Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Mazungumzo ya Familia

Mazungumzo ya Familia

Mazungumzo ya Familia

Ni Nani Aliyefanya Kazi Hii?

Ni viongozi gani wawili wa Israeli ya kale waliokuwa wachungaji wa kondoo? Andika majibu yako kwenye mistari iliyo hapa chini.

1. Dokezo: Soma Kutoka 3:1.

․․․․․

2. Dokezo: Soma 1 Samweli 17:34-36.

․․․․․

ZUNGUMZENI PAMOJA:

Mchungaji mzuri alipaswa kuwa na sifa gani? Kwa nini Yesu alijifananisha na mchungaji na kuwafananisha wanafunzi wake na kondoo?

DOKEZO: Soma Yohana 10:11-16.

UNAJUA NINI KUHUSU MFALME ASA?

3. Asa alifanya nini mara tu baada ya kuwa mfalme?

DOKEZO: Soma 2 Mambo ya Nyakati 14:2-5.

․․․․․

4. Watu milioni moja waliokuja kupigana na Asa walitoka katika nchi gani?

DOKEZO: Soma 2 Mambo ya Nyakati 14:9, 10.

․․․․․

ZUNGUMZENI PAMOJA:

Asa alitenda jinsi gani aliposhauriwa na Hanani?

DOKEZO: Soma 2 Mambo ya Nyakati 16:7-10.

Je, ilikuwa sawa kwa Asa kutenda kwa njia hiyo? Unapaswa kutenda kwa njia gani unaposhauriwa, na kwa nini?

WATOTO WATAFUTE PICHA

Je, unaweza kupata picha hizi katika toleo hili? Kwa maneno yako mwenyewe, eleza jambo linalotendeka katika kila picha.

KATIKA TOLEO HILI

Jibu maswali haya, na utaje mistari ya Biblia ambayo haijaonyeshwa.

UKURASA WA 20 Dunia nzima inakaa katika nguvu za nani? 1 Yohana 5:________

UKURASA WA 21 Upendo haufanyi nini? Waroma 13: ________

UKURASA WA 26 Tunapaswa kujiepusha na nini? 1 Wathesalonike 4:________

UKURASA WA 26 Mtu anayefanya uasherati anatenda dhambi dhidi ya nini? 1 Wakorintho 6:________

● Majibu kwenye ukurasa wa 22

MAJIBU YA UKURASA WA 31

1. Musa.

2. Daudi.

3. Aliondoa ibada ya uwongo.

4. Ethiopia.