita ya Pili ya Ulimwengu, ripoti ya uchunguzi mbalimbali juu ya ngono ilitolewa. Ripoti ya uchunguzi fulani wenye ulifanywa Amerika mu miaka 1940 uliitwa ripoti ya Kinsey, na ilikuwa na zaidi ya kurasa 800. Mbele ile ripoti itolewe, watu hawakuzoea kuzungumuzia waziwazi mambo ya ngono. Lakini, kisha ile ripoti kutolewa, watu walianza kuzungumuzia waziwazi mambo ya ngono. Hata kama habari za mingi zenye zilikuwa mu ile ripoti zilikuwa zimetiwa chumvi sana, ile ripoti ilionyesha kama mawazo ya watu juu ya ngono ilikuwa imeharibika kisha ile vita.

Kwa wakati fulani, watu walijifanya sawa vile wangali wanaheshimia kanuni za mwenendo. Kwa mufano, wenye mamlaka walijikaza kukataza mambo ya ngono ku radio, mu filme, na ku televizyo. Lakini, ilikuwa tu kwa wakati fulani. William Bennett, mwenye wakati fulani alikuwa anasimamia elimu katika Amerika, alisema hivi: “Lakini, kufikia miaka ya 1960, watu wa Amerika walibadilisha haraka kanuni zao za mwenendo.” Ilikuwa pia vile mu inchi zingine za mingi. Juu ya nini tabia za watu ziliharibika sana mu miaka ya 1960?

Mu ile miaka, wanamuke walipewa uhuru zaidi, na watu walibadilisha mawazo yao juu ya ngono. Tena, dawa za kupanga uzazi zilitengenezwa. Kwa hiyo, watu wangeweza “kufanya ngono bila kuogopa” kama kutakuwa mimba. Njo maana ikakuwa kawaida “watu kufanya ngono bila kufunga ndoa.”

Mu ileile wakati, mu magazeti, mu filme, na ku televizyo, watu walianza kukubali kuonyesha mambo yenye hawakukuwaka naonyesha zamani. Kisha wakati fulani, Zbigniew Brzezinski, kiongozi fulani mu guvernema ya Amerika, alisema hivi kuhusu mambo yenye kuonyeshwa ku televizyo: “Vipindi vya televizyo vinaonyesha kama raha njo jambo ya maana zaidi mu maisha, jeuri ni jambo ya kawaida, [na] ni muzuri kufanya ngono na watu wengi.”

Kufikia miaka ya 1970, kasete-video zilikuwa zimeanza kutumiwa sana. Kwa hiyo watu wengi wangeweza kuangalia filme za mambo ya uasherati mu nyumba zao, zenye hawangeweza kuenda kuangalia ku sinema. Kwa sasa, mu inchi za mingi, kama tu mutu iko na ordinatere, anaweza kuangalia pornografia chafu sana kupitia Enternete.

Tuko najionea matokeo ya mubaya sana ya ile mambo. Mulinzi fulani wa gereza alisema hivi: “Miaka kumi yenye imepita, wakati vijana walikuwa nakuya mu gereza, nilikuwa nazungumuza nao juu ya mema na mabaya. Lakini sasa, wakati vijana wanakuya mu gereza, hawaelewe niko nasema nini.”

Wapi Njo Tunaweza Kupata Muongozo?

Makanisa haiwezi kutusaidia kujua tofauti kati ya mema na mabaya. Kuliko kufuata mambo yenye Yesu na wanafunzi wake walifundisha, makanisa iko sasa najiingiza mu mambo ya mubaya sana ya hii dunia. Mwandikaji fulani aliandika hivi: “Watu wote wenye kupigana vita wanasemaka kama Mungu iko nawasaidia.” Kuhusu kufuata kanuni za mwenendo zenye Mungu anatupatia, kiongozi fulani wa dini katika New York alisema hivi: “Kuko mambo kidogo sana yenye mutu anapaswa kufanya juu aingie mu kanisa fulani, kuliko hata mambo yenye mutu anapaswa kufanya juu aingie mu bisi.”

Kwa kweli, inaomba kufanya jambo fulani juu ya kubadilisha mambo mu hii dunia. Inaomba kufanya nini? Inaomba kufanya mabadiliko gani? Nani njo atafanya ile mabadiliko, na ataifanya namna gani?

[Wazo ya fungu]

“Mauaji yenye ilifanyika wakati wa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu [1914] ilifanya ionekane sawa uzima wa mwanadamu hauna maana”

[Picha]

Ilishakuwa mwepesi sana, tena sana kupata mambo yakujifurahisha yenye haifae