Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAMBO TUNAYOJIFUNZA KUTOKANA NA HISTORIA

Al-Khwarizmi

Al-Khwarizmi

WAKATI watu wanapima kilo yao, ao wanataka kujua bei ya chakula chenye wamenunua, mara nyingi wanatumia namba za Kihindu na Kiarabu. Sababu gani zinaitwa “namba za Kihindu na Kiarabu”? Inawezekana namna ya leo ya kuhesabu yenye kutumia namba zero mupaka kenda ilianzia India. Na inawezekana ni wasomi wenye walikuwa wanaandika katika Kiarabu katika kipindi cha enzi ya kati (mwaka wa 476-1500 hivi) ndio walizifikisha katika inchi za Mangaribi. Kati ya wasomi hao, mwenye kujulikana sana ni mwanaume anayeitwa Muhammad ibn-Musa al-Khwarizmi. Inawezekana alizaliwa katika inchi yenye kujulikana leo kuwa Uzbekistan katika mwaka wa 780 hivi kisha kuzaliwa kwa Yesu.Al-Khwarizmi anaitwa “shujaa mukubwa wa hesabu za Kiarabu.” Sababu gani alipewa sifa hiyo?

“SHUJAA WA HESABU ZA KIARABU”

Al-Khwarizmi aliandika juu ya namna ya kutumia muzuri desimali, alifasiria wazi njia ya kufanya hesabu fulani ngumu, na kufanya watu wengi waanze kuitumia. Alifasiria njia hiyo katika kitabu chake The Book of Restoring and Balancing. Neno la Kiswahili aljebra linatoka katika neno la Kiarabu al-jabr lenye alitumia katika jina la kitabu hicho katika Kiarabu. (Kitab al-jabr wa’l-muqabala) Ehsan Masood, muandikaji wa mambo ya sayansi, alisema kama Aljebra inaonwa kuwa “chombo cha maana sana katika hesabu chenye kimekwisha kutokea, na inaunga mukono kila sehemu ya sayansi.” *

Muandikaji mumoja anasema kama “wanafunzi wengi wa masomo ya juu wangefurahi ikiwa [al-Khwarizmi] hakuleta hesabu hizo.” Hata kama zinaonwa kuwa ngumu, al-Khwarizmi alisema kusudi lake lilikuwa kufasiria njia nyepesi za kufanya hesabu katika biashara, kugawanya uriti, kupima vitu, na mambo mengine.

Miaka mingi kisha hapo, watu wenye elimu ya hesabu wa inchi za Mangaribi, kama vile Galileo na Fibonacci, walimuheshimia sana al-Khwarizmi kwa sababu ya mafasirio ya wazi yenye alitoa juu ya namna ya kutumia hesabu za kulinganisha (équations). Mafasirio ya Al-Khwarizmi yalisaidia baadaye katika aljebra, trigonometria, na katika hesabu za kuongeza, kupunguza, kugawanya, na kuzidisha. Trigonometria ilisaidia wasomi wa inchi za Mashariki ya Kati kupima pembe na pande za pembetatu (triangle), na kujifunza zaidi juu ya nyota. *

Aljebra: “Chombo cha maana sana katika hesabu chenye kimekwisha kutokea”

Watu wenye walitumikisha mambo yenye al-Khwarizmi alifanya walianzisha njia mupya za kufanya hesabu zenye kuwa na desimali, na za kupima ukubwa wa eneo ao wa vitu. Watu wa Mashariki ya Kati wenye kuchapa plans za nyumba na wajenzi, walianza kutumia njia hizo mupya mbele ya wenzao wa inchi za Mangaribi, ambao walizijua wakati wa Vita vya Dini. Walirudi kwao na mambo yenye walikuwa wamejifunza. Walisaidiwa na Waislamu wenye elimu waliokamatwa katika vita hiyo na wengine waliohamia katika inchi za Mangaribi.

HESABU ZA KIARABU ZINAFIKA KATIKA INCHI NYINGI

Kisha wakati fulani, vitabu vya al-Khwarizmi vilitafsiriwa katika Kilatini. Fibonacci (mwaka wa 1170-1250 hivi), Muitaliano mwenye elimu ya hesabu, ambaye pia anajulikana kwa jina la Leonardo wa Pisa, alifanya watu wengi waanze kutumia namba za Kihindu na Kiarabu katika inchi za Mangaribi. Alijifunza namba hizo wakati wa safari zake katika inchi za Mediterania na kisha aliandika kitabu chake Book of Calculation.

Kulipita miaka mingi mbele ya watu kujua muzuri mafasirio ya Al-Khwarizmi. Lakini leo, njia zake za hesabu na namna nyingine za kufanya hesabu zenye watu wamevumbua kwa kutumia njia za Al-Khwarizmi, ni mambo ya maana sana katika sayansi na teknolojia, bila kusahau biashara na kazi za kutengeneza vitu.

^ fu. 5 Katika hesabu za leo, herufi kama vile x ao y zinatiwa mahali pa namba fulani zenye hazijulikane. Kwa mufano, x + 4 = 6. Ukitosha 4 pande zote mbili, utaona kuwa x ilitiwa mahali pa 2.

^ fu. 7 Wagiriki fulani wenye kujifunza juu ya nyota walikuwa wa kwanza kupima pande na pembe za pembetatu. Wasomi Waislamu walitumia trigonometria ili kujua ni wapi muji wa Meka, ambao ni muji mutakatifu katika dini ya Waislamu, unapatikana. Waislamu wanapenda kuangalia Meka wakati wanasali. Kulingana na desturi zao, maiti yenye kuzikwa inapaswa kuelekea Meka na Waislamu wenye kuchinja wanyama kwa ajili ya chakula wanapaswa kuangalia muji huo. Tena Waislamu wanapenda kuangalia Meka wakati wanachinja wanyama kwa ajili ya chakula.