Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SEHEMU YA 8

Unabii wa Biblia Unatimizwa

Unabii wa Biblia Unatimizwa

Biblia inasimulia hadithi ya mambo yaliyotokea zamani na pia yatakayotokea wakati ujao. Wanadamu hawawezi kutabiri mambo ya wakati ujao. Ndiyo sababu twajua kwamba Biblia imetoka kwa Mungu. Biblia yasema nini juu ya wakati ujao?

Inasema juu ya vita kuu ya Mungu. Katika vita hiyo Mungu ataisafisha dunia kwa kuondoa ubaya wote na watu wabaya, lakini atalinda wale wanaomtumikia. Yesu Kristo, mfalme wa Mungu atahakikisha kwamba watumishi wa Mungu wanafurahia amani na furaha, na kwamba hawatakuwa wagonjwa tena kamwe wala kufa.

Twaweza kufurahi kwa vile Mungu atafanya paradiso mpya hapa duniani, sivyo? Lakini lazima tufanye jambo fulani iwapo twataka kuishi katika paradiso hiyo. Katika hadithi ya mwisho ya kitabu hiki tunajifunza yanayotupasa kufanya ili tuje tufurahie mambo mazuri ajabu ambayo Mungu amewekea wale wanaomtumikia. Basi soma Sehemu ya 8 ujue ambayo Biblia inatabiri juu ya wakati ujao.

 

KATIKA SEHEMU HII

HADITHI YA 114

Mwisho wa Mabaya Yote

Kwa nini Mungu analituma jeshi lake likiongozwa na Yesu katika vita vya Har—Magedoni?

HADITHI YA 115

Paradiso Mpya Duniani

Wakati fulani watu waliishi katika Paradiso, hilo litatukia tena.

HADITHI YA 116

Tunavyoweza Kuishi Milele

Je inatosha kumjua Yehova na Yesu? Ikiwa sivyo, ni nini kingine kinachohitajiwa?