Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kwa nini uhudhurie mikutano ya Kikristo?

Kwa nini uhudhurie mikutano ya Kikristo?

Vijana Huuliza

Kwa nini uhudhurie mikutano ya Kikristo?

JE, WEWE HUFURAHIA MIKUTANO YA KIKRISTO?

NDIYO → ENDELEA KUHUDHURIA

HAPANA → UNAWEZA KUFANYA NINI ILI UIFURAHIE?

BIBLIA inawaamuru Wakristo wakusanyike pamoja kwa ajili ya ibada. (Waebrania 10:25) Lakini namna gani ikiwa hufurahii kuwa mikutanoni? Namna gani ikiwa unajipata ukiwaza kuhusu mambo ambayo ungekuwa ukifanya mahali pengine? Badili mtazamo wako kwa kujaribu mojawapo ya madokezo yaliyo kwenye kurasa zifuatazo.

1. UWE WA KAWAIDA

Andiko la msingi: “Tusiache ile desturi ya kukutana pamoja, kama vile wengine wanavyofanya.”​—Waebrania 10:25, Biblia Habari Njema.

Kwa nini ufanye kwa ukawaida jambo ambalo hufurahii kulifanya? Kwa ufupi, hiyo ndiyo siri ya kulifurahia! Fikiria jambo hili: Unawezaje kuboresha ustadi wako katika mchezo fulani​—na unawezaje kuufurahia​—ikiwa utafanya mazoezi mara chache tu? Kanuni hiyohiyo inaweza kutumiwa kuhusiana na mikutano ya Kikristo. Kadiri utakavyokuwa wa kawaida mikutanoni, ndivyo utakavyohisi kuwa hali yako ya kiroho inaimarika. Jambo hilo litafanya utamani kuendelea kuhudhuria mikutano!​—Mathayo 5:3.

Madokezo: Baada ya kila mkutano, mwambie angalau msemaji mmoja jambo ambalo umefurahia katika hotuba aliyotoa. Andika kwenye kitabu faida moja uliyopata kwa kuhudhuria mkutano huo. Na kwa kuwa mikutano mingi huzungumzia huduma ya Kikristo, weka mradi wa kuboresha mazungumzo yako na watu wengine kuhusu imani yako. Jambo hilo litafanya habari iliyozungumziwa kwenye mikutano iwe muhimu kwako.

“Tangu utotoni, nilizoezwa kwamba kuhudhuria mikutano ni jambo la lazima. Hata nilipokuwa mdogo, sikuwazia kwamba ningeweza kukosa mikutano. Bado nina mtazamo huo hadi leo.”​—Kelsey.

Jambo kuu: Wale ambao ni wa kawaida mikutanoni huifurahia zaidi​—na wananufaika zaidi!

2. SIKILIZA KWA MAKINI

Andiko la msingi: “Kazieni uangalifu jinsi mnavyosikiliza.”​—Luka 8:18.

Watafiti wanasema kwamba msikilizaji wa kawaida husahau asilimia 60 ya hotuba aliyosikiliza. Kama ungepoteza pesa haraka hivyo, je, hungefanya jambo fulani ili usipate hasara kubwa sana?

Madokezo: Keti pamoja na wazazi wako karibu na jukwaa, mahali ambapo hutakengeushwa kwa urahisi. Andika mambo makuu. Ingawa kila mtu ana njia yake ya kujifunza, kuandika mambo machache kunaweza kukusaidia kumkazia msemaji fikira​—na unaweza kurudia mambo makuu baadaye.

“Zamani, ilikuwa vigumu kwangu kusikiliza kwa makini mikutanoni, lakini sasa nimefanya maendeleo. Ninajaribu kukumbuka sababu iliyofanya nihudhurie. Si desturi tu, kama kwenda kanisani. Ninaenda mikutanoni kuabudu na kujifunzakupata jambo fulani ninaloweza kutumia katika maisha yangu.”​—Kathleen.

Jambo kuu: Kwenda kwenye mkutano na ukose kusikiliza kwa makini ni kama kwenda kwenye karamu halafu usile chochote.

