Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Wanafunzi Waliofadhaika

Wanafunzi Waliofadhaika

Wanafunzi Waliofadhaika

JENNIFER mwenye umri wa miaka 17 alikuwa mmoja kati ya wanafunzi bora kabisa katika darasa lake. Alishiriki katika utendaji mwingi wa baada ya shule na aliheshimiwa na walimu na washauri wa shule. Lakini mwaka mmoja kabla ya kumaliza shule, alianza kuumwa sana na kichwa na kupatwa na kichefuchefu mara nyingi. Anahisi kwamba alikuwa mgonjwa kwa sababu ya saa nyingi alizotumia kukazia sana fikira kazi za shule na kukosa usingizi.

Kuna wanafunzi wengine wengi walio na matatizo kama ya Jennifer. Inaonekana kwamba idadi ya wanafunzi wanaokabili mfadhaiko mwingi shuleni inaongezeka na wengine wanatafuta msaada wa madaktari wa matatizo ya akili. Kwa sababu hiyo, kikundi cha walimu Wamarekani kimeanzisha programu ya kupunguza hali zinazochangia mfadhaiko wa wanafunzi shuleni. Programu hiyo inaitwa Jitahidi Kufanikiwa.

Ikiwa wewe ni mwanafunzi, kama Jennifer huenda unakabili mfadhaiko. Au ikiwa wewe ni mzazi huenda ukaona jinsi mwana au binti yako anavyoshinikizwa sana afaulu shuleni. Wanafunzi na wazazi wanaweza kupata wapi mwongozo unaofaa?