Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA KUMI SITA

Shikamana na Ibada ya Kweli

Shikamana na Ibada ya Kweli
  • Biblia inafundisha nini juu ya sanamu za kidini na kuabudu wazazi wa zamani waliokufa?

  • Namna gani Wakristo wanaona sikukuu za kidini?

  • Namna gani unaweza kufasiria wengine mambo unayoamini bila kuwakasirisha?

1, 2. Kisha kutoka katika dini ya uongo ni ulizo gani unalopaswa kujiuliza, na sababu gani ulizo hilo ni la lazima?

WAZIA kama umevumbua kuwa mutu fulani ametia sumu kwa siri mahali ambapo munashota maji ya kunywa. Kwa kweli maisha yenu yako katika hatari. Utakunywa maji hayo? Hapana. Ni wazi, utatafuta maji safi mahali pengine. Lakini hata kisha kupata maji hayo safi unaweza kujiuliza hivi, ‘nimekunywa maji yale yenye sumu?’

2 Ni vilevile juu ya dini za uongo. Biblia inafundisha kama ibada ya dini za uongo imechafuliwa na mafundisho na mazoea machafu. (2 Wakorintho 6:17) Ndiyo sababu unapaswa kutoka katika ‘Babiloni Mukubwa,’ dini zote za uongo duniani. (Ufunuo 18:2, 4) Je, umekwisha kutoka? Ikiwa umekwisha kufanya hivyo, tunakupongeza. Lakini kujitenga na dini ya uongo ao kutoka kati yake haitoshi. Kisha kutoka, unapaswa kujiuliza, ‘Je, ningali ninashikilia jambo fulani nililozoea kufanya nilipokuwa katika dini ya uongo?’ Tuchunguze mifano fulani.

KUABUDU SANAMU NA WAZAZI WA ZAMANI WALIOKUFA

3. (a) Biblia inasema nini juu ya matumizi ya sanamu, na sababu gani inaweza kuwa vigumu kwa watu fulani kukubali mawazo ya Mungu? (b) Unapaswa kufanya nini ikiwa una vitu vinavyopatana na ibada ya uongo?

3 Watu fulani wana sanamu nyumbani ao vitu vingine vya kuabudu kwa miaka mingi. Je, wewe pia unatumia vitu hivyo? Ikiwa ndiyo, labda utaona kama ni vigumu ao haiwezekani kusali bila kutumia vitu vinavyoonekana. Labda hata unavipenda sana vitu hivyo. Lakini, jua kama Mungu ndiye anayeamua namna anapaswa kuabudiwa, na Biblia inafundisha kama Mungu hapendi tutumie sanamu. (Kutoka 20:4, 5; Zaburi 115:4-8; Isaya 42:8; 1 Yohana 5:21) Basi unaweza kuonyesha kama unashikamana na ibada ya kweli kwa kuharibu kila kitu ulicho nacho kinachopatana na ibada ya uongo. Uvione kabisa vitu hivyo kuwa ‘vitu vinavyochukiza’ namna Yehova anavyoviona.​—Kumbukumbu la Torati 27:15.

4. (a) Namna gani tunajua kama kuabudu wazazi wetu wa zamani waliokufa ni kazi bure? (b) Sababu gani Yehova aliwaonya watu wake wasipime kuzungumuza na roho wabaya kwa njia yoyote?

4 Vilevile kuabudu wazazi wa zamani waliokufa ni jambo la kawaida katika dini nyingi za uongo. Mbele ya kujifunza kweli ya Biblia, watu fulani waliamini kama watu waliokufa wanaishi mahali fulani pasipoonekana na wanaweza kuwasaidia watu walio wazima ao kuwatendea vibaya. Labda ulikuwa unajikaza sana kuwatuliza wazazi wako wa zamani waliokufa. Lakini katika Sura ya 6 ulijifunza kama watu waliokufa hawajui lolote na hawaendelei kuishi mahali fulani. Kwa hiyo, ni kazi bure kabisa kujaribu kuzungumuza nao. Habari yoyote ambayo inaonekana kuwa inatoka kwa watu tuliowapenda waliokufa, kwa kweli inatoka kwa mashetani. Ndiyo sababu Yehova aliwaonya Waisraeli wasipime kuzungumuza na watu waliokufa ao kufanya jambo lolote linaloweza kumufanya mutu azungumuze na roho wabaya.​—Kumbukumbu la Torati 18:10-12.