3. JIHUSISHE

Andiko la msingi: “Chuma hunoa chuma, kadhalika mtu hufundishwa na wenzake.”​—Methali 27:17, BHN.

Ukiwa kijana, unatimiza fungu muhimu katika mikutano ya kutaniko. Usidharau thamani ya kuwapo kwako na kushiriki mikutanoni, iwe ni kwa kutoa maelezo wakati wa sehemu ya maswali na majibu au iwe ni kwa kuzungumza na waamini wenzako.

Madokezo: Jiwekee mradi wa kutoa maelezo angalau mara moja wakati wa sehemu ya maswali na majibu. Jitolee kufanya kazi ya usafi au kazi nyingine inayohitaji kufanywa kabla, wakati, au baada ya mkutano. Anzisha mazungumzo pamoja na mtu ambaye kwa kawaida hupati nafasi ya kuongea naye.

“Nikiwa na umri wa miaka 16 hivi, nilijitolea kuzungusha mikrofoni na kutayarisha jukwaa wakati wa mikutano. Migawo hiyo ilinifanya nihisi kuwa ninahitajika, na ilinichochea kufika mapema na kutokosa mikutano. Jambo hilo lilinisaidia kupendezwa sana na mambo ya kiroho.”​—Miles.

Jambo kuu: Usikae kitako tu​—fanya jambo fulani! Kujishughulisha mara zote kunathawabisha kuliko kuwa mtazamaji tu.

Unaweza kupata makala zaidi za “Vijana Huuliza” katika Tovuti ya www.watchtower.org/ype

[Sanduku/​Picha katika ukurasa wa 21]

UNAALIKWA!

Je, ungependa

Kujifunza ukweli kumhusu Mungu?

Kuboresha utu wako?

Kupata marafiki walio bora?

Mikutano ya Mashahidi wa Yehova inaweza kukusaidia kupata mambo hayo yote​—na zaidi! Mashahidi wa Yehova hukutana mara mbili kila juma kwa ajili ya ibada kwenye Majumba yao ya Ufalme. Hakuna sadaka zinazokusanywa, na wageni wote wanakaribishwa.

Usikose kuhudhuria! Majumba ya Ufalme si kama makanisa ambayo umewahi kuingia. Kwenye mikutano ya Mashahidi wa Yehova, elimu ya Biblia ndiyo hukaziwa zaidi, na utajifunza jinsi Neno la Mungu linavyoweza kukusaidia kuishi maisha bora!​—Kumbukumbu la Torati 31:12; Isaya 48:17.

Sai​Nilipoingia kwenye Jumba la Ufalme kwa mara ya kwanza, nilishangaa kwamba hakukuwa na sanamu, hakukuwa na yeyote aliyevalia kama askofu, na hakuna mtu aliyeniambia nitoe pesa. Kila mtu alinikaribisha, na nilijihisi nikiwa salama. Mambo yaliyozungumziwa mikutanoni yalikuwa rahisi kueleweka, na yalipatana na akili. Hiyo ndiyo kweli ambayo nilikuwa nikiitafuta!

Deyanira​Nilikuwa na umri wa miaka 14 nilipoenda kwenye mikutano ya Mashahidi wa Yehova kwa mara ya kwanza. Kila mtu alinikaribisha vizuri. Ilionekana kwamba kila mtu alifurahi kuniona mikutanoni, na walipendezwa nami kikweli. Kwa sababu ya mambo hayo niliyojionea mara ya kwanza, sikuogopa tena kurudi mikutanoni!

[Sanduku katika ukurasa wa 22]

Chunguza ujue ni habari gani itakayozungumziwa kwenye mkutano unaofuata. Chagua sehemu moja ya mkutano inayokupendeza na . . .

KATA NA UTOE NAKALA

Jaza sehemu inayofuata Jaza sehemu inayofuata

kabla ya kwenda mkutanoni. baada ya kusikiliza

sehemu hiyo.

Kichwa cha sehemu hiyo: Mambo niliyojifunza:

․․․․․ ․․․․․

⇩ ⇩

Mambo ninayotaka kujua Jambo nililofurahia katika

kuhusu habari hii: sehemu hiyo ambalo

ninaweza kumtajia msemaji:

․․․․․ ․․․․․