Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Umutumikie Yehova, Hapana Shetani

Umutumikie Yehova, Hapana Shetani

Siye wote tunapaswa kuchagua ikiwa tutamutumikia Yehova ao Shetani na mashetani wake. Hatuwezi kuwatumikia wote. Uamuzi wa hekima ni kumutumikia Yehova!

Yehova Ni Mwema

Vile tumeona, Mashetani wanafurahiaka kutendea watu mubaya na kuwadanganya. Lakini Yehova haiko vile. Anapenda watu sawa vile baba anapendaka watoto wake. Yeye njo anatoaka “kila zawadi ya muzuri na kila zawadi kamilifu.” (Yakobo 1:17) Hawezi kuima wanadamu kitu yoyote ya muzuri, hata kama itamuomba mambo mingi juu afanye vile.​—Waefeso 2:4-7.

Yesu, Mwana wa Mungu, alionyesha kama anapenda watu kwa kuponyesha magonjwa yao

Fikiria mambo yenye Yesu, Mwana wa Mungu alifanyaka wakati alikuwaka ku dunia. Alisaidiaka bubu waseme na vipofu waone. Aliponyeshaka wenye ukoma na vilema. Alifukuzaka pepo wachafu na kuponyesha kila namna ya ugonjwa. Na hata alitumia nguvu yenye Mungu alimupatia juu ya kufufua wafu.​—Matayo 9:32-35; 15:30, 31; Luka 7:11-15.

Mungu anasemaka tu kweli, hasemake uongo. Hawezi kutudanganya hata kidogo.​—Hesabu 23:19.

Epuka Desturi za Mubaya

Sawa vile inzi yenye inabanwa mu buibui, watu wengi sana wamebanwa mu ushirikina na mafundisho uongo. Wanaogopa wafu, wanaogopa mashetani, wanaogopa laana, wanaogopa wasiwatupie ulozi, na mambo ingine. Wako watumwa wa mafundisho na desturi zenye zinatokana na uongo wa Shetani Ibilisi. Watumishi wa Yehova hawabanwe na ile mambo yote.

Yehova iko na nguvu sana kupita Shetani. Kama unamutumikia, atakulinda juu pepo wachafu wasikutendee mubaya. (Yakobo 4:7) Hata wanakutupia ulozi, haitakukamata. Kwa mufano, mu inchi ya Nigeria, wachawi watatu wa nguvu sana walifanya ulozi juu waue Shahidi fulani wa Yehova mwenye alikatala kutoka mu muji wao. Juu ile ulozi haikumukamata, muchawi mumoja kati ya wale wachawi aliogopa sana, akaenda kwa ule Shahidi, na kumuomba awahurumie.

Waefeso walilunguza vitabu vyao vyote vya uchawi

Kama mashetani wanakusumbua, umuombe Yehova kwa kutumia jina yake na atakulinda. (Mezali 18:10) Lakini juu Yehova akusaidie, unapaswa kuachana na mambo yote yenye iko na uhusiano na uchawi na ibada ya mashetani. Njo vile watumishi wa Mungu wa zamani mu muji wa Efeso walifanyaka. Walikusanyaka vitabu vyao vyote vya uchawi na kuvilunguza. (Matendo 19:19, 20) Watumishi wa Mungu wa leo wanapaswa pia kufanya vile. Wanapaswa kuachana na hirizi, kamba zenye wanavaa juu ya “kujilinda,” vitabu vya uchawi, na kitu ingine yoyote yenye iko na upatano na desturi za kupashana habari na mashetani.

Abudu Mungu wa Kweli

Zaidi ya kuacha ibada ya uongo na kuacha kufanya mambo ya mubaya, kuko mambo ingine yenye unapaswa kufanya juu umufurahishe Mungu. Unapaswa kumuabudu Mungu wa kweli. Biblia inaonyesha namna unaweza kufanya vile:

Ufike ku mikutano ya Kikristo.—Waebrania 10:24, 25

Ujifunze Biblia.—Yohana 17:3

Uhubirie wengine.—Matayo 24:14

Usali kwa Yehova.—Wafilipi 4:6, 7

Ubatizwe.—Matendo 2:41

Ujiunge na Mashahidi wa Yehova

Shetani na mashetani wake wako na watu ku dunia, wenye wanafundishaka mambo ya uongo na kufanya mambo ya mubaya. Lakini Yehova naye iko na watu wake. Wale watu ni Mashahidi wa Yehova. (Isaya 43:10) Mu dunia yote, muko Mashahidi wa Yehova zaidi ya milioni munane. Wote wanajikazaka sana kufanya mambo ya muzuri na kufundisha watu kweli. Mu inchi za mingi, unaweza kukutana nao ku Jumba ya Ufalme na watakukaribisha muzuri sana.

Kazi yao ni kusaidia watu wamutumikie Mungu. Watajifunza na weye Biblia kwako ku nyumba na watakusaidia ujue namna unaweza kumuabudu Mungu mu njia yenye inafaa. Hawatakuomba makuta. Mashahidi wa Yehova wanafurahiaka kufundisha kweli juu wanapenda watu na wanapenda Yehova Mungu.

Mashahidi wa Yehova watakusaidia umutumikie Mungu