Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

 MAWAZO YA BIBLIA

Sanamu

Sanamu

Watu wengi wanaopenda sana mambo ya Mungu wanaabudu sanamu katika ibada yao. Biblia inakubali zoea hilo? Je, linamupendeza Mungu?

Wayahudi waaminifu wa zamani waliabudu sanamu?

‘Musijifanyie sanamu ya kuchongwa wala umbo [ao sura] lililo kama kitu chochote kilicho juu mbinguni wala kilicho chini duniani wala kilicho ndani ya maji chini ya dunia. Musiviinamie wala kushawishiwa kuvitumikia.’—Kutoka 20:4, 5.

Ibada ya sanamu inakatazwa waziwazi katika Maandiko ya Kiebrania, ambayo watu wengi wanaita Agano la Kale

MAWAZO YA WATU

Kitabu kimoja kinasema kwamba Wayahudi walikuwa na sanamu nyingi walizotumia katika ibada yao “na sanamu hizo ziliheshimiwa sana, na kuabudiwa.” * (New Catholic Encyclopedia) Kwa mufano, kitabu hicho kinataja michoro mingi ya matunda, ya maua, na hata ya wanyama ambayo ilipamba hekalu la Yerusalemu.—1 Wafalme 6:18; 7:36.

MAMBO UNAYOPASWA KUJUA

Tofauti na yale New Catholic Encyclopedia inasema, Wayahudi waaminifu hawakuabudu hata michoro yoyote ao mifano iliyokuwa katika hekalu. Kwa kweli, katika Biblia hakuna andiko linaloonyesha kama Waisraeli waaminifu walitumia sanamu katika ibada yao.

MAWAZO YA BIBLIA

Mungu alisema hivi kupitia nabii Isaya: ‘Sitamupa mwingine yeyote utukufu wangu mwenyewe, wala sitazipa sanamu za kuchongwa sifa yangu.’—Isaya 42:8.

 Wakristo wa kwanza walitumia sanamu katika ibada yao?

‘Hekalu la Mungu lina upatano gani na sanamu? . . . Mwache kugusa kitu kilicho najisi [ao kichafu].2 Wakorintho 6:16, 17.

“Wakristo wa kwanza walichukia sana wazo la kuweka sanamu katika makanisa, na waliona kwamba kuinama ao kusali mbele ya mifano ni ibada ya sanamu.”—Historia ya Kanisa la Kikristo (Kiingereza)

MAWAZO YA WATU

Kitabu kimoja kinasema kwamba “hatuwezi kabisa kusema kwamba Wakristo wa kwanza hawakutumia sanamu katika ibada yao.” (New Catholic Encyclopedia) “Makaburi ya Wakristo yanaonyesha muzuri ufundi wa Wakristo wa kwanza. . . . Hata sanamu za watu wanaozungumuziwa katika hadisi za kutunga zimetiwa katika vyumba vitakatifu vya ibada takatifu na makaburi.” *

MAMBO UNAYOPASWA KUJUA

Sanamu za zamani zilizopatwa katika vijia—sehemu za kupitia za chini ya udongo zilizotumiwa kama mahali pa kuzikia watu—ni za kipindi cha miaka kati ya 201-300 tu. Ilikuwa karibu miaka 200 kisha kifo cha Yesu. Kwa hiyo, ile ambayo kitabu kimoja kinaita “ibada ya Wakristo wa kwanza” haiko ibada ya zamani sana ya Wakristo iliyofanywa na wanafunzi wa kwanza-kwanza na inayoelezwa katika Mandiko ya Kigiriki ya Kikristo, ambayo wengi wanaita Agano Jipya. (New Catholic Encyclopedia) Kupatikana kwa sanamu hizo katika makaburi hayo kunaonyesha tu kwamba katika miaka kati ya 201-300, wale waliojiita kuwa Wakristo walikuwa wameiga tabia ya kipagani ya kutumia sanamu, pengine ili kuwavutia waamini wapya. *

MAWAZO YA BIBLIA

‘Mukimbie ibada ya sanamu.’—1 Wakorintho 10:14.

Sanamu zinaweza kutumiwa tu ili kusaidia mutu katika ibada?

‘Mujilinde na sanamu.’—1 Yohana 5:21.

Biblia haikubali desturi ya kuabudu sanamu. Ndio sababu Mashahidi wa Yehova hawaabudu sanamu, hata hakuna sanamu ya dini katika nyumba zao ao mahali pao pa ibada

MAWAZO YA WATU

Kitabu kimoja kinasema: “Kwa kuwa ibada inayopewa sanamu inaenda na kuishia kwa mutu anayefananishwa na sanamu hiyo, vile vile ibada ambayo mutu huyo anastahili kupewa inaweza kupewa sanamu inayofananisha mutu huyo.” (New Catholic Encyclopedia)

MAMBO UNAYOPASWA KUJUA

Wakati Yesu alifundisha mitume wake namna ya kusali, hakuwaambia watumie sanamu. Wazo la kutumia sanamu ili kumuabudu Mungu wa kweli haliwezi kupatikana katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo.

MAWAZO YA BIBLIA

‘Yehova Mungu wako ndiye unayepaswa kumwabudu, na yeye peke yake ndiye unayepaswa kumutolea utumishi mutakatifu.’—Mathayo 4:10.

^ fu. 7 Kulingana na New Catholic Encyclopedia ibada ni “tendo la kidini, tendo la ibada.”

^ fu. 13 Katika habari hii, neno sanamu linamaanisha picha, michoro, mifano, na vitu vingine vinavyoweza kuabudiwa.

^ fu. 14 Sanamu zilitumiwa sana katika desturi nyingi za zamani, kama zile za Misri, Ugiriki, na India.