Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Nizamu inaongoza mutoto kama vile chombo cha kuongoza mashua kinaiongoza na kuifanya ifuate njia

KWA AJILI YA WAZAZI

6: Nizamu

6: Nizamu

MAANA YAKE NINI?

Neno nizamu linaweza kumaanisha kuongoza ao kufundisha. Wakati fulani, neno hilo linatia ndani kurekebisha tabia ya mubaya ya mutoto. Lakini mara nyingi, inatia ndani kumutolea mutoto mbele ya wakati mafundisho kuhusu mwenendo yenye yatamusaidia ajifanyie maamuzi ya muzuri.

SABABU GANI NI JAMBO LA MAANA

Katika miaka ya hivi karibuni, wazazi fulani hawatolee kabisa nizamu watoto wao, kwa sababu wanaogopa kuwa kuwarekebisha kunaweza kufanya watoto wajione kuwa hawafae kitu. Lakini wazazi wenye hekima wanatolea watoto wao sheria zenye kufaa na wanawafundisha kuishi kulingana na sheria hizo.

“Watoto wako na lazima waambiwe kile wanaruhusiwa kufanya na kile hawaruhusiwe kufanya ili kuwasaidia wakuwe watu wazima wenye usawaziko. Bila nizamu, watoto wako kama mashua yenye kukosa chombo cha kuiongoza. Wanaweza kufikia kukamata maamuzi ya mubaya yenye yatafanya wapatwe na matokeo ya mubaya.”​—Pamela.

MAMBO YENYE UNAWEZA KUFANYA

Usikuwe mwenye kubadilika-badilika katika maamuzi yako. Ikiwa mutoto wako hatii sheria zenye ulimuwekea, hakikisha kuwa anapata malipizi. Kwa upande mwengine, ukuwe tayari kupongeza mutoto wako wakati anafuata sheria hizo.

“Kila mara ninapongeza watoto wangu kwa kuwa watiifu katika ulimwengu wenye watu wengi hawako tayari kutii. Kupongeza watoto kunafanya ikuwe mwepesi kwao kukubali kurekebishwa wakati ni lazima kufanya hivyo.”​—Christine.

KANUNI YA BIBLIA: ‘Lolote lile analopanda mutu, atavuna hilo pia.’​—Wagalatia 6:7.

Ukuwe na usawaziko. Nizamu ilingane na miaka ya mutoto, uwezo wake, na uzito wa kosa lenye alifanya. Kwa kawaida nizamu inaleta matokeo ya muzuri zaidi wakati inalingana na kosa lenye lilifanywa. Kwa mufano, ikiwa mutoto anatumikisha telefone mubaya, hilo linaweza kufanya muzazi amunyanganye telefone ao kumutilia mipaka kuhusu namna ya kuitumia. Kwa wakati huohuo, uepuke kuvurugika juu ya jambo fulani lenye haliko la maana kwa sababu tu linakukasirikisha.

“Ninajikaza kutambua ikiwa mutoto wangu alikosa kutii kimakusudi ao ikiwa alikosea kwa sababu tu ya kudanganyika. Kuko tofauti kati ya tabia ya mubaya yenye inaombwa kurekebisha na kosa lenye lilifanywa bila kujua.”​—Wendell.

KANUNI YA BIBLIA: ‘Musiwe mukiwakasirisha watoto wenu, ili wasivunjike moyo.’​—Wakolosai 3:21.

Ukuwe mwenye upendo. Ni mwepesi zaidi watoto wakubali nizamu na kuifuata ikiwa wanajua kama muzazi anachochewa na upendo wakati anatoa nizamu hiyo.

“Wakati mutoto wetu mwanaume alifanya makosa, tulimuhakikishia kuwa tulifurahia maamuzi yote ya muzuri yenye alifanya zamani. Tulimufasiria kama kosa lake halitamuharibishia sifa yake ikiwa anafanya mabadiliko na kwamba tuko tayari kumusaidia kufanya hivyo.”​—Daniel.

KANUNI YA BIBLIA: ‘Upendo ni wenye ustahimilivu [ao, uvumilivu] na wenye fazili.’​—1 Wakorintho 13:4.