Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Hekima Yenye Inaweza Kukuletea Furaha mu Maisha

Hekima Yenye Inaweza Kukuletea Furaha mu Maisha

“Wakati naona mambo ya mubaya mu dunia, kama vile vita, umaskini, magonjwa, na kutendea watoto mubaya, ile inanihuzunisha sana. Lakini, niko na tumaini.”​—RANI. *

Rani alipata furaha ya kweli wakati alijifunza kama ni Muumbaji wetu, Mungu Mweza-Yote, njo anaweza kutupatia hekima ya kweli. Soma habari zenye kufuata, juu uone namna mafundisho yake inaweza kukusaidia . . .

  • ukuwe na familia yenye furaha

  • uishi na wengine kwa amani

  • ujue namna ya kutosheka mu maisha

  • ujue juu ya nini tunatesekaka na kufa

  • ukuwe na tumaini hakika juu ya wakati wenye kuja

  • umujue Muumbaji wetu na ukuwe rafiki yake

Na utaelewa tena kama Muumbaji wetu hapatiake hekima yake kikundi fulani tu ya watu, lakini anaipatiaka bila kulipa kila mutu mwenye anaitafuta.

^ fu. 2 Majina mu hii gazeti imebadilishwa.