Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Uasi Unatokea Mbinguni

Uasi Unatokea Mbinguni

Wakati Shetani alitumia nyoka juu ya kuzungumuza na Eva, Eva naye alimuasi Mungu

Viumbe wote wenye Yehova aliumba walikuwa watu wazuri. Kisha malaika mumoja aligeuka na kuwa mutu mubaya. Jina yake Shetani Ibilisi. Shetani alipenda watu ku dunia wamuabudu, kuliko kumuabudu Yehova. Hivi njo mambo ilikuwaka:

Mu bustani ya Edeni, mulikuwaka miti ya mingi yenye ilikuwaka natoa matunda ya butamu. Yehova aliambia Adamu na Eva kama wanaweza kula matunda ya ile miti yote. Lakini aliwaambia kama hawapaswe kula matunda ya muti moja. Aliwaambia kama ikiwa wanakula matunda ya ile muti, watakufa.​—Mwanzo 2:9, 16, 17.

Siku moja Eva alikuwaka yeye peke, kisha nyoka ikaanza kuzungumuza naye. Kusema kweli, haiko nyoka njo ilikuwaka nazungumuza naye. Shetani Ibilisi njo alifanyaka ionekane sawa vile nyoka njo iko nasema. Shetani aliambia Eva kama akikula matunda ya ile muti yenye Mungu aliwakataza, atakuwa na hekima sawa vile Mungu. Na tena, alimuambia kama hatakufa. Lakini ile mambo mbili yenye Shetani alisema, ilikuwa ya uongo. Hata vile, Eva aliamini mambo yenye Shetani alimuambia na akakula ile tunda. Kisha, akapatia Adamu, naye akakula.​—Mwanzo 3:1-6.

Ile habari ya kweli inatufundisha kama Shetani ni muasi na ni muongo. Aliambia Eva kama hatakufa ikiwa anakosa kumutii Mungu. Lakini ile ilikuwa uongo. Eva alikufaka, na Adamu naye alikufaka. Shetani yeye hakukufaka. Lakini, atakufaka tu juu alifanyaka zambi. Kwa sasa angali muzima na anaendelea kudanganya wanadamu. Angali muongo, na iko nafanya yake yote juu ya kuchochea watu wavunje sheria za Mungu.​—Yohana 8:44.

Malaika Wengine Wanaasi

Kisha, malaika wengine waligeuka na kuwa wabaya. Wale malaika walionaka wanamuke wa sura ya muzuri ku dunia na wakapenda kufanya nao ngono. Wakashuka ku dunia na kuvala mwili ya wanadamu. Kisha wakaanza kujikamatia wanamuke. Lakini Mungu hakuwaumbaka juu wafanye vile.​—Mwanzo 6:1, 2; Yuda 6.

Malaika wabaya walikuya ku dunia juu ya kufanya ngono na wanamuke

Tena ile ililetea wanadamu magumu ya mingi. Bibi za wale malaika walizala watoto wenye hawakukuwa sawa watoto wengine. Wale watoto walikuwa warefu sana, wakali, na hawakukuwa na huruma. Dunia iliharibika sana mupaka Yehova akaamua kuleta Garika juu ya kuharibu watu wabaya. Noa na familia yake njo tu waliokokaka juu walikuwaka watu wazuri.​—Mwanzo 6:4, 11; 7:23.

Lakini malaika wabaya hawakukufaka. Walirudiaka mbinguni. Hata vile, Mungu aliwapatia malipizi. Hakuwaruhusu wachangane na malaika wengine waaminifu. Zaidi ya ile, hakuwaruhusu tena wavale mwili ya wanadamu. Na atawaharibu wakati wa hukumu.​—2 Petro 2:4; Yuda 6.

Shetani Anafukuzwa Mbinguni

Shetani na malaika wake wabaya walifukuzwa mbinguni

Ku mwanzo-mwanzo wa miaka 1900, kulitokeaka vita mbinguni. Kitabu ya Ufunuo inaeleza mambo yenye ilipitikanaka: “Na mara moja vita ikatokea mbinguni: Mikaeli na malaika wake wakapigana na ule nyoka mukubwa, na ule nyoka mukubwa na malaika wake wakapigana lakini hawakushinda, na mahali hapakupatikana tena mbinguni kwa ajili yao. Basi ule nyoka mukubwa akatupwa chini, ule nyoka wa zamani, mwenye kuitwa Ibilisi na Shetani, mwenye anapotosha dunia yote yenye kuikaliwa na watu; akatupwa chini katika dunia, na malaika wake wakatupwa chini pamoja naye.”

Mambo ilikuwa namna gani kisha Shetani kutupwa ku dunia? Kitabu ya Ufunuo inasema hivi: “Kwa sababu hiyo mufurahi, ninyi mbingu na ninyi wenye kukaa ndani yake!” Malaika wazuri walifurahi sana juu Shetani na malaika wake, ao roho wake wabaya, hawakukuwa tena mbinguni. Lakini mambo ingekuwa namna gani juu ya watu ku dunia? Biblia inasema hivi: “Ole wa dunia na wa bahari, kwa sababu Ibilisi ameshuka kwenu, akiwa na kasirani kali, akijua kwamba iko na kipindi kifupi cha wakati.”​—Ufunuo 12:7-9, 12.

Shetani na malaika wake wanadaganya na kuletea watu mateso ku dunia. Wale malaika wabaya wanaitwa pepo wachafu. Ni maadui wa Mungu. Wote ni watu wabaya sana.