Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Hekima ya Kukuongoza Uwe na Maisha Yenye Furaha

Hekima ya Kukuongoza Uwe na Maisha Yenye Furaha

“Bado ninahuzunishwa na mambo mabaya yanayotokea ulimwenguni kama vile vita, njaa, magonjwa, na kutendewa vibaya kwa watoto​—lakini sasa nina tumaini.”​—RANI. *

Rani alipata furaha ya kweli alipojifunza kwamba, Muumba wetu, Mungu mweza-yote, ndiye chanzo cha hekima ya kweli. Unaposoma makala zinazofuata za gazeti hili, ona jinsi mafundisho ya Mungu yanavyoweza kukusaidia . . .

  • kuwa na familia yenye furaha

  • kuwa na uhusiano mzuri na wengine

  • kuwa na furaha na kuridhika

  • kuelewa kwa nini tunateseka na kufa

  • kuamini kwamba hivi karibuni Muumba wetu atakomesha mateso yote na kutupatia maisha yenye furaha

  • kumjua Muumba wetu na kumkaribia

Pia, utajifunza kwamba hekima kutoka kwa Muumba wetu ni kwa ajili ya kila mtu.

^ fu. 2 Majina katika gazeti hili yamebadilishwa.