Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Teknolojia Iko na Matokeo Gani Juu ya Uwezo Wako wa Kujifunza?

Teknolojia Iko na Matokeo Gani Juu ya Uwezo Wako wa Kujifunza?

Watu wako naendelea kujifunza sana, ikuwe kwa ajili ya masomo, kwa ajili ya kazi, ao kwa ajili ya mambo ingine. Teknolojia inaweza kusaidia watu wajifunze. Tofauti na zamani, leo ni mwepesi sana kupata habari mingi bila hata kutoka ku nyumba na uko mu kiti yako tu.

Lakini, watu wengi wenye wanatumia sana teknolojia wamevumbua kama . . .

  • wako na magumu ya kukaza akili juu ya mambo yenye wako wanasoma.

  • wako na magumu ya kukaza akili juu ya jambo moja mu ileile wakati.

  • wanajisikia kuwa wenye kuchoka wakati wako wao peke.

MAMBO UNAPASWA KUJUA

KUSOMA

Watu wenye mara mingi wanatumia sana vyombo vya kielektroniki, wakati fulani wanakosaka uvumilivu wa kusoma habari ao kitabu yote. Kwa hiyo, wanaangalia tu mbiombio juu ya kupata wazo kubwa na basi.

Kusoma haraka-haraka, kunasaidia wakati unapenda kupata jibu ya haraka ku ulizo fulani. Lakini, inaweza kukuzuia kuelewa kwa undani zaidi habari fulani.

JAMBO YA KUFIKIRIA: Ni kwa kiasi gani unaweza kusoma habari za murefu-murefu? Juu ya nini tunaweza kusema kama kusoma habari fulani kwa uangalifu kunaweza kukusaidia kujifunza muzuri zaidi?​—MEZALI 18:15.

KUKAZA UANGALIFU

Watu fulani wanasema kama teknolojia, inawapatia uwezo wa kufanya mambo mbili wakati ileile. Kwa mufano, kuandikia marafiki ujumbe fulani na huku wako wanajifunza. Lakini, wakati akili yao inagawanyika ni nguvu sana kufanya muzuri mambo yenye wako wanafanya zaidi sana kama ile mambo inaomba kukaza akili.

Juu ya kukaza akili, inaomba kuwa na sifa ya kujizuia. Ile inaweza kukusaidia kujifunza. Kijana moja mwenye anaitwa Grace, anasema hivi: “Kukaza akili juu ya jambo moja kunakusaidia kufanya makosa kidogo na kunakusaidia usihangaike sana. Nimejifunza kama ni jambo ya lazima sana kukazia uangalifu jambo moja na kuepuka kufanya mambo mingi mu wakati moja.”

JAMBO YA KUFIKIRIA: Unawaza kufanya mambo mingi mu wakati moja, kunakuzuia kuelewa muzuri habari yenye uko nasoma na kunakuzuia kukumbuka mambo yenye uko najifunza?​—MEZALI 17:24.

KUJISIKIA KUWA WEYE PEKE

Watu fulani, hawajisikiake muzuri wakati wako wao peke mu fasi yenye iko ya kimya, njo maana wanakimbiliaka teknolojia juu ya kujifurahisha. Mwanamuke mumoja mwenye anaitwa Olivia, anasema hivi: “Siwezake kupitisha dakika 15 bila kuona ku telefone yangu, tablete, ao kuangalia televizyo. Juu kama sifanye vile, inanichokeshaka.”

Lakini kusema kweli, wakati mutu iko yeye peke ile inamupatia nafasi ya muzuri zaidi ya kufikiri kwa uzito juu ya mambo ya lazima, na kufanya vile kunasaidiaka mutu kujifunza. Ile haisaidie tu vijana, lakini pia watu wakubwa.

JAMBO YA KUFIKIRIA: Saa yenye uko weye peke, je, unatumiaka ile wakati ili kufikiri?​—1 TIMOTEO 4:15.

MAMBO UNAWEZA KUFANYA

CHUNGUZA MUZURI NAMNA UNATUMIKISHA TEKNOLOJIA

Ni mu njia gani unaweza kutumikisha teknolojia ili kusaidia uwezo wako wa kufikiri uendelee kuwa muzuri tena zaidi? Namna gani teknolojia inaweza kuvuruga uwezo wako wa kukaza akili juu ya jambo fulani na pia wa kujifunza?

KANUNI YA BIBLIA: “Linda hekima yenye kutenda na uwezo wa kufikiri.”​—MEZALI 3:21.