Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KICHWA | BIBLIA NI YA MAANA LEO?

Kanuni Zinazotumika Sikuzote na Zenye Kufaa Kila Mutu—Uaminifu

Kanuni Zinazotumika Sikuzote na Zenye Kufaa Kila Mutu—Uaminifu

KANUNI YA BIBLIA: “Ndoa na iheshimiwe kati ya wote, na kitanda cha ndoa kiwe bila unajisi [uchafu].”Waebrania 13:4.

FAIDA: Watu fulani wanaona maneno hayo kuwa yamepitwa na wakati. Lakini wanakosea, wanakosea kabisa! Kukosa uaminifu kunaumiza sana leo kama vile kuliumiza wakati Biblia iliandikwa.​—Methali 6:34, 35.

Jessie, aliye bwana pia baba, aliandika hivi: “Uaminifu katika ndoa umetusaidia sana mimi na bibi yangu kuwa na uhusiano wenye nguvu na umetusaidia pia tukuwe na furaha. Kwa kweli, kutumainiana ni jambo la maana sana katika ndoa. Kukosa uaminifu kunaharibisha hali hiyo ya kutumainiana,” na hata kunaletea watoto matokeo mabaya!

Ligaya * alitia ndoa yake katika hatari. Anasema hivi: “Nilianza kufanya urafiki na watu wabaya. Hilo lilifanya nianze maisha ya kutoka-toka usiku na kukosa uaminifu kwa bwana yangu.” Je, maisha hayo yalimuletea furaha? Yeye na bwana yake walibishana kila wakati, na alikosa furaha kabisa. Anaongeza hivi: “Wakati ninakumbuka hali mbaya yenye kuleta haya yenye mimi mwenyewe nilikuwa nimejiingiza ndani, ninatambua kuwa wazazi wangu walikuwa na sheria wakati walikuwa wanasema, ‘Mashirika mabaya yanaharibu tabia nzuri.’”—1 Wakorintho 15:33.

Ligaya anaendelea kusema hivi: “Mbele mambo yaharibike sana, niliamua kuacha tabia yangu mbaya na kujifunza Biblia, na mara hiyo kutumikisha mambo nilikuwa ninajifunza.” Matokeo yalikuwa gani? Aliokoa ndoa yake, na bwana yake akaanza kumutendea muzuri na kwa heshima. Anasema hivi: “Biblia ilibadilisha maisha yangu na sihuzunike kwa sababu niliacha tabia yangu ya zamani na wale walioitwa kuwa marafiki.”

^ fu. 6 Majina fulani yamebadilishwa.