Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Mazungumzo Ya Familia

Mazungumzo Ya Familia

Mazungumzo Ya Familia

Ni Nini Kimekosekana Katika Picha Hii?

Soma 2 Wafalme 5:1, 9-16, 20-27. Kisha utazame picha. Ni vitu gani vimekosekana? Andika majibu yako kwenye mistari iliyo hapa chini. Unganisha nukta zilizopo ili ukamilishe picha hii, kisha uipake rangi.

1. ․․․․․

2. ․․․․․

3. ․․․․․

[Mchoro]

(Ona nakala iliyochapishwa)

ZUNGUMZENI PAMOJA:

Gehazi alisema mambo gani mawili ya uwongo?

DOKEZO: Soma 2 Wafalme 5:22, 25.

Ni nani aliyejua kwamba Gehazi alikuwa akisema uwongo?

DOKEZO: Soma 2 Wafalme 5:25, 26; 2 Mambo ya Nyakati 16:9; Waebrania 4:13.

Kwa nini unapaswa kuepuka kusema uwongo?

DOKEZO: Soma Methali 12:22; Yohana 8:44.

UTENDAJI WA FAMILIA:

Someni simulizi hilo la Biblia pamoja. Ikiwezekana, mmoja asome sehemu ya msimuliaji, wa pili asome sehemu ya Elisha, wa tatu asome sehemu ya Naamani na watumishi wake, na wanne asome sehemu ya Gehazi.

Kusanya na Ujifunze

Kata, kunja katikati, na uhifadhi

KADI YA BIBLIA 8 HEZEKIA

MASWALI

A. Hezekia alikuwa na umri wa miaka mingapi alipowekwa kuwa mfalme wa Yuda?

B. Yehova alirefusha kimuujiza uhai wa Hezekia kwa miaka mingapi?

C. Jaza mapengo. Kwa sababu ya sala za Hezekia na ushikamanifu wake, Yehova alimtuma malaika akawaua askari-jeshi ․․․․․ wa Ashuru.

[Chati]

4026 B.C.E. 1 W.K. 98 W.K.

Adamu Aumbwa Aliishi miaka Kitabu cha

ya 700 K.W.K. mwisho cha

Biblia

kinaandikwa

[Ramani]

Aliishi Yerusalemu

ASHURU

Yerusalemu

HEZEKIA

MAMBO MACHACHE KUMHUSU

Mfalme mwaminifu ambaye alilifungua tena hekalu na kulirekebisha, akaharibu vifaa vya ibada ya uwongo, na kuwahizimiza watu waadhimishe Pasaka. (2 Wafalme 18:4; 2 Mambo ya Nyakati 29:3; 30:1-6) Licha ya kwamba baba yake, Mfalme Ahazi, alikuwa mfano mbaya, Hezekia ‘aliendelea kushikamana na Yehova.’—2 Wafalme 18:6.

MAJIBU

A. Miaka 25.—2 Wafalme 18:1, 2.

B. Miaka 15.—2 Wafalme 20:1-6.

C. 185,000.—2 Wafalme 19:15, 19, 35, 36.

Watu na Nchi

4. Majina yetu ni Kyrl na Sheen. Tuna umri wa miaka 6 na 9. Tunaishi Filipino. Kuna Mashahidi wangapi wa Yehova nchini Filipino? Ni 62,000, 126,000, au 172,000?

5. Ni alama gani inayoonyesha eneo tunaloishi? Chora duara kuzunguka alama hiyo, na uchore alama nyingine kuonyesha eneo unaloishi kisha uone kwenu ni umbali gani kutoka Filipino.

A

B

C

D

Watoto Watafute Picha

Je, unaweza kupata picha hizi katika toleo hili? Kwa maneno yako mwenyewe, eleza jambo linalotendeka katika kila picha.

● Majibu ya “MAZUNGUMZO YA FAMILIA” kwenye ukurasa wa 20

MAJIBU YA UKURASA WA 30 NA 31

1. Gari la Naamani.

2. Mifuko yenye fedha.

3. Mavazi.

4. 172,000.

5. D.