Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Mazungumuzo ni kama kilalo chenye kinakuunganisha na watoto wako

KWA AJILI YA WAZAZI

5: Mazungumuzo

5: Mazungumuzo

MAANA YAKE NINI?

Mazungumuzo ya kweli yanafanyika wakati kunakuwa ubadilishanaji wa mawazo na namna kila mutu anajisikia kati yako na watoto wako.

SABABU GANI NI JAMBO LA MAANA

Inaweza kuwa nguvu kuzungumuza na vijana, zaidi sana vijana wa miaka kati ya 13 na 19. Pengine zamani kidogo kama vile Kitabu Décryptage kinasema, “ni kama vile ulikuwa na ruhusa ya kujua mambo ya siri katika maisha ya watoto wako.” Kinasema pia kuwa ni kama vile hawakuambie mengi na pengine wanaweza hata kuambia wengine mambo yenye hawatakuambia. Lakini, hata kama inaonekana kuwa watoto wako hawapendi kuzungumuza, huo ndio wakati wako na lazima sana ya kuzungumuza!

MAMBO YENYE UNAWEZA KUFANYA

Zungumuza na mutoto wakati wowote wenye anapenda. Fanya hivyo hata kama ni usiku sana.

“Inawezekana useme, ‘Sasa ndio wakati unapenda tuongee? Tulikuwa pamoja muchana wote!’ Lakini hatutanungunika ikiwa mutoto anapenda kutuambia mambo yenye kuwa katika moyo wake. Hilo ndilo jambo lenye kila muzazi anapenda mutoto wake afanye, haiko vile?”​—Lisa.

“Hata kama ninapenda kulala mbele ya wakati, mazungumuzo ya muzuri zaidi yenye nimekwisha kufanya na watoto wangu, yalifanyika kisha katikati ya usiku.”​—Herbert.

KANUNI YA BIBLIA: ‘Kila mumoja na aendelee kutafuta, si faida yake mwenyewe, bali [ao, lakini] ile ya ule mutu mwengine.’​—1 Wakorintho 10:24.

Usiruhusu mambo mengine yakukengeushe. Baba mumoja anasema hivi: “Wakati fulani ninajikuta niko ninafikiria mambo mengine wakati watoto wangu wako wanaongea na mimi. Na hata kama siwakataze kuongea, wanaweza kuona kama niko ninafikiria mambo mengine na kwamba siwasikilize!”

Ikiwa unakengeushwa na televizyo ao vyombo vingine vya kielektronike kama vile telefone, uzime vyombo hivyo ao uviweke pembeni. Kaza akili juu ya mambo yenye mutoto wako iko anasema, na uone mahangaiko yake kuwa yanastahili kukaziwa uangalifu, hata kama yanaweza kuonekana kuwa hayako ya maana sana kwako.

“Tunapaswa kuhakikishia watoto wetu kuwa tunahangaikia sana namna wanajisikia. Ikiwa hawaone kuwa tunawahangaikia, hawatatuambia mambo yenye kuwahangaisha, wanaweza hata kuambia watu wengine.”​—Maranda.

“Usikasirike, hata kama mawazo ya mutoto wako hayako ya muzuri kabisa.”​—Anthony.

KANUNI YA BIBLIA: ‘Mukazie uangalifu jinsi [ao, namna] munasikiliza.’​—Luka 8:18.

Tumia nafasi zenye kujitokeza wakati munafanya mambo mengine. Wakati fulani ni mwepesi sana watoto waongee ikiwa wanakaa bila kuangaliana uso kwa uso na muzazi.

“Tunatumia nafasi ya kuzungumuza wakati tuko ndani ya motokari tukienda mahali fulani. Kukaa mumoja pembeni ya mwingine kuliko kukaa tukiangaliana uso kwa uso kumefanya tukuwe na mazungumuzo ya muzuri.”​—Nicole.

Nafasi ingine ya muzuri yenye munaweza kutumia ili kuzungumuza ni wakati muko munatumia chakula.

“Wakati tunatumia chakula mangaribi, kila mumoja wetu anazungumuzia jambo la mubaya ao la muzuri lenye lilitokea siku hiyo. Kufanya hivyo kunatuunganisha na kunafanya kila mumoja wetu ajue kuwa hatupaswe kupambana na magumu peke yetu.”​—Robin.

KANUNI YA BIBLIA: ‘Ukuwe mwepesi kuhusu kusikia [na] si mwepesi wa kusema.’​—Yakobo 1:19.