5. Unaweza kufanya nini ikiwa zamani katika dini yako ulikuwa ukitumia sanamu ao kuabudu wazazi wako wa zamani waliokufa?

5 Ikiwa hapo zamani ulikuwa ukitumia sanamu ao kuabudu wazazi wako wa zamani waliokufa, unaweza kufanya nini? Soma na uwaze sana juu ya maandiko yanayoonyesha mawazo ya Mungu juu ya mambo hayo. Sali kwa Yehova kila siku ukimuelezea tamaa yako ya kushikamana na ibada ya kweli, na umuombe akusaidie uwe na mawazo kama yake.​—Isaya 55:9.

WAKRISTO WA KWANZA HAWAKUWA WANAFANYA SIKUKUU YA NOELI

6, 7. (a) Watu wanawaza Noeli ni ukumbusho wa nini, wanafunzi wa Yesu walifanya sikukuu hiyo? (b) Wakati wa wanafunzi wa Yesu, ni nani waliokuwa wanafanya sikukuu ya kuzaliwa?

6 Ibada ya mutu inaweza kuchafuliwa na dini ya uongo kupitia sikukuu zinazopendwa na watu wengi. Tuchukue mufano wa sikukuu ya Noeli. Watu wengi wanawaza Noeli inafanywa ili kukumbuka kuzaliwa kwa Yesu Kristo, na karibu dini zote zinazojiita kuwa za Kikristo zinafanya sikukuu ya Noeli. Hata hivyo, hakuna ushuhuda wowote unaonyesha kama wanafunzi wa Yesu walikuwa wanafanya sikukuu hiyo. Kitabu kimoja (Sacred Origins of Profound Things) kinasema hivi: “Kwa miaka 200 kisha kuzaliwa kwa Kristo, hakuna mutu aliyejua kabisakabisa siku Kristo alizaliwa, na ni watu wachache tu waliotaka kujua.”

7 Hata ikiwa wanafunzi wa Yesu wangejua tarehe kabisa ya kuzaliwa kwake, hawangefanya sikukuu hiyo. Kwa sababu gani? Kwa sababu, kama vile kitabu kimoja (The World Book Encyclopedia) kinasema, Wakristo wa zamani “waliona kufanya sikukuu ya kuzaliwa kwa mutu yeyote kuwa desturi ya kipagani.” Sikukuu za kuzaliwa zinazotajwa katika Biblia ni zile tu za watawala wawili ambao hawakuwa waabudu wa Yehova. (Mwanzo 40:20; Marko 6:21) Tena sikukuu za kuzaliwa zilifanywa ili kuheshimu miungu ya kipagani. Kwa mufano, tarehe 24 mwezi wa 5, Waroma walikuwa wanafanya sikukuu ya kuzaliwa kwa mungu mwanamuke aliyeitwa Diana. Siku ifuatayo, walikuwa wanafanya sikukuu ya kuzaliwa kwa mungu-jua aliyeitwa Apollo. Kwa hiyo, ni wapagani waliokuwa wakifanya sikukuu ya kuzaliwa wala si Wakristo.

8. Juu ya sikukuu ya kuzaliwa, watu waliamini mambo gani ya uongo? Fasiria.

8 Kuna sababu nyingine ambayo ingewafanya Wakristo wa zamani wasifanye sikukuu ya kuzaliwa kwa Yesu. Inaonekana kuwa wanafunzi wake walijua kama watu waliamini mambo ya uongo juu ya sikukuu za kuzaliwa. Kwa mufano, Wagiriki na Waroma wengi wa zamani waliamini kama roho fulani ilikuwa hapo wakati wa kuzaliwa kwa kila mutu na roho hiyo ilikuwa inamulinda katika maisha yake yote. Kitabu kimoja (The Lore of Birthdays) kinasema kama, “roho hiyo ilikuwa na uhusiano wa kiuchawi pamoja na mungu ambaye siku ya kuzaliwa kwake ililingana na siku ya kuzaliwa kwa mutu huyo.” Kwa kweli, Yehova hawezi kufurahishwa na sikukuu yoyote ambayo inamupatanisha Yesu na mambo ya uongo. (Isaya 65:11, 12) Basi, namna gani sikukuu ya Noeli ilianza kufanywa na watu wengi?

