Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

HADITHI YA 11

Upinde wa Mvua wa Kwanza

Upinde wa Mvua wa Kwanza

UNAJUA jambo la kwanza ambalo Nuhu alifanya wakati yeye na jamaa yake walipotoka katika safina? Alimtolea Mungu zawadi. Unaweza kumwona akifanya hivyo katika picha iliyo chini. Nuhu alitoa zawadi hiyo ya wanyama ili amshukuru Mungu kwa kuokoa jamaa yake katika gharika kuu.

Unadhani Yehova alipendezwa na zawadi hiyo? Ndiyo. Alimwahidi Nuhu kwamba hangeuharibu ulimwengu tena kwa gharika.

Upesi nchi yote ikakauka, Nuhu na jamaa yake wakaanza kuishi tena nje ya safina. Mungu akawabarikia na kuwaambia: Zaeni watoto wengi. Mwongezeke mpaka watu waishi pote duniani.’

Lakini baadaye, labda watu wangeogopa kwamba gharika kama hiyo ingetokea tena. Basi Mungu alitoa kitu cha kukumbusha watu ahadi yake kwamba hataifunika tena dunia yote kwa maji. Unajua ni kitu gani? Upinde wa mvua.

Umepata kuuona? Unaona mmoja katika picha hii?

Mungu aliahidi hivi: Watu wote na wanyama hawataharibiwa tena kwa gharika. Ninaweka upinde wangu wa mvua katika wingu. Upinde wa mvua utakapoonekana, nitauona nikumbuke ahadi yangu.’

Basi unapoona upinde wa mvua, unakukumbusha nini? Ahadi ya Mungu kwamba hatauharibu ulimwengu tena kwa gharika kuu.