Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

HADITHI YA 43

Yoshua Anakuwa Kiongozi

Yoshua Anakuwa Kiongozi

MUSA anataka kuingia Kanaani pamoja na Waisraeli. Hivyo anauliza hivi: ‘Yehova, uniruhusu nivuke Mto Yordani, niione nchi nzuri.’ Lakini Yehova anasema: ‘Basi! usiseme tena hivyo?’ Unajua kwa nini Yehova alisema hivyo?

Ni kwa sababu ya jambo lililotokea wakati Musa alipoupiga mwamba. Kumbuka, yeye na Haruni hawakumheshimu Yehova. Hawakuwaambia watu kwamba ni Yehova aliyekuwa akiwaletea maji katika mwamba ule. Kwa sababu hiyo Yehova alisema hangewaruhusu waingie Kanaani.

Basi miezi michache baada ya Haruni kufa Yehova anamwambia Musa hivi: ‘Mchukue Yoshua umsimamishe mbele ya E·le·aʹzari kuhani na watu. Na mbele ya wote mwambie kila mtu kwamba Yoshua ndiye kiongozi mpya.’ Musa anafanya kama Yehova anavyosema, kama unavyoona katika picha.

Kisha Yehova anamwambia Yoshua hivi: ‘Uwe hodari, usiogope. Utawaingiza Waisraeli katika nchi ya Kanaani niliyowaahidi, mimi nitakuwa na wewe.’

Baadaye Yehova anamwambia Musa apande juu ya Mlima Nebo katika nchi ya Moabu. Musa anatazama ng’ambo ya Mto Yordani na kuiona nchi nzuri ya Kanaani. Yehova anasema hivi: ‘Hii ndiyo nchi niliyoahidi kuwapa wana wa Ibrahimu, Isaka na Yakobo. Nimekuruhusu uione, lakini sitakubali uingie ndani yake.’

Huko juu ya Mlima Nebo Musa anakufa. Alikuwa mwenye miaka 120. Alikuwa bado ana nguvu, macho yake yalikuwa bado yakiona vizuri. Watu wanahuzunika sana na kulia kwa sababu Musa amekufa. Lakini wanafurahi kuwa na Yoshua kiongozi wao mpya.