NAMNA SIKUKUU YA NOELI ILIVYOANZA

9. Namna gani watu walifikia kuifanya tarehe 25 mwezi wa 12 iwe sikukuu ya kuzaliwa kwa Yesu?

9 Mamia ya miaka kisha Yesu kurudi mbinguni ndipo watu walianza kufanya sikukuu ya kuzaliwa kwake tarehe 25 mwezi wa 12. Lakini Yesu hakuzaliwa tarehe hiyo, inaonekana alizaliwa mwezi wa 10. * Basi, sababu gani watu walichagua 25 mwezi wa 12? Labda kisha miaka kupita, watu fulani waliojiita Wakristo “walitaka tarehe hiyo ipatane na sikukuu ya kipagani ya Waroma ya ‘kuzaliwa kwa jua.’” (The New Encyclopædia Britannica) Wakati wa baridi kali, jua lilipoonekana kuwa linafifia kabisa, wapagani walikuwa wakifanya sikukuu ili kulifanya jua lirudi na kuwaletea joto na nuru. Waliwaza kama jua lilianza kurudi tarehe 25 mwezi wa 12. Viongozi wa kidini walikubali sikukuu hiyo na kuifanya ionekane kuwa ya “Kikristo” ili kuwavuta wapagani wawe Wakristo. *

10. Wakati fulani uliopita, sababu gani watu wengine hawakufanya sikukuu ya Noeli?

10 Imejulikana tangu zamani kama Noeli ilitokana na wapagani. Kwa sababu Noeli haipatani na Biblia, katika miaka ya 1600 ilikatazwa katika Angleterre na sehemu zingine za Amerika wakati ilikuwa ikitawaliwa na Angleterre. Mutu yeyote ambaye hakwenda kazini siku ya Noeli alilipishwa amande. Hata hivyo, bila kukawia, desturi hizo za zamani zilirudi, na zingine mupya ziliongezwa. Noeli ikawa tena sikukuu kubwa, na hivyo ndivyo ilivyo leo katika inchi nyingi. Lakini kwa kuwa Noeli inatokana na dini ya uongo, wale wanaotaka kumupendeza Mungu hawafanyi sikukuu ya Noeli wala sikukuu nyingine yoyote inayotokana na ibada ya kipagani. *

JE, KUJUA NAMNA SIKUKUU FULANI ILIVYOANZA NI KWA LAZIMA KABISA?

11. Sababu gani watu fulani wanafanya sikukuu, hata hivyo, ni jambo gani linalopaswa kuwa la lazima sana kwetu?

11 Watu fulani wanakubali kama sikukuu kama vile ya Noeli zilianzishwa na wapagani, hata hivyo, wanawaza kama si vibaya kuzifanya. Wanawaza si vibaya kwa sababu watu wengi wanapofanya sikukuu hizo hawaoni kama zinapatana na ibada ya uongo. Tena, wanawaza si vibaya kwa sababu vipindi hivyo vinatolea familia nafasi ya kuwa pamoja. Je, wewe pia unawaza hivyo? Labda unawaza hivyo kwa sababu unaipenda familia yako sana, wala si kwa sababu unaipenda dini ya uongo; ndio sababu unaona vigumu kushikamana na ibada ya kweli. Ikiwa ni hivyo, jua kama Yehova, aliyeanzisha familia, anataka usikilizane vizuri na watu wa jamaa yako. (Waefeso 3:14, 15) Lakini unaweza kusikilizana nao bila kuharibu urafiki wako na Mungu. Mutume Paulo alionyesha jambo linalopaswa kuwa la lazima sana kwetu, alisema hivi: “Endeleeni kuhakikisha lile linalokubalika kwa Bwana.”​—Waefeso 5:10.

