Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Yesu Kristo Ndiye Masiya Aliyeahidiwa

Yesu Kristo Ndiye Masiya Aliyeahidiwa

NYONGEZA

Yesu Kristo​—Ndiye Masiya Aliyeahidiwa

ILI kutusaidia tumutambue Masiya, Yehova Mungu aliwaongoza manabii wake wengi waandike habari juu ya kuzaliwa na kufa kwa Mukombozi aliyeahidiwa na pia huduma yake. Yesu Kristo alitimiza unabii wote huo ulioandikwa katika Biblia. Jambo la ajabu ni hili: Mambo yote yaliyotabiriwa, hata madogo, yalitimia. Kwa mufano, acha tuchunguze unabii fulani uliosema tangu zamani juu ya kuzaliwa kwa Masiya na maisha yake ya utotoni.

Nabii Isaya alitabiri kama Masiya angetokea katika kizazi cha Mufalme Daudi. (Isaya 9:7) Unabii huo ulitimia, Yesu alizaliwa katika kizazi cha Daudi.​—Mathayo 1:1, 6-17.

Mika, nabii mwingine wa Mungu alitabiri kama mutoto huyo angezaliwa “Bethlehemu Efratha” na kama mwishowe angekuwa mutawala (Mika 5:2) Wakati Yesu alipozaliwa, huko Israeli kulikuwa na miji miwili iliyokuwa ikiitwa Bethlehemu. Muji mumoja ulikuwa karibu na Nazareti, kaskazini mwa inchi hiyo, na ule muji mwingine ulikuwa karibu na Yerusalemu huko Yudea. Zamani, muji wa Bethlehemu uliokuwa karibu na Yerusalemu, ulikuwa ukiitwa Efratha. Yesu alizaliwa katika muji huo kama vile unabii ulikuwa umesema!​—Mathayo 2:1.

Unabii mwingine wa Biblia ulitabiri kama Mwana wa Mungu angeitwa “kutoka Misri.” Yesu alipokuwa mutoto, alipelekwa Misri. Kisha kifo cha Herode, alirudishwa kutoka Misri, hivyo unabii huo ukatimia.​—Hosea 11:1; Mathayo 2:15.

Kwenye  ukurasa wa 200, chini ya kichwa “Unabii” kuna maandiko yanayoeleza mambo mengi juu ya Masiya. Tafazali, linganisha maandiko hayo na yale yanayopatikana chini ya kichwa “Utimizo.” Kufanya hivyo kutakusaidia uone ukweli wa Neno la Mungu na imani yako itajengwa sana.

Unapochunguza maandiko hayo, kumbuka kama maandiko ya unabii yaliandikwa maelfu ya miaka mbele ya kuzaliwa kwa Yesu. Yesu mwenyewe alisema: “Mambo yote yaliyoandikwa katika sheria ya Musa na katika Manabii na Zaburi juu yangu lazima yatimizwe.” (Luka 24:44) Kama unavyoona mwenyewe katika Biblia yako, unabii huo mbalimbali ulitimia kabisakabisa, bila kukosea!

 [Muchoro kwenye ukurasa wa 200]

UNABII MBALIMBALI JUU YA MASIYA

TUKIO

UNABII

UTIMIZO

Alizaliwa katika kabila la Yuda

Mwanzo 49:10

Luka 3:23-33

Alizaliwa na bikira

Isaya 7:14

Mathayo 1:18-25

Muzao wa Mufalme Daudi

Isaya 9:7

Mathayo 1:1, 6-17

Yehova anamutangaza kuwa Zaburi 2:7 Mathayo 3:17

Mwana wake

Watu wengi wanakosa Isaya 53:1 Yohana 12:37, 38

kumuamini

Anaingia Yerusalemu Zekaria 9:9 Mathayo 21:1-9

juu ya punda

Anasalitiwa na rafiki yake Zaburi 41:9 Yohana 13:18,

Yohana 13:21-30

Anauzishwa kwa vipande Zekaria 11:12 Mathayo 26:14-16

30 vya feza

Anabaki kimya mbele ya Isaya 53:7 Mathayo 27:11-14

washitaki wake

Wanapigia mavazi yake kura Zaburi 22:18 Mathayo 27:35

Anatiwa kwenye muti wa Zaburi 22:7, 8 Mathayo 27:39-43

mateso na anatukanwa

Hakuna mufupa wake Zaburi 34:20 Yohana 19:33, 36

unaovunjwa

Anazikwa pamoja na matajiri Isaya 53:9 Mathayo 27:57-60

Anafufuliwa mbele ya Zaburi 16:10 Matendo 2:24, 27

mwili wake kuoza

Anatukuzwa kwenye mukono Zaburi 110:1 Matendo 7:56

wa kuume wa Mungu