Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Namna ya Kuwa Mwenye Kutosheka

Namna ya Kuwa Mwenye Kutosheka

Kila mutu anapenda kuwa na furaha na anapenda kuwa mwenye kutosheka. Na Muumbaji wetu anapenda tujisikie vile, njo maana anatupatia mashauri ya muzuri sana yenye inaweza kutusaidia.

Ufanye Kazi kwa Bidii

“Afanye kazi kwa bidii, akifanya kazi ya muzuri kwa mikono yake, ili akuwe na kitu cha kumupatia mutu mwenye kuwa katika uhitaji.”​—WAEFESO 4:28.

Muumbaji wetu anapenda tutumike kwa bidii na tuone kazi kuwa kitu ya muzuri. Juu ya nini? Mutu mwenye anatumikaka kwa bidii iko na furaha juu anaweza kujitimizia mambo yenye iko nayo lazima na mambo yenye watu wa familia yake wako nayo lazima. Tena, anaweza kusaidia hata mutu mwenye iko na lazima ya kitu fulani. Na mukubwa yake wa kazi atamupenda sana. Njo maana inakuwaka nguvu kwa mufanyakazi muzuri kupoteza kazi yake. Kwa hiyo, maandiko iko na sheria ya kusema kama matokeo ya kufanya kazi kwa bidii ni “zawadi ya Mungu.”​—Muhubiri 3:13.

Ukuwe Munyoofu

“Tuko hakika kwamba tuko na zamiri nyoofu, kwa kuwa tunataka kujiendesha kwa unyoofu katika mambo yote.”​—WAEBRANIA 13:18.

Kama tuko wanyoofu ao waaminifu, tutakuwa wenye kujiheshimia, tutakuwa na amani ya akili, na usiku tutalala kwa amani. Tena, wengine watatutumainia na kutuheshimia. Lakini watu wadanganyifu, wanakosaka ile mambo yote ya muzuri. Tena, zamiri yao inaweza kuwa iko nawasumbua, na kila wakati wanaweza kuwaza kama watu watajua mambo yao ya udanganyifu.

Makuta Isikuwe Jambo ya Maana Sana mu Maisha Yako

“Njia yenu ya maisha ikuwe bila upendo wa feza, wakati munatosheka na vitu vya sasa.”​—WAEBRANIA 13:5.

Tuko na lazima ya makuta juu ya kupata chakula na mambo ingine ya lazima. Lakini, ni hatari sana “kupenda” makuta. Mutu mwenye kupenda makuta, anaweza kutumia wakati yake yote na nguvu yake yote mu kutafuta-tafuta makuta mingi. Ile inaweza kufanya akuwe na matatizo na bibi, ao bwana yake, akose wakati ya kupitisha na watoto wake, na afikie hata kugonjwa. (1 Timoteo 6:9, 10) Zaidi ya ile, mutu mwenye anapendaka makuta, anaweza kuwa mudanganyifu. Mutu mumoja mwenye hekima alisemaka hivi: “Mutu muaminifu atapata baraka nyingi, lakini mwenye anaharakisha kupata utajiri, hatakosa kuwa na hatia.”​—Mezali 28:20.

Chagua Elimu ya Muzuri Sana

“Linda hekima yenye kutenda na uwezo wa kufikiri.”​—MEZALI 3:21.

Elimu ya muzuri, inatusaidia tukuwe watu wenye kutegemeka na wazazi wazuri. Lakini elimu tu yenye tunapata ku masomo haiwezi kutusaidia kila wakati kupata kila kitu yenye tuko nayo lazima na kutupatia furaha. Kama tunapenda kabisa kupata matokeo ya muzuri mu mambo yote yenye tuko nafanya, tuko na lazima ya elimu yenye Mungu anatupatia. Maandiko inasema hivi juu ya mutu mwenye anamusikilizaka Mungu: “Kila jambo lenye anafanya, litafanikiwa.”​—Zaburi 1:1-3.