Unaweza kula bombo inayookotwa katika mufereji wenye uchafu?

12. Toa mufano unaoonyesha kwa nini tunapaswa kuepuka desturi na sikukuu zilizoanzishwa na wapagani.

12 Labda unawaza kama si lazima watu wajue namna sikukuu fulani ilivyoanza. Je, kujua namna sikukuu fulani ilivyoanza ni kwa lazima? Ndiyo! Kwa mufano: Tuseme umeona bombo katika mufereji wenye uchafu. Je, unaweza kuiokota na kuikula? Haiwezekani! Bombo hiyo ni chafu. Kama vile bombo hiyo, sikukuu hizo zinaweza kuonekana kuwa zenye kuvutia, lakini kumbuka kama zimeokotwa mahali pa uchafu. Ili kushikamana na ibada ya kweli, inafaa kuwa na maoni kama nabii Isaya. Yeye aliwaambia waabudu wa kweli hivi: ‘Musiguse kitu chochote kilicho najisi.’​—Isaya 52:11.

TUMIA AKILI ILI USIWAKWAZE WENGINE

13. Ni nini inayoweza kutokea unapokataa kuungana na wengine katika sikukuu fulani?

13 Unapokataa kujiunga na wengine katika sikukuu fulani wanaweza kutaka kujua sababu ya uamuzi wako. Kwa mufano, wafanyakazi wenzako wanaweza kupenda kujua kwa nini hauungani nao katika sikukuu fulani zinazofanywa kazini. Utafanya nini ukipewa zawadi ya Noeli? Ukiikubali unafanya vibaya? Utafanya nini ikiwa bibi yako ao bwana yako ni mutu wa dini ingine? Unaweza kufanya nini ili watoto wako wasijisikie kuwa wamekosewa na kitu kwa sababu hawafanyi sikukuu fulani?

14, 15. Unaweza kufanya ao kusema nini ikiwa mutu fulani anakupa salamu za sikukuu ao anataka kukupa zawadi?

14 Inafaa kutumia akili ili kujua namna ya kufanya ao kujibu unapokutana na hali fulani. Ikiwa mutu fulani anakupa salamu za sikukuu, unaweza tu kumushukuru. Lakini utasema nini ikiwa ni mutu ambaye unaonana naye mara kwa mara ao unatumika pamoja naye? Kwa mutu kama huyo, labda unaweza kumuelezea mengi zaidi. Iwe unamujua mutu ao hapana, usimukwaze kwa maneno yako. Biblia inatushauri hivi: ‘Maneno yenu na yawe yenye neema sikuzote, yenye kukolezwa chumvi, ili mujue jinsi munavyopaswa kumujibu kila mutu.’ (Wakolosai 4:6) Uwe mwangalifu ili usiwakosee watu heshima. Uwaelezee tu uamuzi wako bila kuwakwaza. Uwaelezee waziwazi kama hakuna ubaya wa kutoleana zawadi ao kuwa pamoja na wengine ili kufurahi, hata hivyo ungependa kufanya mambo hayo wakati mwingine.

15 Basi utafanya nini ikiwa mutu fulani anataka kukupa zawadi? Mutu huyo anaweza kusema: “Najua haufanyi sikukuu hii. Hata hivyo, ninapenda kukupa zawadi hii.” Labda utaamua kama kupokea zawadi na kufanya sikukuu ni mambo mawili tofauti. Ikiwa mutu huyo hajui mambo unayoamini, unaweza kumuelezea kwa nini wewe haufanyi sikukuu hiyo. Hilo litamusaidia ajue kwa nini unakubali zawadi yake, lakini wewe hauwezi kuwatolea watu zawadi yoyote siku hiyo. Lakini, ikiwa mutoaji anataka kuonyesha wazi kama wewe haushikamani kabisa na mambo unayoamini ao kama unaweza kuvunja kanuni ya Mungu kwa sababu ya faida fulani za kimwili, si vizuri kukubali zawadi.

UTAFANYA NINI IKIWA WATU WA FAMILIA WANA DINI YAO?

