Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAONI YA BIBLIA | Kuzungumuza na Mashetani

Kupashana Habari na Mashetani

Kupashana Habari na Mashetani

Ni vibaya kujaribu kuzungumuza na watu waliokufa?

‘Musiwaendee wenye kuwasiliana na pepo, . . . ili kutiwa unajisi nao.’​—Mambo ya Walawi 19:31.

MAMBO WATU WANASEMA:

Kwa kweli, watu wanapenda kupata uhakika kwamba mutu waliyemupenda ambaye amekufa hateseke. Kwa hiyo wanasema hivi: “Sababu gani tusijaribu kuzungumuza naye kupitia mutu anayepashana habari na mashetani ao muaguzi? Labda mutu huyo anaweza kutupatia utulivu fulani na amani ya akili.”

MAMBO BIBLIA INASEMA:

Biblia inasema waziwazi juu ya watu walio wazima kujaribu kupashana habari na watu waliokufa, tabia ambayo ilienea sana wakati wa zamani. Kwa mufano, Sheria ya Yehova Mungu kwa taifa la Israeli ilisema hivi: ‘Asipatikane ndani yako yeyote anayetafuta shauri kwa mwenye kuwasiliana [kuzungumuza] na pepo ao yeyote anayeuliza habari kutoka kwa wafu. Kwa maana kila mutu anayefanya mambo hayo ni chukizo kwa Yehova.’ (Kumbukumbu la Torati 18:10-12) Biblia inasema pia kwamba watu wanaopashana habari na mashetani kwa njia yoyote ‘hawatauriti ufalme wa Mungu.’​—Wagalatia 5:19-21.

Watu waliokufa wanaweza kuwasaidia walio wazima?

‘Walio hai wanajua kwamba watakufa; lakini wafu, hawajue lolote kamwe.’​—Mhubiri 9:5.

MAMBO WATU WANASEMA:

Watu wengi wanasema kwamba watu waliokufa wanaendelea kuishi kwa njia fulani. Kwa hiyo, wanaweza kujaribu kuzungumuza na watu waliokufa, pengine ili kuwauliza habari ao kuwatuliza ili wasiwasumbue watu walio wazima.

MAMBO BIBLIA INASEMA:

‘Walio hai wanajua kwamba watakufa; lakini wafu, hawajue lolote kamwe. . . . Upendo wao na chuki yao na wivu wao [waliosikia wakati walikuwa wangali hai] tayari zimepotea.’ (Mhubiri 9:5, 6) Kwa kweli, Biblia inafundisha kwamba watu waliokufa wamekufa kabisa! Hawawezi kufikiri, kutenda, wala kumuabudu Mungu. Andiko la Zaburi 115: 17 linasema hivi: ‘Wafu wenyewe hawamusifu [Mungu], wala wowote wanaoingia mahali penye kimya.’

Habari zingine za watu wanaozungumuza na mashetani ni za kweli?

“Je, maombi yatolewe kwa watu waliokufa kwa ajili ya watu walio hai?”​—Isaya 8:19.

MAMBO WATU WANASEMA:

Watu fulani wanasema kwamba watu wanaopashana habari na mashetani wana uwezo wa kufunua habari ambayo ni watu waliokufa na familia yao ao marafiki wao ndio tu wanaweza kuijua.

MAMBO BIBLIA INASEMA:

Sura ya 28 ya kitabu cha 1 Samweli inaeleza namna mufalme Sauli ambaye hakuwa muaminifu alivunja sheria ya Mungu iliyokataza kuwaendea watu wenye kupashana habari na mashetani. Alimuendea mutu mwenye kupashana habari na mashetani, mwanamuke ambaye alionekana kuwa anazungumuza na Samweli, mutu wa Mungu aliyekuwa amekufa! Lakini, je, kwa kweli alizungumuza na Samweli? Hapana! Kwa kweli, mwanamuke huyo alizungumuza na mudanganyifu fulani aliyejifanya kuwa Samweli.

Mudanganyifu huyo alikuwa roho muovu, mujumbe wa Shetani, “baba ya uwongo.” (Yohana 8:44) Sababu gani roho waovu, ao mashetani, wanafanya watu wafikiri kwamba watu waliokufa wanaendelea kuishi? Kusudi lao ni kumusemea Mungu uongo na kufanya watu waizarau Biblia, Neno lake.​—2 Timotheo 3:16.

Je, mambo ambayo tumezungumuzia yanamaanisha kwamba watu waliokufa hawana tumaini lolote? Hapana kabisa! Biblia inaahidi kwamba wakati unaokuja kutakuwa ufufuo wa wale ‘wanaopumuzika’ katika kaburi. * (Yohana 11:11-13; Matendo 24:15) Kwa sasa, tuna uhakika kwamba watu tuliowapenda ambao wamekufa hawateseke kwa njia yoyote.

^ Sura ya 7 ya kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? inasema “Tumaini la Kweli juu ya Watu Tuliowapenda Waliokufa.” Unaweza kusoma kitabu hicho kwenye adresi yetu ya Internete www.pr418.com.