Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Miradi iko kama plani ya nyumba; ikiwa unajikaza, unaweza kuifanya ikuwe kweli

KWA AJILI YA VIJANA

12: Miradi

12: Miradi

MAANA YAKE NINI?

Muradi ni zaidi ya kuwa tu na ndoto, ni kusema, kitu fulani chenye ungependa kifanyike. Miradi ya kweli inatia ndani kuwa na mupango, kubadilika kulingana na hali, na kutumika kwa bidii bila kutafuta njia za haraka-haraka ili kufikia miradi hiyo.

Miradi inaweza kuwa ya muda mufupi (yenye mutu anaweza kutimiza katika siku fulani ao majuma fulani), ya muda wa kadiri (yenye mutu anaweza kutimiza katika miezi), na ya muda murefu (yenye mutu anaweza kutimiza katika mwaka moja ao zaidi). Mutu anaweza kutimiza miradi ya muda murefu ikiwa anatimiza kwanza miradi mbalimbali ya muda mufupi na ya muda wa kadiri.

SABABU GANI NI JAMBO LA MAANA

Kutimiza miradi kunaweza kukufanya ujiaminie zaidi, kutia nguvu urafiki wako pamoja na wengine, na kukufanya ukuwe mwenye furaha zaidi.

Kujiaminia: Wakati unajiwekea miradi ya kidogo-kidogo na kuitimiza, unapata nguvu ya kujiwekea miradi mikubwa zaidi. Unapata pia nguvu ya kupambana na magumu ya kila siku​—kama vile kupinga mikazo kutoka kwa watu wengine.

Urafiki: Watu wanafurahia kuzungukwa na watu wenye wanajiwekea miradi yenye usawaziko​—ni kusema, wale wenye wanajua kile wanataka na ambao wako tayari kutumika ili kukitimiza. Zaidi ya hilo, moja kati ya njia zenye zinaweza kukusaidia kutia nguvu urafiki wako pamoja na wengine ni kutumika na mutu mwingine mwenye iko na muradi kama wako.

Furaha: Wakati unajiwekea muradi na kuutimiza, hilo linakuletea furaha kubwa.

“Napendaka kujiwekea miradi. Inanisaidia nikuwe na mengi ya kufanya na kunitolea jambo fulani lenye ninaendelea kujikaza kutimiza. Na wakati mutu anatimiza muradi fulani, inafurahisha sana kuangalia nyuma na kusema, ‘Oh, nilitimiza kabisa muradi wangu! Nimetimiza mambo yenye nilisema nitafanya.’”​—Christopher .

KANUNI YA BIBLIA: “Anayeuangalia upepo hatapanda mbegu; naye anayetazama mawingu hatavuna.”​—Mhubiri 11:4.

MAMBO YENYE UNAWEZA KUFANYA

Fuata hatua hizi ili kujiwekea miradi na kuitimiza.

Tambua miradi yenye unapenda kutimiza. Fanya liste ya miradi yenye ungependa kutimiza, na uanze na miradi ya maana zaidi​—kwa kuchagua muradi wa kwanza wenye unapenda kutimiza, wa pili, wa tatu, na kuendelea.

Fanya mipango. Kwa ajili ya kila muradi, fanya mambo yenye kufuata:

  • Uweke tarehe ya kweli yenye unapenda kutimiza muradi huo.

  • Panga hatua zenye zitakusaidia kutimiza muradi huo.

  • Fikiria mbele ya wakati vizuizi, na ufikirie namna ya kuvishinda.

Tenda. Usingojee mupaka wakati utapata kila kitu ili uanze. Ujiulize, ‘Ni jambo gani la kwanza kabisa ninaweza kufanya lenye litanisaidia kutimiza muradi wangu?’ Kisha ufanye jambo hilo. Chunguza maendeleo yako kisha kutimiza kila hatua.

KANUNI YA BIBLIA: “Mipango ya mwenye bidii bila shaka inaleta faida.”​—Methali 21:5.