Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KITULIZO KWA WALE WENYE KUWA NA MUKAZO

Uko na Mukazo?

Uko na Mukazo?

“Kila mutu iko na mukazo (ao, stress) kwa kiasi fulani, lakini mukazo wenye niko nao unavuka mipaka. Mukazo wenye niko nao hauletwe tu na tatizo moja kubwa, lakini unaletwa na hali mingi, magumu, na pia miaka mingi yenye inaonekana kama haina mwisho ya kumuhangaikia bwana yangu mwenye ni mugonjwa kimwili na kiakili.”​—Jill. a

“Bibi yangu aliniacha, na nililazimika kuchunga watoto wawili peke yangu. Haikuwa mwepesi kufanya vile. Zaidi ya ile, nilipoteza kazi yangu, na sikuwa na feza za kutosha ili kutengeneza gari yangu. Sikujua nifanye nini. Nililemewa sana na mukazo. Nilijua muzuri kama ilikuwa mubaya kujiua, kwa hiyo nilimuomba Mungu aniache nikufe.”​—Barry.

Kama vile Jill na Barry, wakati fulani unajisikia kuwa unalemewa na mukazo? Ikiwa ni vile, tunatumaini kama habari zenye kufuata zitakutolea kitulizo na kukusaidia. Zinazungumuzia mambo yenye mara mingi inaleta mukazo, matokeo ya kuwa na mukazo, na namna tunaweza kupata kitulizo kwa kiasi fulani.

a Majina imebadilishwa.