Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

UNAWEZA KUKABILIANA NA MKAZO—JINSI GANI?

Je, Una Mkazo?

Je, Una Mkazo?

“Kila mtu ana mkazo kwa kadiri fulani, ila mimi nahisi ninalemewa sana na mkazo. Mkazo nilionao hausababishwi na jambo moja kubwa bali na mambo mengi ninayokabili; mahangaiko ya kila siku na kumtunza kwa miaka mingi mume wangu ambaye inaonekana hatapona matatizo yake ya kimwili na kiakili.”—Jill. a

“Mke wangu aliniacha, na nililazimika kuwalea watoto wawili peke yangu. Haikuwa rahisi kulea watoto nikiwa mwenyewe. Zaidi ya hilo nilifutwa kazi na sikuwa na pesa za kutosha kurekebisha gari langu. Sikujua nifanye nini. Mkazo ulinilemea sana. Moyoni nilijua kwamba ni vibaya kujiua, kwa hiyo nilimwambia Mungu kwamba bora nife.”—Barry.

Kama Jill na Barry, je, wakati mwingine wewe huhisi umelemewa na mkazo? Ikiwa ndivyo, tunatumaini kwamba makala zinazofuata zitakufariji na kukusaidia. Makala hizo zinaeleza baadhi ya mambo yanayosababisha mkazo, jinsi mkazo unavyotuathiri, na jinsi tunavyoweza kupunguza mkazo kwa kadiri fulani.

a Baadhi majina yamebadilishwa.