Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Mazungumzo ya Familia

Mazungumzo ya Familia

Mazungumzo ya Familia

Ni Nini Kimekosekana Katika Picha Hii?

Soma Marko 1:9-11. Kisha utazame picha. Ni nini kinachokosekana? Andika majibu yako kwenye mistari iliyo hapa chini na ukamilishe picha hii kwa kuchora vitu vinavyokosekana na kupaka rangi.

1. ․․․․․

2. ․․․․․

ZUNGUMZENI PAMOJA:

Kwa nini Wakristo hubatizwa?

DOKEZO: Soma Marko 8:34; 1 Petro 2:21; 3:21.

Unafikiri unapaswa kuwa na umri wa miaka mingapi ili ubatizwe? Kwa nini unasema hivyo?

UNAJUA NINI KUHUSU MTUME YUDA ISKARIOTE?

3. Yuda alikuwa na pendeleo gani la pekee ambalo hakuna mtume mwingine alipewa?

DOKEZO: Soma Yohana 13:29.

․․․․․

4. Yuda alishindwa na kishawishi gani?

DOKEZO: Soma Yohana 12:6.

․․․․․

ZUNGUMZENI PAMOJA:

Unafikiri ni nini kilichomfanya Yuda afanye dhambi? Unaweza kukabili kishawishi kama hicho wakati gani? Kufikiria kisa cha Yuda kunaweza kukusaidia jinsi gani ufanye maamuzi mazuri?

WATOTO WATAFUTE PICHA

Je, unaweza kupata picha hizi katika toleo hili? Kwa maneno yako mwenyewe, eleza jambo linalotendeka katika kila picha.

KATIKA TOLEO HILI

Jibu maswali haya na utaje mistari ya Biblia ambayo haijaonyeshwa.

UKURASA WA 4 Kila siku ina nini cha kutosha? Mathayo 6:________

UKURASA WA 9 Baba yetu wa mbinguni anaahidi kwamba hatafanya nini kamwe? Waebrania 13:________

UKURASA WA 10 Tangu mwanzo Mungu alikusudia kwamba mwanadamu afanye nini? Marko 10:________

UKURASA WA 29 Wanawake wenye umri mkubwa wanaweza kuwasaidia wanawake wachanga kufanya nini? Tito 2:________

● Majibu kwenye ukurasa wa 17

MAJIBU YA UKURASA WA 31

1. Yohana Mbatizaji.

2. Njiwa.

3. Alitunza sanduku la pesa.

4. Alitaka pesa naye akaziiba.