Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

 HABARI KUU | USIKATE TAMAA!

Kwa Sababu Kuna Tumaini

Kwa Sababu Kuna Tumaini

“Wapole wataimiliki dunia, nao watapata furaha yao tele katika wingi wa amani.” —ZABURI 37:11.

Biblia inakiri kwamba maisha ya mwanadamu ni “mafupi na yenye kujaa msukosuko.” (Ayubu 14:1) Leo, sote hupatwa na misiba mbalimbali. Lakini watu wengine huhisi wametamaushwa kabisa na maisha, kana kwamba hakuna tumaini lolote la wakati ujao. Je, unahisi hivyo? Ikiwa ndivyo, uwe na hakika kwamba Biblia inatoa tumaini la kweli kwa ajili yako na wanadamu wote. Kwa mfano:

  • Biblia inafundisha kwamba Yehova Mungu alitaka tuwe na maisha bora.Mwanzo 1:28.

  • Yehova Mungu anaahidi kuifanya dunia yetu iwe paradiso.Isaya 65:21-25.

  • Bila shaka, ahadi hiyo itatimizwa. Andiko la Ufunuo 21:3, 4 linasema:

    “Hema la Mungu liko pamoja na wanadamu, naye atakaa pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Na Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao. Naye atafuta kila chozi kutoka katika macho yao, na kifo hakitakuwapo tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena. Mambo ya zamani yamepitilia mbali.”

Tumaini hilo si ndoto tu. Yehova Mungu amekusudia kulitimiza, naye ana nguvu na nia ya kufanya hivyo. Tumaini la Biblia ni lenye kutegemeka na linakufariji ili “Usikate tamaa!”

KUMBUKA: Ingawa hisia zako zinaweza kubadilika-badilika kama mashua iliyo kwenye bahari yenye msukosuko, tumaini lililo katika Biblia linaweza kuwa kama nanga inayokuimarisha.

UNACHOWEZA KUFANYA SASA: Chunguza yale ambayo Biblia inafundisha kuhusu tumaini la kweli la wakati ujao. Mashahidi wa Yehova watafurahi kukusaidia. Unaweza kuwasiliana nao katika eneo lenu au upate habari muhimu katika Tovuti yao ya jw.org/sw. *

^ fu. 11 Pendekezo: Tembelea jw.org/sw na utafute sehemu ya MACHAPISHO >

MAKTABA KWENYE MTANDAO. Ukiwa hapo tafuta maneno kama vile “kushuka moyo” au “kujiua” ili upate msaada zaidi.