Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Jina la Mungu la pekee lenye kuandikwa katika herufi ya Kiebrania ya zamani linapatikana mara nyingi katika maandishi ya zamani ya Biblia

MAWAZO YA BIBLIA

Jina la Mungu

Jina la Mungu

Mamilioni ya watu wanazungumuza na Mungu kwa kutumia majina yake ya cheo, kama vile Bwana, Allah, ao tu Mungu. Lakini, Mungu iko na jina lake la pekee. Unapaswa kulitumia?

Jina la Mungu ni nani?

MAMBO WATU FULANI WANASEMA

 

Watu wengi wenye kujiita Wakristo wanaamini kwamba jina la Mungu ni Yesu. Wengine wanawaza kwamba kwa sababu kuko Mungu Mweza-Yote mumoja tu, haiko lazima kutumia jina lake la pekee. Tena wengine wanasema kwamba haifae kutumia jina la Mungu.

MAMBO BIBLIA INASEMA

 

Jina la Mungu Mweza-Yote haiko Yesu, kwa sababu Yesu haiko Mungu Mweza-Yote. Lakini, Yesu alifundisha waabudu wenzake kusali Mungu kwa kusema hivi: “Baba, jina lako na litakaswe.” (Luka 11:2) Yesu mwenyewe alisali Mungu kwa kusema: “Baba, litukuze jina lako.”​Yohana 12:28.

Katika Biblia, Mungu anasema hivi: ‘Mimi ni Yehova. Hilo ni jina langu, nami sitamupa mwingine yeyote utukufu wangu mwenyewe.’ (Isaya 42:8) “Yehova” ni tafsiri ya Kiswahili ya herufi ine za Kiebrania YHWH, zenye kufanyiza jina la Mungu. Jina hilo linapatikana mara 7000 hivi katika Maandiko ya Kiebrania. * Jina hilo linatumiwa mara nyingi kuliko jina lingine lolote la cheo, kama vile “Mungu” “Mweza-Yote,” ao “Bwana,” na mara nyingi zaidi kuliko jina lingine lolote, kama vile Abrahamu, Musa, ao Daudi.

Katika Biblia, hakuna kwenye Yehova anakataza watu kutumia jina lake kwa njia ya heshima. Lakini, Maandiko yanaonyesha kwamba watumishi wa Mungu walijisikia huru kutumia jina lake. Walilitia katika majina ya watoto wao, kama vile Eliya, jina lenye kumaanisha “Mungu wangu ni Yehova,” na Zekaria, jina lenye kumaanisha “Yehova Amekumbuka.” Na hawakusita kutumia jina la Mungu katika mazungumuzo ya kila siku.​—Ruthu 2:4.

Mungu anapenda tutumie jina lake. Tunatiwa moyo ‘kumushukuru Yehova, na kuliitia jina lake.’ (Zaburi 105:1) Yehova anatambua muzuri hata wale “wanaolifikiria jina lake.”​—Malaki 3:16.

“Ili watu wajue kwamba wewe, ambaye jina lako ni Yehova, Wewe peke yako ndiye Uliye Juu Zaidi, juu ya dunia yote.”​Zaburi 83:18.

Jina la Mungu linamaanisha nini?

Watu fulani wa elimu ya Biblia wanaamini kwamba katika Kiebrania jina Yehova linamaanisha “Yeye Anafanya Kuwa.” Maana hiyo inaonyesha kwamba Mungu anaweza kujifanya mwenyewe ao uumbaji wake kuwa jambo la lazima ili kutimiza mapenzi yake. Ni Muumbaji Mweza-Yote tu ndiye anastahili kubeba jina hilo.

NAMNA JAMBO HILO LINAKUHUSU

 

Kujua jina la Mungu kutabadilisha mawazo yako juu yake. Hilo litafanya ikuwe mwepesi zaidi kumukaribia. Kwa kweli, inawezekana kuwa rafiki ya mutu mwenye haujue jina lake? Kwa kuwa Yehova amekufunulia jina lake katika Biblia, anapenda umukaribie.​—Yakobo 4:8.

Ukuwe hakika kwamba Yehova atatenda sikuzote kulingana na jina lake akiwa Mungu mwenye kutimiza ahadi zake. Ndio sababu Biblia inasema: “Wale wanaolijua jina lako watakutegemea.” (Zaburi 9:10) Utafikia kuwa na tumaini kama hiyo kadiri unajifunza kwamba jina la Mungu linapatana sana na sifa zake, kama vile upendo mushikamanifu, rehema, huruma, na haki. (Kutoka 34:5-7) Inatia moyo sana kujua kwamba Yehova anatimiza sikuzote ahadi zake, hatatenda hata kidogo tofauti na sifa zake.

Ni wazi kwamba kujua jina la Mungu Mweza-Yote ni pendeleo. Kunaweza kukuletea baraka leo na wakati wenye kuja. Mungu anaahidi hivi: ‘Nitamulinda kwa sababu amelijua jina langu.’​—Zaburi 91:14.

‘Kila mutu anayeliitia jina la Yehova ataokoka.’​—Yoeli 2:32.

Namna jina la Mungu linatafsiriwa katika luga mbalimbali

^ fu. 9 Tafsiri nyingi za Biblia zinaondoa jina la Mungu na kutia pa nafasi hizo jina la cheo kama vile “BWANA” katika herufi kubwa, lakini tafsiri zingine zinatia jina la Mungu katika maandiko fulani tu ao katika maelezo ya chini. Biblia Takatifu Tafsiri ya Ulimwengu Mpya inatumia sana jina la Mungu kotekote katika maandiko.