Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ni hatua za namna gani zenye unaachia watoto wako wafuate??

KWA AJILI YA WAZAZI

8: Onyesha Mufano

8: Onyesha Mufano

MAANA YAKE NINI?

Wazazi wenye kuonyesha mufano wanaishi kulingana na mambo yenye wanafundisha. Kwa mufano, hauwezi kutazamia mutoto wako akuwe anasema kweli ikiwa siku moja wakati haukupenda kuongea na mutu mwenye alikuja kukuona, mutoto alikusikia unasema, “Umuambie kama nimetoka.”

“Watu wengi wanasema ‘Ufanye kile ninasema, hapana kile ninafanya.’ Lakini hilo haliwezi kusaidia watoto. Watoto wako kama sifongo (chiffon) yenye kunyonya kila kitu chenye tunasema ao kufanya, na wanaweza kutuambia wakati mambo yenye tunafanya hayapatane na mambo yenye tunajaribu kuwafundisha.”​—David.

KANUNI YA BIBLIA: “Wewe, unayehubiri ‘Usiibe,’ je, wewe unaiba?”​—Waroma 2:21.

SABABU GANI NI JAMBO LA MAANA

Watoto na hata vijana wenye kuwa na miaka kati ya 13 na 19 wanachochewa zaidi sana na wazazi wao kuliko mutu mwingine yeyote​—kutia ndani watoto ao vijana wenzao. Hilo linamaanisha kuwa wewe ndiye uko na nafasi ya muzuri zaidi ya kuongoza watoto wako katika njia ya muzuri; ikiwa tu unatenda kulingana na mambo yenye unafundisha.

“Tunaweza kusema jambo fulani mara nyingi na kujiuliza ikiwa mutoto wetu iko anasikiliza, lakini wakati tu tunashindwa kufanya vile tulisema, mutoto atatukumbusha jambo hilo. Watoto wanaangalia kila kitu tunafanya, hata kama tunawaza kuwa hawaangalie.”​—Nicole.

KANUNI YA BIBLIA: “Hekima inayotoka juu . . . si ya kinafiki.”​—Yakobo 3:17.

MAMBO YENYE UNAWEZA KUFANYA

Chunguza kanuni zako mwenyewe. Ni mambo gani ya kujifurahisha yenye unaangaliaka? Unatendea namna gani bibi ao bwana yako na watoto wako? Marafiki wako ni watu wa namna gani? Unafikiriaka watu wengine? Kwa kifupi, uko na sifa zenye unapenda watoto wako wakuwe nazo?

“Mimi na bwana yangu hatuambie watoto wetu wafuate kanuni zenye sisi wenyewe hatufuate.”​—Christine.

Omba musamaha wakati unafanya makosa. Watoto wako wamekwisha kujua kama haukamilike. Kwa kusema “munisamahe” wakati unakosea ​—ikuwe bibi ao bwana yako ao watoto​—unawafundisha somo la maana la kusema kweli na kuwa munyenyekevu.

“Watoto wetu wanapaswa kusikia vile tunakubali makosa yetu na kuomba musamaha juu ya makosa yetu. Ikiwa hatufanye vile, hawatakuwa wanakubali wakati wanafanya makosa.”​—Robin.

“Tukiwa wazazi, mambo yenye tunafanya yako na matokeo makubwa zaidi juu ya watoto wetu, na mufano wetu ni njia ya muzuri zaidi yenye tunaweza kutumia kwa sababu kila wakati wanaona mufano wetu. Ni kama vile wanafundishwa kila wakati kupitia namna wazazi wao wanaishi.”​—Wendell.