Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Mamilioni ya Viumbe Roho

Mamilioni ya Viumbe Roho

Biblia inasema kwamba kuna roho wengi. Yehova mwenyewe ni roho.—Yohana 4:24; 2 Wakorintho 3:17, 18.

Wakati mmoja Yehova alikuwa peke yake katika ulimwengu wote mzima. Kisha akaanza kuumba viumbe wa roho wanaoitwa malaika. Malaika wana nguvu na akili kuliko wanadamu. Yehova aliwaumba malaika wengi. Katika maono, Danieli mtumishi wa Mungu aliona malaika milioni mia moja.—Danieli 7:10; Waebrania 1:7.

Malaika hao waliumbwa na Mungu hata kabla hajaiumba dunia. (Ayubu 38:4-7) Malaika hao si watu waliokuwa wakiishi hapa duniani na baadaye wakafa na kwenda mbinguni.

Roho Mkuu Zaidi, Yehova, aliumba mamilioni ya viumbe wa roho