Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Ungejibuje?

Ungejibuje?

Ungejibuje?

Ilitukia Wapi?

1. Tukio hili lilitukia katika jiji gani?

DOKEZO: Soma Matendo 2:1-13.

Chora mviringo kwenye jibu lako katika ramani.

Athene

Yerusalemu

Babiloni

▪ Wanafunzi wengi walitoka eneo gani?

․․․․․

▪ Kwa nini watu fulani waliwadhihaki wanafunzi?

․․․․․

ZUNGUMZENI PAMOJA:

Unapolinganisha simulizi hili na lile lililo katika Mwanzo 11:1-9, unaona mambo gani yanayofanana na yanayotofautiana?

Katika Toleo Hili

Jibu maswali haya na utaje mistari ya Biblia ambayo haijaonyeshwa.

UKURASA WA 4 Mtu anaweza kumezwa na kitu gani? 2 Wakorintho 2:________

UKURASA WA 6 Amani ya Mungu itafanya nini? Wafilipi 4:________

UKURASA WA 28 Watu wengine wana bidii kwa ajili ya Mungu lakini wanakosa nini? Waroma 10:________

UKURASA WA 29 Tunapaswa kumtii nani? Matendo 5:________

Watoto Watafute Picha

Je, unaweza kupata picha hizi katika toleo hili? Kwa maneno yako mwenyewe, eleza jambo linalotendeka katika kila picha.

Unajua Nini Kuhusu Mwamuzi Othnieli?

Soma Waamuzi 3:7-11. Sasa jibu maswali yafuatayo.

2. ․․․․․

Alitoka katika kabila gani?

DOKEZO: Soma Yoshua 15:17, 20.

3. ․․․․․

Alikomboa Israeli kutoka kwa mtawala gani?

4. ․․․․․

Kweli au si kweli? Aliishi kabla ya Musa.

ZUNGUMZENI PAMOJA:

Kalebu aliyekuwa ndugu ya baba ya Othnieli aliweka mfano gani mzuri?

DOKEZO: Soma Hesabu 14:6-9. Taja mtu mmoja wa ukoo wako ambaye unamheshimu, na ueleze ni kwa nini unamheshimu.

▪ Majibu kwenye ukurasa wa 11

MAJIBU YA UKURASA WA 31

1. Yerusalemu.—Matendo 2:5.

▪ Galilaya.—Matendo 2:7.

▪ Walifikiri walikuwa wamelewa.—Matendo 2:13.

2. Yuda.—Yoshua 15:17, 20.

3. Kushan-rishathaimu.—Waamuzi 3:8.

4. Si kweli.