Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAGUMU INAYALA MU DUNIA

4 | Ulinde Tumaini Yako

4 | Ulinde Tumaini Yako

JUU YA NINI NI JAMBO YA MAANA?

Magumu yenye kuwa mu hii dunia inaweza kufanya watu wahangaike kimwili na kihisia. Wengi wenye wameteseka na ile magumu wanawaza kama hali haitabadilikaka. Ile inafanya watende namna gani?

  • Wamoja hawapende hata kuwaza juu ya wakati wenye kuja.

  • Wengine wanakunywa pombe ao wanatumia dawa za kulewesha juu ya kusahau magumu yao.

  • Na wengine wanapenda hata kufa kuliko kuishi. Wanajiuliza, “Juu ya nini tuendelee kuishi?”

Mambo Yenye Unapaswa Kujua

  • Magumu fulani yenye unapambana nayo inaweza kuwa ya wakati kidogo tu na mambo inaweza kubadilika na kuwa muzuri, mu njia yenye hauwazie.

  • Hata kama magumu yako haiishe, kuko mambo fulani yenye unaweza kufanya yenye inaweza kukusaidia uvumilie.

  • Biblia inatoa tumaini ya kweli kabisa. Inaonyesha nini njo itamaliza magumu ya wanadamu.

Mambo Yenye Unaweza Kufanya Sasa

Biblia inasema hivi: “Musihangaike hata kidogo juu ya kesho, kwa maana kesho itakuwa na mahangaiko yake yenyewe. Kila siku iko na matatizo yake yenye yanaeneana na siku hiyo.”​—Matayo 6:34.

Usihangaike sana juu ya kesho. Usihangaike kupita kiasi juu ya mambo yenye inaweza kutokea kesho mupaka ufikie kushindwa kufanya mambo yenye unaweza kufanya leo.

Kama unaanza kuogopa juu ya mambo ya mubaya yenye inaweza kutokea, ile itafanya tu uhangaike tena zaidi na itaregeza tumaini yako juu ya wakati ya muzuri yenye kuya.

Biblia Inatupatia Tumaini ya Kweli

Muandikaji fulani wa zaburi alisemaka hivi wakati alikuwa anasali kwa Mungu: “Neno lako ni taa ya muguu wangu, na mwangaza wa njia yangu.” (Zaburi 119:105) Ona mambo yenye kuonyesha kama njo vile Biblia, Neno ya Mungu, inakuwaka kabisa.

Usiku, taa inaweza kutusaidia tujue fasi kwenye tuko tunaenda. Ni vile pia na Biblia. Mu Biblia muko mashauri ya hekima yenye inaweza kutuongoza wakati tunataka kukamata maamuzi fulani ya nguvu.

Taa inaweza kuangazia njia yetu na inaweza kutusaidia kuona mbali zaidi. Vilevile, Biblia inaweza kuangazia mawazo yetu juu tuone kama mbele kuko tumaini.