Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

HADITHI YA 114

Mwisho wa Mabaya Yote

Mwisho wa Mabaya Yote

UNAONA nini hapa? Jeshi juu ya farasi weupe. Lakini tazama wanakotoka. Wanatoka mbinguni juu ya mawingu! Je! kuna farasi huko mbinguni?

Hakuna, hao si farasi halisi. Twajua hivyo kwa sababu farasi hawawezi kukimbia katika mawingu, sivyo? Lakini Biblia inasema juu ya farasi mbinguni. Unajua sababu yake?

Ni kwa sababu wakati mmoja farasi walitumiwa sana katika vita. Hivyo Biblia inaposema watu wamepanda farasi wakitoka mbinguni, inaonyesha Mungu ana vita atakayopigana na watu duniani. Unajua mahali pa vita hiyo? Ni Har–Magedoni. Vita hiyo itaondoa mabaya yote duniani.

Yesu Ndiye ataongoza vita hiyo katika Har–Magedoni. Kumbuka, Yehova amechagua Yesu awe mfalme wa serikali Yake. Ndiyo sababu Yesu anavaa kofia ya mfalme. Nao upanga unaonyesha kwamba ataua adui wote wa Mungu. Je! tushangae kwa vile Mungu ataharibu watu wote wabaya?

Tazama tena Hadithi ya 10. Waona nini hapo? Gharika kuu iliyoharibu watu wabaya. Nani alileta Gharika hiyo? Yehova Mungu. Sasa tazama Hadithi ya 15. Jambo gani linatokea hapo? Sodoma na Gomora inaharibiwa kwa moto alioleta Yehova.

Fungua Hadithi ya 33. Angalia linalowapata farasi hao na magari ya vita ya Wamisri. Nani alifanya maji hayo yawaangukie? Yehova. Alifanya hivyo ili alinde watu wake. Itazame Hadithi ya 76. Utaona hapo Yehova aliacha hata watu wake, Waisraeli, waharibiwe kwa sababu ya ubaya wao.

Hivyo, basi, tusishangae kwa vile Yehova atatuma majeshi yake ya mbinguni aondoe mabaya yote duniani. Lakini fikiria hayo yatakuwa na maana gani! Fungua ukurasa mwingine tuone.