Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

HADITHI YA 99

Katika Chumba cha Juu

Katika Chumba cha Juu

SASA ni usiku wa Alhamisi, zimepita siku mbili. Yesu na mitume wake 12 wamekuja kwenye chumba kikubwa hiki cha juu ili wale chakula cha Kupitwa. Yule mwanamume unayeona akiondoka ni Yuda Iskariote. Anakwenda kuwaambia makuhani namna ya kumkamata Yesu.

Jana, Yuda aliwaendea akawauliza: ‘Mtanipa nini nikiwasaidia kumkamata Yesu?’ Wakasema: ‘Vipande 30 vya fedha.’ Basi Yuda sasa anakutana na watu hao ili awaongoze kwa Yesu. Je! si jambo baya hilo?

Chakula cha Kupitwa ndiyo sasa chamalizika. Lakini Yesu anaanza chakula kingine cha pekee. Anawapa mitume wake mkate na kusema: ‘Uleni, kwa sababu unamaanisha mwili wangu utakaotolewa kwa ajili yenu.’ Kisha anawapa kikombe cha divai na kusema: ‘Nyweni, kwa sababu kinamaanisha damu yangu, itakayomwagwa kwa ajili yenu.’ Biblia yakiita ‘chakula cha Bwana cha jioni.’

Waisraeli walikula chakula cha Kupitwa kiwakumbushe wakati malaika wa Mungu ‘alipozipita’ nyumba zao huko Misri. Lakini sasa Yesu anataka wafuasi wake wamkumbuke, na namna alivyowatolea uhai wake.

Baada ya kula Chakula cha Bwana cha Jioni, Yesu anawaambia mitume wake wawe hodari na kuwa na imani yenye nguvu. Mwishowe, wanamwimbia Mungu nyimbo kisha wanaondoka. Ebu tuone wanakokwenda.