Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

HADITHI YA 64

Sulemani Anajenga Hekalu

Sulemani Anajenga Hekalu

KABLA Daudi hajafa, alimpa Sulemani ramani ya Mungu ya kujenga hekalu la Yehova. Katika mwaka wa nne wa kutawala kwake, Sulemani anaanza kujenga hekalu, linamalizwa baada ya miaka saba na nusu. Makumi ya maelfu ya wanaume wanajenga hekalu hilo. Na pesa nyingi sana zinatumiwa kulijenga kwa sababu dhahabu na fedha nyingi zinatumiwa ndani.

Anaagiza sanduku la agano liwekwe katika chumba cha ndani cha hekalu, na vitu vingine vilivyowekwa katika hema vinawekwa katika chumba kingine.

Hekalu hilo linapomalizika, kunakuwa na sherehe kubwa. Sulemani anapiga magoti mbele ya hekalu na kusali, kama unavyomwona katika picha. ‘Hata mbingu yote haikutoshi wewe,’ Sulemani anamwambia Yehova, ‘namna gani hekalu dogo hili. Lakini, Ee Mungu, tafadhali wasikilize watu wako wanaposali kuelekea mahali hapa.’

Sulemani anapomaliza sala yake, moto unashuka kutoka mbinguni. Unazichoma dhabihu za wanyama zilizotolewa. Na nuru yenye kung’aa kutoka kwa Yehova inajaa hekalu. Hiyo inaonyesha kwamba Yehova anasikiliza, na kwamba anapendezwa na hekalu na sala ya Sulemani. Badala ya kwenda kuabudu katika hema, watu wanakwenda katika hekalu.

Sulemani anatawala kwa hekima muda mrefu, na watu wanafurahi. Lakini Sulemani anaoa wanawake wengi wa nchi nyingine wasiomwabudu Yehova. Unaweza kumwona mmoja wao akiabudu mbele ya sanamu? Mwishowe wake zake wanamgeuza Sulemani, anaabudu miungu mingine. Unajua yanayotokea Sulemani anapofanya hivyo? Anakuwa mkali, na watu hawana furaha tena.

Kwa hiyo Yehova anamkasirikia Sulemani, naye anamwambia hivi: ‘Nitakunyang’anya ufalme nimpe mwingine. Sitafanya hivyo wakati wa maisha yako, bali wakati wa utawala wa mwanao. Ebu tuone hayo yanavyokuwa.