Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Pepo Wachafu Ni Wauaji!

Pepo Wachafu Ni Wauaji!

Tangu zamani, Shetani na pepo wachafu hawakuwake na huruma na wanatendeaka watu mubaya. Kwa mufano, Shetani aliuaka wanyama na watumishi wa Yobu. Kisha akaua watoto kumi wa Yobu kwa kutokeza “upepo mukali” wenye uliharibu nyumba yenye walikuwaka ndani. Kisha pale, Shetani akamupiga Yobu “kwa majipu yenye maumivu makali kuanzia kikanyangio cha muguu wake mupaka sehemu ya juu ya katikati ya kichwa chake.”​—Yobu 1:7-19; 2:7.

Mu siku za Yesu, mashetani walifanya watu fulani kuwa bubu na vipofu. (Matayo 9:32, 33; 12:22) Walitesa mwanaume fulani na kumufanya ajikate-kate na majiwe. (Marko 5:5) Tena walifanya mutoto mwanaume alalamike, ajitupe chini, na “ajigeuze-geuze.”​—Luka 9:42.

Zamani pepo wachafu waliletea watu magonjwa na kufanya wajigeuze-geuze

Leo, Shetani na pepo wachafu ni wauaji sana kupita hata zamani. Wamekuwa wakali sana tangu wafukuzwe mbinguni. Habari za kutoka mahali mbalimbali mu dunia yote zinaonyesha kama hawana huruma hata kidogo. Wanaletea watu fulani magonjwa. Wanahangaisha watu wengine usiku, kwa kuwafanya wakose usingizi, ao kwa kuwafanya walote ndoto za kuogopesha. Wanatendeaka wengine mubaya kingono. Na tena, wanafanyaka wengine wakuwe waenda-wazimu, waue, ao wajiue.

Leo pepo wachafu wanafanya watu wakuwe wakali sana; wanahangaisha wengine usiku kwa kuwafanya walote ndoto za kuogopesha

Lintina, mwenye anaishi Suriname, anasema kama pepo muchafu, ao roho mubaya aliua watu 16 wa jamaa yake, na alimutesa kimwili na kiakili kwa miaka 18. Kupitia mambo yenye alijionea, anasema kama pepo wachafu “wanafurahiaka kutesa mupaka kifo, watu wenye wamekwisha kufanya kuwa wafungwa wao.”

Lakini Yehova iko na uwezo wa kulinda watu wake juu Shetani asiwatendee mubaya.​—Mezali 18:10.