Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI FULANI ZA ULIMWENGU

Habari Fulani Juu ya Uhusiano na Wengine

Habari Fulani Juu ya Uhusiano na Wengine

Juu ya uhusiano na wengine, Biblia ndiyo nafasi ya kwanza unaweza kutafutia shauri, ao pengine ndiyo nafasi ya mwisho? Ona namna hekima ya Biblia ya tangu zamani inapatana na uchunguzi wa hivi karibuni.

India

Kulingana na uchunguzi moja wa 2014, vijana 61 juu ya 100 wenye miaka kati ya 18 na 25, wanaamini kuwa kufanya ngono mbele ya kufunga ndoa “haliko tena tatizo kubwa katika inchi ya India.” Munganga mumoja katika muji wa Mumbai aliambia gazeti Hindustan Times kama, kwa mawazo yake, “kuanzisha urafiki wa kimapenzi hakumaanishe kama vijana wako na wazo juu ya ndoa. Ikuwe ni kufanya ngono kwa usiku moja, urafiki wa kijuu-juu ao wa kuendelea, haiko lazima wafanye mapatano ya ndoa.”

FIKIRIA JAMBO HILI: Magonjwa yenye kuambukizwa kupitia ngono na mahangaiko ya moyo yanatokea zaidi kwa sababu ya kufanya ngono mbele ya kufunga ndoa ao kisha kufunga ndoa?—1 Wakorintho 6:18.

Denmaki

Kubishana mara nyingi na watu wa familia kunaongeza mara mbili uwezekano wa kufa kati ya miaka 35 na 50. Kwa kipindi cha miaka 11, wachunguzi kwenye masomo ya juu ya Copenhague walifanya uchunguzi juu ya watu karibu 10000 wenye miaka kati ya 35 na 50. Walitambua kama watu wenye walikuwa wanazoea kubishana na mutu wa familia yao, walikuwa katika hatari zaidi ya kufa haraka kuliko wale wenye hawakuzoea kukosana. Muandikaji mumoja wa uchunguzi huo anasema kama kupambana muzuri na mahangaiko, kushugulikia mambo yenye tunaombwa kutimiza, na kupambana muzuri na hali za kukosa kuelewana “kunaweza kuonwa kuwa njia za maana za kupunguza vifo vya haraka.”

BIBLIA INASEMA HIVI: ‘Yeyote anayezuia maneno yake ana ujuzi, na mutu mwenye utambuzi ana roho ya utulivu.’—Methali 17:27.

Inchi ya Amerika

Uchunguzi moja wa hivi karibuni, wenye ulifanywa katika jimbo la Louisiana juu ya ndoa 564 za watu wenye walitokea kuoana, unaonyesha kama watu wenye wanaachana na kurudishana tena na tena katika uchumba, wako na uwezekano zaidi wa kuachana katika miaka tano ya kwanza ya ndoa yao. Tena, inawezekana wakuwe na matatizo mengi ya kukosa kuelewana na wasifurahie sana ndoa yao.

BIBLIA INASEMA HIVI: ‘Kile ambacho Mungu ameunganisha [katika ndoa] mutu yeyote asikitenganishe.’—Mathayo 19:6.