Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

5 Mateso Itaishaka?

5 Mateso Itaishaka?

Juu ya Nini Ni Muzuri Kujiuliza Vile?

Juu kama kuko sababu ya kuamini kuwa mateso itaishaka, ile itafanya tukuwe na mawazo ya muzuri kuhusu maisha na kumuhusu Mungu.

Jambo la Kufikiria

Watu wengi wangependa kumaliza mateso, lakini hawana uwezo wa kutosha wa kufanya vile. Ona mifano yenye kufuata:

Hata kama kumekuwa maendeleo mu mambo ya kinganga . . .

  • Ugonjwa wa moyo unaendelea kuua watu wengi sana.

  • Kansere inaua mamilioni ya watu kila mwaka.

  • Katika gazeti moja (Frontiers in Immunology), David Bloom, mutu mwenye elimu mingi, aliandika hivi: “Watu wanaendelea kupambana na magonjwa ya zamani na ya sasa, na hata wanapambana na magonjwa ingine yenye haijakuwaka tangu zamani.”

Hata kama inchi fulani ziko na utajiri mwingi . . .

  • Kila mwaka, mamilioni ya watoto wanakufa, zaidi sana mu maeneo kwenye watu wako maskini.

  • Mamiliare ya watu wanaishi mu maeneo yenye haiko safi.

  • Mamia ya mamilioni hawana maji safi.

Hata kama watu wengi wanajua haki za wanadamu . . .

  • Ripoti moja ya Umoja wa Mataifa inasema kama, biashara ya kuuzisha watu inaendelea katika inchi na maeneo mingi, na watu wenye wanafanya vile hawapewe malipizi. Ile ni kwa sababu wenye mamlaka ao “hawajue mambo yenye iko inafanyika, ao hawana uwezo wa kutosha wa kumaliza tatizo hilo.”

    IKIWA UNAPENDA KUJUA MINGI ZAIDI

    Angalia video Ufalme wa Mungu Ni Nini? yenye kuwa ku jw.org.

Mambo Yenye Biblia Inasema

Mungu anatuhangaikia.

Anahangaikia maumivu na huzuni yetu.

“[Mungu] hajazarau wala kuchukizwa na mateso ya ule mwenye kukandamizwa; hajamuficha uso wake. Wakati alimulilia amusaidie, alisikia.”​ZABURI 22:24.

“Mumutupie mahangaiko yenu yote, kwa sababu yeye anawahangaikia ninyi.”​1 PETRO 5:7.

Mateso haitaendelea milele.

Biblia inatuambia kama kusudi la Mungu litatimia.

“Mungu . . . atapanguza kila chozi katika macho yao, na kifo hakitakuwa tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu havitakuwa tena.”​UFUNUO 21:3, 4.

Mungu atamaliza mambo yenye inafanya wanadamu wateseke.

Atafanya vile kupitia Ufalme wake, wenye Biblia inaonyesha kama ni serikali ya kweli.

“Mungu wa mbinguni atasimamisha ufalme wenye hautaharibiwa hata siku moja. Na ufalme huo hautapewa watu wengine wowote. . . . Ufalme huo peke yake utasimama milele.”​DANIELI 2:44.