16. Namna gani unaweza kuepuka kuwakwaza watu wa familia juu ya mambo ya sikukuu?

16 Hapa tena inaomba kuepuka kuwakwaza. Si lazima kubishana nao juu ya kila desturi ao sikukuu wanayotaka kufanya. Heshimu mawazo yao, kama vile ungependa pia wao waheshimu mawazo yako. (Mathayo 7:12) Usifanye jambo lolote linaloonyesha kama wewe pia unajiunga nao katika sikukuu. Lakini, usipitishe kiasi juu ya mambo yasiyopatana moja kwa moja na sikukuu hiyo. Hata hivyo, usifanye mambo yatakayosumbua zamiri yako.​—1 Timotheo 1:18, 19.

17. Namna gani unaweza kuwasaidia watoto wako ili wasijisikie kuwa wanakosewa na kitu wanapowaona watoto wengine wanafanya sikukuu?

17 Unaweza kufanya nini ili watoto wako wasijisikie kuwa wanakosewa na kitu kwa sababu hawafanyi sikukuu isiyopatana na Biblia? Ikiwa katika mwaka kuna nyakati za kujifurahisha katika familia jambo hilo linaweza kufanya wasisumbuke wanapoona watoto wengine wanafanya sikukuu. Tena, wazazi wengine wanapanga kuwatolea watoto wao zawadi wakati fulani. Zawadi nzuri zaidi ambayo unaweza kuwapatia watoto wako ni kuwa pamoja nao na kuwaonyesha upendo.

SHIKAMANA NA IBADA YA KWELI

Kushikamana na ibada ya kweli kunaleta furaha kabisa

18. Namna gani kuhuzuria mikutano ya Kikristo kunaweza kukusaidia kushikamana na ibada ya kweli?

18 Ili umupendeze Mungu, achana na ibada ya uongo na shikamana na ibada ya kweli. Inaomba kufanya nini? Biblia inasema hivi: ‘Acheni tufikiriane ili kuchocheana katika upendo na matendo mazuri, bila kuacha kukusanyika pamoja sisi wenyewe, kama vile wengine walivyo na desturi, bali tutiane moyo, na kufanya hivyo zaidi kwa kadiri munavyoona siku ile kuwa inakaribia.’ (Waebrania 10:24, 25) Mikutano ya Kikristo inakutolea nafasi ya kumuabudu Mungu kwa furaha na kwa njia anayokubali. (Zaburi 22:22; 122:1) Kwenye mikutano hiyo, Wakristo waaminifu ‘wanabadilishana vitia moyo.’​—Waroma 1:12.

19. Kwa nini ni lazima kuzungumuzia wengine mambo unayojifunza katika Biblia?

19 Unaweza pia kuonyesha kama unashikamana na ibada ya kweli kwa kuwaambia wengine mambo ambayo unajifunza katika Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova. Kwa kweli, watu wengi ‘wanaugua na kulia’ kwa sababu ya mambo mabaya yanayotendeka duniani leo. (Ezekieli 9:4) Labda unajua watu fulani wanaohuzunika kwa sababu ya mambo hayo. Sababu gani usizungumuze nao juu ya tumaini la wakati ujao ambalo Biblia imekutolea? Ukijiunga na Wakristo wa kweli na kuzungumuza na wengine juu ya mafundisho ya kweli unayojifunza katika Biblia, tamaa yoyote ya kushiriki desturi za dini ya uongo ambayo labda ingali katika moyo wako itamalizika polepole. Jua kama utakuwa na furaha sana na utabarikiwa sana ikiwa unashikamana na ibada ya kweli.​—Malaki 3:10.

^ fu. 9 Walichagua pia tarehe 25 mwezi wa 12 juu ya sikukuu ya Saturnalia. Tarehe 17 mupaka 24 mwezi wa 12, Waroma walikuwa wanafanya sikukuu ya mungu wao wa kilimo. Kwenye sikukuu hiyo ya Saturnalia, watu walikuwa wanakula na kunywa, walijifurahisha sana na kutoleana zawadi.

^ fu. 10 Ili kupata maelezo zaidi ya mawazo ya Wakristo wa kweli juu ya sikukuu zingine zinazopendwa na watu wengi, soma Nyongeza, ukurasa wa 222-223.